Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

MICHEZO

 Taifa Stars kukipiga na Swaziland:COCAFA


Timu ya Taifa ya Tanzania,Taifa Stars
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imeendelea na mazoezi katika uwanja wa Olympia Park kujiandaa na mchezo wa fungua dimba dhidi Swaziland katika michuano ya COSAFA
Kocha mkuu wa timu ya Taifa Stars Mart Nooij amesema vijana wake wanaendelea vizuri na mazoezi, ikiwa leo ni siku ya pili.
kocha Nooij amesema hali ya uwanja ni nzuri, uwanja una nyasi nzuri hali inayopelekea kikosi chake kufanya mazoezi katika mazingira mazuri.
Akiongelea mchezo wake wa kwanza wa ufunguzi dhidi ya timu ya Taifa ya Swaziland utakaochezwa siku ya jumatatu, amesema anawajua Swaziland ni timu nzuri, mara ya mwisho katika mchezo wa kirafiki walitoka nao sare, hivyo anawaandaa vijana wake kupata ushindi katika mchezo huo.
Kikosi cha Swaziland kina wachezaji mchanganyiko wakiwemo wanaocheza ligi ya nyumbani na baadhi wanaocheza soka la kulipwa nchini Afrika Kusini.
Taifa Stars itacheza mchezo wa kwanza dhidi ya Swaziland katika Uwanja wa Olympia Park siku ya jumatatu.



 Utafiti:Mazoezi yatakuongezea miaka 5 zaidi



Utafiti:Mazoezi yatakuongezea miaka 5 zaidi

Utafiti umeonesha kuwa watu wanaofanya mazoezi ya kila mara wanaishi kwa miaka mitano zaidi ya wale ambao hawafanyi mazoezi yeyote.
Aidha utafiti huo uliowajumuisha watu waliokomaa umebaini kuwa watu walio na umri mkubwa wanaishi maisha marefu zaidi pindi wanaoacha kuvuta sigara.
Utafiti huo wa miaka 11 uliwajumuisha watu wazima 5,700 nchini Norway ulidhibitisha kuwa watu waliofanya mazoezi kwa takriban saa tatu kwa juma wanaishi zaidi ya miaka mitano zaidi ya wale ambao hawakufanya mazoezi yeyote.
Wanasayansi hao wameanzisha kampeini za uhamisisho wa faida za kufanya mazoezi hasa kwa watu wazima.


Utafiti huo wa miaka 11 uliwajumuisha watu wazima 5,700 nchini Norway

Wakiandika katika jarida moja la utabibu wa michezo linalochapishwa nchini Uingereza, wanasayansi hao wanasema kuwa maisha ya
kuketi bila ya kuwa shughuli yeyote inayochemsha damu mwilini inachangia pakubwa kuzorota kwa uwezo wa mwili kuhimili dhoruba ya maambukizo tofauti tofauti haswa mtu anapozeeka.
Chuo kikuu cha Oslo kilithibitisha kufuatia utafiti huo kuwa hata mtu akifanya mazoezi mepesi ni kheri kuliko kukosa mazoezi kabisa.
Takwimu za utafiti zinaonyesha kuwa japo watu wenye umri zaidi ya miaka 65 wakishiriki mazoezi yeyote kwa dakika 150, hiyo itatosha kumweka katika hali nzuri ya kiafya.


Watu wanaofanya mazoezi ya kila mara wanaishi kwa miaka mitano zaidi ya wale ambao hawafanyi mazoezi yeyote

Aidha kwa wale wenye umri kati ya miaka 68 hadi 77 wanahitaji kufanya mazoezi kwa zaidi ya saa moja kwa juma ilikupata manufaa yake.
Kwa ujumla asilimia 40% ya washirika waliofanya mazoezi kwa takriban nusu saa kila siku walikuwa bado hai katika utafiti huo uliodumu kwa miaka 11.
Ripoti hiyo iliongezea kusema kuwa hata wale wazee waliokuwa na miaka 73 walipoanza mazoezi asilimia kubwa ilikuwa hai zaidi ya wenzao ambao hawakufanya mazoezi yeyote.

 


TWIGA STARS KUINGIA KAMBINI JUMAPILI.

  • Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter Share on linkedin
index
Kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Wanawake Tanzania (Twiga Stars), Rogasian Kaijage ametangaza kikosi cha wachezaji thelathini (30) kitakachoingia kambini siku ya jumapili kujiandaa na mchezo wa kufuzu Mataifa Afrika dhidi ya Zambia mwezi Machi mwaka huu.
Kaijage ametangaza program yake ya mazoezi itakayochukua takribani wiki nne (4) ili kuhakikisha wachezaji wanakua tayari kwa ajili ya mchezo huo utakaochezwa kati ya Machi 21, 22 mwaka huu, huku akipanga kucheza mchezo mmoja wa kirafiki kabla ya kuelekea Lusaka Zambia kwenye mchezo wa awali.
Twiga Stars ambayo itakua kambini katika Hosteli za Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF zilizopo Karume, imeingia moja kwa moja katika hatua ya pili kucheza na Zambia kufuatia kuwa na matokeo mazuri katika msimamo wa viwango vya soka la wanawake barani Afrika.
Wachezaji walioitwa ni, Asha Rashid, Esther Chaburuma, Fatuma Bushiri, Fatuma Hassan, Fatuma Mustapha, Fatuma Omari, Eto Mlenzi, Mwajuma Abdallah, Sofia mwasikili, Zena Khamis, Mwanahamis Omar, Fatuma Khatibu, Fadhira Hamad, Anastazia Anthony, Shelder Boniface.
Wengine ni Thereza Yonna, Happines Hezron, Amina Ally, Donizia Daniel, Fatuma Issa, Vumilia Maarifa, Maimuna Hamisi, Najiati Abbasi, Stumai Abdallah, Ziada Ramadhani, Zuwena Aziz, Irene Joseph (Mfunzo – Zanzibar), Dawa Haji Vuai (JKU – Zanzibar), Belina Julius na Amina Ramadhani.

 

 

 

 

Hayatou ataka kuendelea kuongoza Caf





Issa Hayatou, rais wa shirikisho la soka braniAfrika, Caf

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika, Caf, Issa Hayatou anataka kubadili sheria za chombo hicho kuhusu umri wa mwisho katika uongozi, ili aweze kuendelea kugombea.
Caf inataka maafisa wanapotimiza miaka 70 kujiuzulu madaraka lakini mabadiliko yatapendekezwa na kujadiliwa katika mkutano wa shirikisho hilo mwezi Aprili.
Hayatou, mwenye umri wa miaka 68, yuko katika muhula wa saba katika utawala wa Caf, akiwa amechaguliwa mwaka 1998.
"Fifa haina kikomo cha umri kwa wajumbe wake wa kamati kwa hiyo Caf inataka kuleta hoja hiyo kwa maafisa wake," amesema mjumbe wa kamati kuu ya Caf Kwesi Nyantakyi.
Utawala wa sasa wa Hayatou unaishia mwaka 2017 na anataka miaka minne zaidi hadi mwaka 2021, atakapotimiza umri wa miaka 75.
Kifungu katika katiba ya Caf inasema "katika wakati wao wa uchaguzi, wagombea wote waliopendekezwa kuingia katika kamati kuu ya Caf lazima wawe wajumbe wa vyama vya soka katika nchi zao na lazima wewe chini ya umri wa miaka 70."
Lakini kifungu hiki kinaweza kuondolewa endapo pendekezo la kufuta ukomo wa umri litapitishwa katika mkutano mkuu wa Caf, kama linavyotarajiwa.
Mabadiliko ya sheria hii inafuatia mafanikio katika miaka ya hivi karibuni katika kupitisha vifungu vya katiba vinavyopunguza upinzani katika utawala wa Hayatou.
Awali Caf iliweka sheria kwamba wagombea wa nafasi ya urais wanaweza kutoka ndani ya kamati yake ya utendaji, kipengele ambacho kilidhibitiwa kwa karibu na Hayatou. Fifa haina sharti hilo.
Hayatou mzaliwa wa Cameroon, afisa wa zamani wa riadha, tayari ni mjumbe mwandamizi wa muda mrefu katika muundo wa Fifa, ambako anahudumu kama makamu wa rais, na anakabiliwa na wapinzani wachache kutoka Afrika katika nafasi hiyo.

Nahodha,Costa Concordia afungwa jela






Capt.Francesco Schettino ahukumiwa miaka 16 jela

Nahodha wa meli ya Costa Concordiailiyosababisha vifo vya watu watu 32 wakiwemo wafanyakazi wa meli hiyo amehukumiwa kwenda jela.
Kwa mjibu wa hukumu hiyo Nahodha huyo atatumikia kifungo cha miaka 16 jela baada ya kubainika kuwa na makosa ya kuua bila kukusudia.
Francesco Schettino hakuwepo Mahakamani wakati hukumu hiyo ikitolewa. Miaka mitatu iliyopita Meli hiyo ya Costa Concordia iligonga miamba karibu na pwani ya Giglio nchini Italia na kusababisha vifo hivyo.
Hata hivyo Schettino bado anafursa ya kuweza kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.

Francis Cheka : miaka mitatu jela

  • Saa 7 zilizopita
Mshirikishe mwenzako






Francis Cheka mwenye fulana nyekundu akiwa amezingirwa na mataji yake.

Bondia wa kulipwa nchini Tanzania, Francis Cheka, ambaye ni maarufu kwa jina la SMG, amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela na faini ya Sh milioni moja kwa kosa la kumpiga meneja waje wa baa yake , Bahati Kibanda.
Cheka alitiwa hatiani Julai 2 mwaka jana kwa kumpiga na kumsababishia maumivu makali Kibanda ambaye alikwenda hapo kudai fedha zake katika baa aliyokuwa anaifanyia kazi ijulikanayo kwa jina la Vijana Social Hall.
Cheka anayeshikilia mkanda wa WBF alipandishwa Kizimbani katika Mahakama yaHakimu Mkazi mkoa wa Morogoro, kwa shitaka hilo lililosomeka kuwa ni la shambulio la kudhuru mwili na kujeruhi.
Hakimu Mwandamizi wa mahakama ya mkoa wa Morogoro Said Msuya alikubaliana na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka na kuthibitisha shitaka hilo.
Cheka anadaiwa kutenda kosa hilo kwa Kabanda ambaye alikuwa ni Meneja wa baa yake ya Vijana Social iliyopo maeneo ya Sabasaba katika Manispaa ya Morogoro baada ya kudaiwa kutoridhishwa na mahesabu ya mauzo.
Hakimu Msuya alisema kuwa adhabu hiyo ni fundisho kwa mshitakiwa na watu wengine wanaotumia vibaya nguvu zao kwa watu wengine na anatakiwa kumlipa mlalamikaji fidia ya Sh milioni moja.
Pamoja na Cheka kupewa nafasi ya kujitetea, bondia huyo hakutoa maelezo yoyote na kuiachia mahakama hiyo kutoa adhabu inayostahili kwa bondia huyo aliyejizolea sifa kemkem katika ngumi za kulipwa nchini.
Hata hivyo, familia ya Cheka inampango wa kukata rufaa kupinga hukumu hiyo.

TEMEKE yatwaa ubingwa TAIFA CUP








Timu ya Temeke ikipokea hundi

Chama cha kandanda mkoa wa Dar essalaam DRFA, kimeipongeza timu ya Temeke kwa kutwaa Ubingwa wa Taifa Wanawake,baada ya kuifunga Pwani kwa bao 1-0,kwenye mchezo wa fainali uliopigwa jumapili ya Januari 31 kwenye dimba la Azam Complez huko Chamazi.
Katika fainali hiyo iliyohudhuriwa na waziri mwenye dhamana ya michezo Dk.Fenella Mukangara,imeshuhudiwa Temeke ikijipatia bao lake mnamo dakika ya 66 kupitia kwa mchezaji wao Neema Paul.
Temeke walifanikiwa kutinga hatua ya fainali baada ya kuwafunga ndugu zao Ilala kwa mabao 4-0,huku pwani wakitinga hatua hiyo kwa kuifunga Kigoma mabao 3-2,katika michezo ya nusu fainali.
Mshindi amejinyakulia kitita cha shilingi milioni tatu, makamu bingwa sh. milioni mbili, wakati mshindi wa tatu ameondoka na sh. milioni moja katika michuano hiyo.
Mbali na Temeke kubeba ubingwa huo,pia imefanikiwa kutoa mlinda mlango bora, Belina Julius aliyezawadiwa kitita cha shilingi 500,000/-.
Mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu uliwakutanisha, Ilala dhidi ya Kigoma ambapo ilala imefanikiwa kuchukua nafasi ya tatu baada ya kushinda mabao 3-0.
Uongozi wa DRFA,unatoa shukurani kwa mashabiki wa mkoa wa Dar es salaam na maeneo ya jirani,ambao wamejitokeza kwa wingi kushuhudia michuano hiyo,na kuwaomba waendelee na mfumo huo ili kuleta hamasa kwa wachezaji.

Chelsea,Mancity na Totenham nje ya F.A









fa

Manchester City,Chelsea Southampton na Totenham zimeondolewa katika mechi za kombe la FA baada ya kuadhibiwa na timu kutoka daraja la chini la ligi ya EPL.
Timu hizo ambazo zinaongoza katika jedwali la ligi kuu ya Uingereza Zilishangazwa baada ya kushindwa nyumbani na wapinzani wao.
Hii ni mara ya pili kwa mabingwa wa ligi ya Uingereza Mancity kuondolewa nyumbani na Middlesborough ambao walishinda kwa 2-0.








fa

Vilevile kilabu ya daraja la kwanza Bradford City ilionyesha mchezo wa hali ya juu ilipotoka nyuma 2-0 na kuweza kuwashinda viongozi wa ligi ya Uingereza Chelsea 4-2 katika mechi ya FA ilioijaa mbwembwe za aina aina.
Katika uwanja wa Totenham bao la Jeffrey Schlupp lilisaidia Leicester kuishinda Totenham.
Leicester ilikuwa nyuma kwa bao moja kabla ya kusawazisha na kuongeza la ushindi.








fa

Uwanjani Southampton Mshambuliaji Marouane Chamakh alifunga mabao mawili na kuisaidia kilabu ya Crystal palace kupata ushindi wa 3-2 dhidi ya Southampton katika mechi iliokuwa na mchezo mzuri.
Matokeo ya FA
Cardiff 1 - 2 Reading FT
Chelsea 2 - 4 Bradford FT
Derby 2 - 0 Chesterfield FT
Man City 0 - 2 Middlesbrough FT
Preston 1 - 1 Sheff Utd FT
Southampton 2 - 3 Crystal Palace FT
Sunderland 0 - 0 Fulham FT
Tottenham 1 - 2 Leicester FT

Michuano ya kombe la Capital One










Raheem Sterling

Raheem Sterling aliihakikishia Liverpool kucheza nusu fainali za kombe la Capital One huku Chelsea ikibakia vizuri baada ya bao la penalti la Eden Hazard wa Chelsea katika dakika ya 18 kurejeshwa na Sterling katika dakika ya 59.
Chelsea ilipatiwa penalti baada ya Emre Can kumchezea vibaya Hazard.
Hata hivyo, Sterling aliipatia Liverpool bao ililostahili katika mchezo wa kwanza uwanja wake wa nyumbani wa Anfield.
Timu hizo zinarudiana Jumanne, tarehe 27 Januari, 2015.

MARIO BALOTELLI NA VITUKO VYAKE

Mario Balotelli ni mchezaji wa Liverpool alipost picha hii kwenye page yake ya Instagram akiangalia timu yake kupitia tv akiwa nyumbani. Liverpool na Chelsea walipepetana kugombea kikombe cha Capital One na timu hizo zilitoshana nguvu kwa kufungana goli moja kwa moja Balotelli akuweza kuwepo uwanjani kwa vile ni mgonjwa.

Senegal yaibwaga Ghana













Senegal yaichapa Ghana

Mshambuliaji wa Senegal Moussa Sow alifunga bao la mda wa lala salama na kuisaidia Senegal kupata ushindi dhidi ya Black stars ya Ghana.
Mchezaji huyo aliyeingia dakika za mwisho za mechi hiyo alifunga bao lake kunako dakika ya 90 na kuipatia timu yake alama zote tatu.
Mchezaji wa Ghana Andrew Ayew alifunga mkwaju wa Penalti baada ya kiungo wa kati wa Everton Christian Atsu kuangushwa katika eneo la hatari.
Lakini Senegal ilijitahidi na kupiga chuma cha goli la Ghana kupitia mchezaji Kara Mbodj,kabla ya mshambuliaji wa Stoke Mame Biram Diouf kufunga bao la kusawazisha huku Mousa Sow akifunga bao la Ushindi.

Algeria yainyuka Afrika Kusini 3-1














Timu ya soka ya Algeria

Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika, Afcon imeendelea nchini Equatorial Guinea, ambapo timu za kundi C zilipambana kusaka pointi tatu muhimu katika kuendelea na kinyang'anyiro cha taji la michuano hiyo.Timu ya Algeria, walionyesha ubora wao katika kusakata kabumbu, pale walipowachakaza Afrika Kusini mabao 3-1.
Afrika Kusini ndiyo iliyoanza kuliona lango la Algeria katika dakika ya 51 likifungwa na Phala. Algeria ilisawazisha bao hilo kwa mpira aliojifunga Thulani Hlatshwayo katika dakika ya 67, huku Ghoulam na Sliman wakifunga katika dakika ya 72 na 83 kama wanavyofuatana.
Algeria inashika nafasi ya 18 ya ubora katika viwango vya Fifa wakati Afrika Kusini ni ya 52. Kikosi cha Afrika Kusini chenye wachezaji 23, 18 kati yao wanacheza ligi ya ndani ya nchi yao.
Afrika Kusini pia ilikosa goli la penalti kupitia kwa Tokelo Rantie. Na endapo angepata mkwaju huo wa penalti Afrika Kusini ingeoongoza kwa mabao 2-0. Hata hivyo hiyo imebakia katika kumbukumbu tu za mchezo huo.
Mchezo wa mapema hiyo jana usiku, ulizikutanisha timu za Ghana na Senegal, ambapo Senegal iliibuka na ushndi wa mabao 2-1. Kama ilivyokuwa kwa Afrika Kusini, Ghana ndiyo iliyokuwa ya kwanza kuona lango la Senegal kwa mkwaju wa penalti uliofungwa na Andre Ayew dakika ya 14. Hadi mapumziko Ghana ilikuwa mbele kwa bao hilo. Senegal ilibadilika na kuweza kusawazisha dakika ya 58 kupitia kwa mchezaji wake Mame Diouf. Mpambano huo ukionekana kumalizika kwa sare ya 1-1, mchezaji Sow alibadili matokeo kwa kufunga bao katika dakika ya 90 na kuiwezesha Senegal kuibuka mshindi wa mechi hiyo.
Katika kundi C, Algeria na Senegal zina pointi tatu kila moja, huku Ghana na Afrika Kusini zikibakia bila pointi.
Leo ni heka heka kwa kundi D lenye timu za Ivory Coast, Mali, Cameroon na Guinea. Mchezo wa kwanza utazipambanisha Ivory Coast na Guinea, baadaye watafuatiwa na Mali wakimenyana na Cameroon.
Habari nyingine za kimchezo zinamhusu mchezaji mahiri wa Ghana Asamoah Gyan. Mchezaji huyo ana matumaini atashiriki katika mchezo unaofuata kwa timu yake baada ya kukosa mchezo dhidi ya Senegal, kutokana na kuumwa malaria.
Anasema "wamesikitishwa na matokeo ya kufungwa 2-1 na Senegal. Anasema alifikiria wangetumia uzoefu wao". "walitushinikiza, walidhibiti mchezo daki 30 za mwisho na tungelazimisha sare. Lakini tulipoteza umakini na kufungwa goli dakika ya mwisho ya mchezo.
"Nilikuwepo kuipa moyo timu yangu- na tumepoteza leo. Sasa najisikia nafuu- Nazungumza na jopo la madaktari na tutaona kitakachotokea." Ni kauli ya Asamoah Gyana ambaye alikuwa akisumbuliwa na malaria na kukosa mechi ya kwanza kwa timu yake ya Ghana.
Timu ya Algeria, walionyesha ubora wao katika kusakata kabumbu, pale walipowachakaza Afrika Kusini mabao 3-1.
Afrika Kusini ndiyo iliyoanza kuliona lango la Algeria katika dakika ya 51 likifungwa na Phala. Algeria ilisawazisha bao hilo kwa mpira aliojifunga Thulani Hlatshwayo katika dakika ya 67, huku Ghoulam na Sliman wakifunga katika dakika ya 72 na 83 kama wanavyofuatana.
Algeria inashika nafasi ya 18 ya ubora katika viwango vya Fifa wakati Afrika Kusini ni ya 52. Kikosi cha Afrika Kusini chenye wachezaji 23, 18 kati yao wanacheza ligi ya ndani ya nchi yao.
Afrika Kusini pia ilikosa goli la penalti kupitia kwa Tokelo Rantie. Na endapo angepata mkwaju huo wa penalti Afrika Kusini ingeoongoza kwa mabao 2-0. Hata hivyo hiyo imebakia katika kumbukumbu tu za mchezo huo.
Mchezo wa mapema hiyo jana usiku, ulizikutanisha timu za Ghana na Senegal, ambapo Senegal iliibuka na ushndi wa mabao 2-1. Kama ilivyokuwa kwa Afrika Kusini, Ghana ndiyo iliyokuwa ya kwanza kuona lango la Senegal kwa mkwaju wa penalti uliofungwa na Andre Ayew dakika ya 14. Hadi mapumziko Ghana ilikuwa mbele kwa bao hilo. Senegal ilibadilika na kuweza kusawazisha dakika ya 58 kupitia kwa mchezaji wake Mame Diouf. Mpambano huo ukionekana kumalizika kwa sare ya 1-1, mchezaji Sow alibadili matokeo kwa kufunga bao katika dakika ya 90 na kuiwezesha Senegal kuibuka mshindi wa mechi hiyo.
Katika kundi C, Algeria na Senegal zina pointi tatu kila moja, huku Ghana na Afrika Kusini zikibakia bila pointi.
Leo ni heka heka kwa kundi D lenye timu za Ivory Coast, Mali, Cameroon na Guinea. Mchezo wa kwanza utazipambanisha Ivory Coast na Guinea, baadaye watafuatiwa na Mali wakimenyana na Cameroon.
Habari nyingine za kimchezo zinamhusu mchezaji mahiri wa Ghana Asamoah Gyan. Mchezaji huyo ana matumaini atashiriki katika mchezo unaofuata kwa timu yake baada ya kukosa mchezo dhidi ya Senegal, kutokana na kuumwa malaria.
Anasema "wamesikitishwa na matokeo ya kufungwa 2-1 na Senegal. Anasema alifikiria wangetumia uzoefu wao". "walitushinikiza, walidhibiti mchezo daki 30 za mwisho na tungelazimisha sare. Lakini tulipoteza umakini na kufungwa goli dakika ya mwisho ya mchezo.
"Nilikuwepo kuipa moyo timu yangu- na tumepoteza leo. Sasa najisikia nafuu- Nazungumza na jopo la madaktari na tutaona kitakachotokea." Ni kauli ya Asamoah Gyana ambaye alikuwa akisumbuliwa na malaria na kukosa mechi ya kwanza kwa timu yake ya Ghana.

Arsenal yawashangaza mabingwa wa EPL
















Santi Carzola

Santi Carzola alifunga bao moja na kutengeza jengine na kuisadia Arsenal kuicharaza Mancity mabao 2-0 nyumbani Manchester.
Ushindi huo wa Arsenal pia ulisitisha msururu wa kutofungwa wa Mancity wa mechi 12.
Mchezaji wa Uhispania Santi Carzola aliyekuwa moto wa kuotea mbali dhidi ya Mancity alifunga mkwaju wa penalty baada ya beki wa Arsenal Nacho Monreal kuangushwa katika eneo la hatari na beki Vincent Kompany.














Mancity

Arsenal iliongeza bao la pili katika kipindi cha pili baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na Santi Carzola kuwekwa wavuni na Olivier Giroud.
Matokeo hayo yameiwacha City ikiwa na alama 5 chini ya viongozi wa ligi Chelsea.
City na Arsenal walitoka sare ya 2-2 wakati walipokutana kwa mara ya kwanza katika uga wa Emirates mnamo mwezi Septemba

Asamoah Gyan kuikosa mechi na Senegal

















Asamoah Gyan

Nahodha wa timu Ghana Asamoah Gyan anaugua maradhi yanayosemekana kuwa ni malaria na huenda asikipige na Senegal leo.
Shirikisho la soka la Ghana limetoa maelezo kuwa mshambuliaji huyo alikuwa amepumzishwa hospitali katika mji wa Mongomo tangu Jumamosi jioni na kuruhusiwa Jumapili asubuhi ,na inaelezwa kuwa maradhi hayo yametibiwa katika hatua za awali na mchezaji huyo anaendelea vyema.
Na upande wa Senegal,Alain Giresse anapaswa kufanya maamuzi juu ya afya ya Sadio Mane, ambaye alikuwa nje ya dimba kutokana na kigimbi chake kuumia.Sadio ni mchezaji wa timu ya Southampton na alijumuishwa katika kikosi cha Senegal pamoja na kwamba timu yake iligoma kwa maelezo kwamba hatakuwa sawa kiafya.
Lakini Giresse ameendelea kushikilia msimamo wake kwa kusema kama hataweza kucheza katika mechi za awali,itakuwa maraya ya pili kama si ya tatu tutaangalia maendeleo ya hali yake.
Jina moja kubwa linalokosekana katika kikosi cha Senegal,ni mchezaji wa timu ya West Ham mshambuliaji Diafra Sakho,ambaye alikuwa na maumivu ya mgongo na hakuwa sehemu ya kikosi cha timu ya Senegal.Hata hivyo mchezaji mwenziwe wa timu ya Upton Park Cheikhou Kouyate yeye ataungana na kikosi hicho.
Kwa upande wake Sadio yeye,anaeleza kuwa alikuwa na ndoto ya kuichezea timu yake ya taifa katika kombe hilo la mataifa ya Afrika na kipaumbele ni timu ya Taifa na West Ham baadaye.kwa heshima alonayo kwa klabu yake,wanaheshimu uamuzi wake endapo kama asingekuwa na maumivu hayo, ni fursa pekee ambayo mtu yeyote asingependa kuikosa.
Kukosekana kwa Gyan katika kikosi cha taifa lake, yaeza kuwa mtihani kwa kocha wake mpya mGhana Avram Grant aliyewahi kuwa boss wa Chelsea lengo lake ni kuona Black Stars hawafungiki katika michuano hiyo dhidi ya Senegal.
Lakini walau analo chaguo, anaweza kumwita mchezaji wa timu ya Marseille ,mchezaji wa mbele Andre Ayew na pia mchezaji wa timua ya Everton Christian Atsu ama hata Mubarak Wakaso wa timu ya Celtic.

Chelsea yaipa kichapo Swansea


















Diego Costa

Chelsea imeimarisha uongozi wake katika ligi ya Uingereza baada ya kuicharaza kilabu ya Swansea mabao 5 bila jibu katika mechi iliodhibitiwa na chelsea kuanzia mwanzo hadi mwisho.
Kiungo wa kati wa Chelsea Oscar ndiye aliyefungua mtiririko huo wa mabao alipofunga sekunde chache tu baada ya mechi kuanza.
Mshambuliaji hatari wa Chelsea Diego Costa alifanya mambo kuwa magumu kwa Swansea baada ya kupachika bao la pili katika dakika ya 20 kabla ya kuongeza bao jengine katika dakika ya 34.
















Fellaini

Oscar alifunga bao lake la pili na kuiweka Chelsea mbele na mabao 4-0 kufikia mwisho wa kipindi cha kwanza.
Katika kipindi cha pili Swansea ilijitahidi na kiweza kukosa mabao ya wazi lakini ilipofikia dakika ya 79 Schurlle alipafunga bao la tano.
Katika mechi nyengine Manchester United imeibuka mshindi kufuatia msururu wa matokeo mabaya baada ya kuichapa QPR mabao 2-0.
Marouane Fellaini na James Wilson walifunga mabao hayo yaliokuja katika kipindi cha pili katika uwanja wa Loftus Road.
















liverpool

Nayo Liverpool iliendelea kumpa presha kocha wa Aston Villa Paul Lambert baada ya kuishinda Aston Villa na hivyobasi kupata ushindi wa tatu mfululizo.
Borini alifunga bao la kwanza katika dakika ya 24 kabla ya lambert kumaliza kazi katika dakika ya 79.
Haya ndio matokeo ya mechi za jumamosi
Aston Villa 0 - 2 Liverpool
Burnley 2 - 3 Crystal Palace
Leicester 0 - 1 Stoke
QPR 0 - 2 Man Utd
Swansea 0 - 5 Chelsea
Tottenham 2 - 1 Sunderland

Paula Radcliffe kustaafu riadha


















Paula Radcliffe

Mwanariadha Paula Radcliffe raia wa Uingereza anatarajia kustaafu kucheza mchezo huo mwishoni mwa mwezi wanne.
Paula mwenye umri wa miaka 41, ambaye alishinda mara tatu katika michuano ya marathoni ya
Radcliffe, ambae aliweka rekodi ya kukimbi kwa masaa mawili dakika 15 na sekunde 25 katika michuano ya mwaka 2003
Mratibu wa riadha wa London Hugh Brasher. “Amesema tumemteua Paula kushiriki michezo ya marathoni kwa mara mwisho kabla hajapumzika”.
Mbio hizo za marathoni zitafanyika tarehe 26 mwezi wa nne.

Wilfried Bony: Ajiunga rasmi City





















Kifaa Bony

Mshambuliaji wa Wilfried Bony amesaini mkataba wa miaka minne unusu kuichezea timu Manchester City wenye thamani ya £28milion.
Bony amekubali mkataba huu na atavaa jezi namba 14iliyokua ikitumiwa na nyota na Javi Garcia.
Baada kusajiliwa na City Bony ameelezea ni "Ni heshima kubwa kuwa hapa na ni changamoto kwangu".
Mchezaji huyo mwenye miaka 26 alitua ligi ya England mwaka 2013 akijiunga na klabu ya Swansea akitokea Vitesse Arnhem ya Uholanzi kwa ada ya uhamisho ya £12milioni na kuwa moja kati ya wafungaji bora katika ligi kuu.
Kwa uhamisho huu unamfanya Bony kuwa mmoja kati ya wachezaji wa Afrika wanaolipwa pesa nyingi duniani katika mchezo wa soka.

Michuano Afrika:Wasiomudu kupewa tiketi






















Rais wa Guinea ya Ikweta Teodoro Obiang Nguema

Rais wa Guinea ya Ikweta Teodoro Obiang Nguema , amesema yeye mwenyewe atalipa jumla ya tiketi elfu arobaini kwa ajili ya wapenzi wa soka nchini mwake ili waweze kuhudhuria mechi ya Kombe la Mataifa Afrika.
Michuano hiyo inayoanza jumamosi, yalitangazwa kufanyika nchini humo baada ya kuthibitishwa kuwa hayatafanyika morocco kama ilivyopaswa.
Rais Obiang anasema anaona ni wajibu kwake na wengine wenye uwezo kununua tiketi kufanya hivyo akitoa wito wa kujaza viwanja. Ametoa wito kwa wale wenye uwezo wa kuwasaidia masikini kufanya hivyo

YANGA SASA YAWASHITAKI FIFA JAJA, KASEJA NA OKWI

Klabu ya Yanga imechukua uamuzi wa kuwashitaki wachezaji watatu moja kwa moja kwenye Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa).
Yanga imetangaza kuwashitaki kipa Juma Kaseja, kiungo Mganda Emmanuel Okwi na mshambuliaji Jaja raia wa Brazil.Mkurugenzi wa Sheria wa Yanga, Frank Chacha amesema leo wamechukua uamuzi huo kutokana na wachezaji hao kukiuka vifungu vya sheria.“Lakini pia tutaishitaki Simba kwa kuhusika kuvunja vifungu vya kisheria kutokana na kumshawishi Okwi kuvunja mkataba wetu,” alisema Chacha.
Jaja:
Yanga inasema alishindwa kurejea nchini kwa madai ana matatizo ya kifamilia. Lakini wanashangazwa kuwa hajarudi hadi leo na kuna taarifa amepata timu nyingine, hivyo wanashitaki.
Okwi:
Amekiuka sheria kwa kuvunja mkataba, wanaamini hakuwa sahihi na pia Simba ilimshawishi kuvunja mkataba nayo wanaishitaki.
Kaseja:Alishindwa kufuata vipengele vya kikatiba ikiwa ni pamoja na kutokwenda mazoezini wanadai bila ya kuwa na taarifa yoyote

Radamel Falcao ataenda wapi msimu ujao?
























Radamel Falcao kuchezea moja kati ya timu bora msimu ujao

Radamel Falcao atachezea moja kati ya timu bora duniani msimu ujao,hata kama haitakuwa Manchester United, hayo ni maneno ya wakala wa Falcao, Jorge Mendes
Mchezaji huyu mwenye umri wa miaka 28 alitokea Monaco na kujiunga na Man U kwa mkopo mwezi Septemba lakini tangu wakati huo aliifungia Man U magoli matatu pekee.
United wana muda mpaka mwezi June hapo wataamua kama wataendelea naye au la.
Nini maamuzi ya Falcao mwenyewe ?
Falcao mwenyewe ameshaamua kuwa hatarejea Monaco, yaani angependa kubaki United
hata hivyo, akiwa na United Falcao hakuwemo hata kwenye kikosi cha wachezaji 18 walipokutana na Southampton tarehe 11 mwezi huu.
Lois Van gaal amesema uamuzi wake uliegemea kwenye uchaguzi wa wachezaji ambao alihisi kuwa ndio bora zaidi kwa mchezo huo.

Ronaldo atwaa tuzo ya FIFA Duniani 2015
























Cristiano Ronaldo mara baada ya kupatiwa tuzo yake

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo ameibuka mshindi katika tuzo ya FIFA kama mwanasoka bora duniani mwaka huu Ikiwa ni kwa mara ya pili mfululizo.
Tuzo hii iliwajumuisha wachezaji wa soka watatu ambao Lionel Messi, Manuel Neuer na Ronaldo ambaye ameibuka mshindi.
Na mfungaji goli zuri la mwaka tuzo hiyo imechukuliwa na mwanasoka kutoka nchini Colombia James Rodriguez ambapo goli hilo lililovunja rekodi ni lile alilofunga Colombia dhidi ya Uruguay mwaka 2014 katika kombe la dunia.

Maandalizi:Kombe la Mataifa ya Afrika


























Timu ya Taifa ya DRC itakayoshiriki Kombe la Mataifa ya Afrika

Mlinzi wa Orlando Pirates Ayanda Gcaba ameitwa kwenye timu ya taifa ya Afrika Kusini Bafanabafana ili kuziba nafasi ya Patrick Phungwayo.
Bafanabafana inashiriki fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika michuano itakayoanza Januari 17 mwaka huu.
Phungwayo ambaye naye ni mchezaji wa Orlando Pirates alilazimika kurudi nyumbani baada ya kupata majeruhi ambayo hayatamwezesha kuitumikia timu yake ya taifa.
Kocha wa Bafana bafana Epharaim Shakes Mashaba amesema amesikitishwa kwa kumkosa Phungwayo lakini ameonyesha kuwa na matumaini na mbadala wa mchezaji huyo Ayanda Gcaba
wakati huo huo mashabiki wa timu ya taifa ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo nayo itashiriki mashindano hayo wamekuwa na matumaini ya timu yao kufanya vizuri na hata kunyakua kombe hilo.

Messi:''Tetesi za kuhama ni porojo tu''



























Messi na wachezaji wenzake wa Barcelona

Mchezaji mahiri, Lionel Messi anasema kuwa atasalia katika klabu ya Barcelona baada ya kukanusha umbea wa watu kwamba yuko njiani kutoka Barceola.
Messi ambaye ni mshambuliaji wa Barcelona anasisitiza kwamba hataki kuondoka Barca na kusema madai kwamba alimtaka kocha Luis Enrique, kupigwa kalamu ni porojo tupu.
Taarifa za awali zilisema kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alitaka sana kuondoka katika klabu hio kufuatia tofauti kati yake na kocha Enrique.
"sina nia ya kuondoka na kuhamia klabu yoyote kama vile Chelsea au Man City,'' alisema Messi baada ya kuhakikisha timu yake ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Atletico Madrid.
"nimechoshwa sana na umbea wa watu. Sikutaka klabu kumfuta kazi mtu yeyote. ''
Messi, ameteuliwa kuwania tuzo ya mcherzaji bora zaidi duniani, amekuwa akicheza Nou Camp, kwa miaka mingi huku akipata akishinda mataji mengi.


























Messi akipepea uwanjani

'Messi awajibu wadaku na wambea'
''Watu wanavyoongoea untadhani mimi ndiye mkuu wa klabu. Mimi simuulizi mtu yeyote kufanya uamuzi. Kila kilichosemwa ni uongo mtupu na ningetaka watu kufahamu kwamba madai yote yaliyotolewa ni uongo mtupu. ''
Kulikuwa na tetesi kuwa Messi alikuwa njiani kuondoka Barca, kufuatia taarifa kwamba alitofautiana sana na kocha Enrique, ambaye alichukua usukani wa klabu mwaka jana.
Lakini Messi aliongeza kuwa: ''watu wanasema hizi taarifa kwa lengo la kutuvuruga. Yote haya yananiumiza moyo wangu kwa sababu waliyoyasema hayo ni watu wa Barca. Lazima tuungane. ''
Messi alicheza mchezo wa kufana sana wakati Barcelona walipoicharaza mabingwa watetezi wa La Liga Atletico Madrid.

Mchezaji bora Fifa duniani kutangazwa





























Manuel Neuer

Tuzo ya mchezaji Bora wa dunia wa Fifa kwa mwaka 2014 inatarajiwa kutangazwa leo ambapo tayari wachezaji watatu wamechujwa ili kuania tuzo hiyo inayojulikana kwa jina la FIFA Ballon d'Or 2014.



























Lionel Messi na Cristiano Ronaldo

Wachezaji watatu waliobaki kwenye fainali ni pamoja na Christiano Ronaldo ambaye ni mchezaji wa timu ya Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno.
Mwingine ni Lionel Messi mshambuliaji wa Barcelona na mchezaji wa timu ya taifa ya Argentina.
Na wa tatu ni Manuel Neuer Mlinda mlango wa Bayern Munich ambaye pia hudakia timu yake ya taifa ya Ujerumani.

Mchezaji wa kilabu ya Wolfsburg afariki





























Mchezaji Lukaku akimenyana na marehemu Junior Malanda.mchezaji huyo wa miaka 20 alifariki katika ajali ya gari huko Ujerumani

Mchezaji wa safu ya ulinzi ya katikati katika kilabu ya Wolfsburg nchini Ujerumani amefariki katika ajali ya barabarani.
Mchezaji huyo mwenye umri wa mika 20 aliripotiwa kukaa katika kiti cha nyuma cha gari kazkazini Magharibi mwa Ujerumani ambapo kulingana na maafisa wa polisi wa Ujerumani lilikuwa likipelekwa kwa mwendo wa kasi.
Ajali hiyo ilitokea katika eneo la Bundesatobahn 2.
Malanda alitarajiwa kusafari hadi Afrika kusini na wenzake jioni ya leo kwa kambi ya mazoezi.

Bony kuhamia Mancity kwa £30m






























Wlfried Bony

Kilabu ya Uingereza Swansea City imekubali ada ya uhamisho ya takriban pauni milioni 30 kutoka kwa Manchester City ya kumnunua Wilfried Bony, 26.
Meneja wa Swansea, Gary Monk amesema kuwa itahitaji "kitita cha ajabu" kumhamisha Bony kutoka Swansea.





























Wilfried bony na Kocha wa Swansea

Alikuwa mfungaji bora wa mwaka wa kalenda 2014 akipachika mabao 20.
Bony alijiunga na Swansea mwaka 2013 kutoka Vitese Arnhem kwa pauni milioni 12.
Mchezaji huyo kwa sasa yuko na kikosi cha timu ya taifa ya Ivory Coast kujiandaa na michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.

Sanaa ya sarakasi yainua vijana TZ

Nchini Tanzania si jambo la ajabu kuona Watoto na wakubwa wakicheza sarakasi mitaani.lakini sifa hii ya kuwa nchi maarufu kwa sarakasi barani Afrika inatoka wapi, Mwandishi wa BBC alizuru Dar es Salaam kubaini hayo.
































Mcheza sarakasi Raia wa Zimbabwe Winston Ruddel alianza kusaka vipaji kwa ajili ya taasisi yake iitwayo Mama Afrika, kituo chake cha kwanza kilikua jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania, huko alianzisha shule ya Sarakasi, Mama Afrika
































''Awali ilikua kama nilifanya makosa'', anaeleza Ruddel.'' nilipewa Mkataba mjini Las Vegas kwa ajili ya maonyesho ya sarakasi, hivyo nikaja Tanzania kutafuta vijana walio na ufahamu na mchezo wa sarakasi, tukafanya kazi pamoja, lakini wamarekani hawakuvutiwa na vijana wale. Tayari nilishawaahidi mkataba, hivyo nikaanza kuwatafutia kazi.,wishowe,tulipata kazi nyingi zilizonilazimu kufungua shule ili kukidhi mahitaji.ilianza kwa kosa dogo lililozaa mafanikio makubwa''.
































Mmoja kati ya waliofundisha katika shule hiyo, Selemani Mohamedi Nomondo, anasema ''nilianza kunyonganyonga viungo vyangu nikiwa na umri wa miaka mitatu, ikiwa utaanza mapema zaidi, mwili wako utazoea na hutasikia maumivu, kwa kutazama inaonekana ngumu, kuliko uhalisia ulivyo''.
































Maonyesho ya Mama Afrika hutumia muziki katika kazi zake jukwaani, pia shuleni wakati wa mafunzo. Ngoma ni kiini cha mchezo wa sarakasi huwapa wasanii ari ya mchezo na kusaidia katika uchezaji kwa wanakikundi.
































Rajab Zubwa anasema yeye ni mtu wa kwanza kuwa mwanasarakasi '' nilisoma kwa miaka minne nchini China miaka ya 1960.Tanzania na China walikuwa na uhusiano wa karibu wa kisiasa hivyo Serikali zote mbili zilianzisha mafunzo ya kubadilishana, anaeleza'' nilipata faida kubwa nilipokuwa kwenye shule ya Sarakasi na niliporejea nilikuwa mwalimu wa sarakasi.
































Maonyesho ya Mama Afrika mpaka sasa yamefanyika katika mabara matano, ikiwemo mjini New York.kuna maonyesho mengi yanafanyika kwa wakati mmoja , lakini sio rahisi kuwa sehemu ya maonyesho ni wahitimu wanye uwezo wa juu pekee kutoka kwenye shule hiyo hufanikiwa kufika katika hatua ya kimataifa.
































Watoto wanakaribishwa katika shule ya Mama Afrika wakati wa mwisho wa wiki na wanapokua likizo.
































Tangu shule hii ilipoanzishwa mwaka 2003 zaidi ya wanafunzi 300 walimaliza masomo yao.wengi walianza kufanya maonyesho mbali mbali ya sarakasi, wengine walijiunga na Kampuni za sarakasi duniani.
































Pamoja na tamaduni za micheo hii nchini Tanzania, programu za shule hazidhaminiwi na Serikali wala Sekta binafsi, shule ya Ruddel iko maeneo ya Magomeni moja ya eneo waishio watu wengi wa kipato cha chini jijini Dar es Salaam, baada ya kazi ngumu ya mafunzo wanafunzi hupata chakula.
































''Jina langu Tumaini, mimi ni Mshonaji nguo wa Mama Afrika.huwa tunavaa nguo halisi za kiafrika jukwaani, tunatumia vitambaa vizuri ambavyo huvaliwa mitaani.
































Naitwa Deborah Dixon ni mmoja kati ya wasichana wachache ambao hufanya sarakasi kwa mtindo wa kukunjakunja viungo.wasichana wengi hupenda kufanya sarakasi kwa mchezo wa kucheza ngoma kwa sababu ya tamaduni za kifamilia si sawa kwa watoto wao wa kike kutanua miguu na kugalagala kwenye sakafu.kwa upande wangu kukunjakunja viungo ni sanaa .
































Ally Kibwana Ally anasema'' kwangu mimi kuwa na Mama Afrika kunamaanisha kuwa niliweza kuishi kutegemea kipaji changu. Nimetembelea sehemu nyingi duniani na kujifunza mengi.sasa ninatoa ujuzi huo kwa Wanafunzi wengine ili nao waweze kupata nafasi kama mimi''.
































Anaongeza; ''tofauti kubwa kati ya wasanii hapa na maeneo mengine duniani ni kuwa hapa Watu wanafurahia wanachokifanya.Inawezekana tukawa hatuna ujuzi na utaalam kama ilivyo kwa wasanii ya China na Urusi lakini tunanguvu inayotuunganisha na hadhira.''

Stars maboresho kuivaa Rwanda


































Kikosi cha maboresho Stars

Kikosi cha Taifa Stars Maboresho kitacheza mechi ya kirafiki na timu ya Taifa ya Rwanda itakayofanyika Januari 22 mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Mechi hiyo ni sehemu ya programu ya Kocha Mart Nooij kuiandaa timu hiyo kwa ajili ya mechi za mchujo michuano ya Afrika kwa Wachezaji wanaocheza Ligi za Ndani (CHAN).
Mechi za mchujo za michuano hiyo ambayo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Rwanda zinaanza Mei mwaka huu.
Kocha Nooij anatarajia wakati wowote kutangaza kikosi cha timu hiyo inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ambacho kitakusanyika Januari 18 mwaka huu jijini Dar es Salaam, na siku moja baadaye kwenda jijini Mwanza



  Droo kupanga mechi kombe la FA yafanyika



































Mabingwa watetezi wa kombe la FA, wakishangilia ushindi mwaka uliopita.

Droo ya kupanga mechi za raundi ya 4 ya Kombe la FA imefanyika.
Katika mpangilio huo, vigogo Manchester United imepangwa kucheza na timu ya daraja la chini ya Cambridge United.
Mabingwa Watetezi, Arsenal, watakuwa Ugenini kucheza na Brighton au Hove Albion ambayo ipo Daraja la chini ya Ligi Kuu England.
Chelsea itakipiga na Mill wall au Bradford City. Manchester City itapepetana na Middlesbrough
Southampton/Ipswich na Crystal Palace
Blackburn Rovers na Swansea City
Michezo ya raundi ya nne inatarajiwa kupigwa Januari 24 na 25.
NAKO kwenye kombe la mapinduzi
Baada ya kutojulikana kuwa nani atacheza na Simba katika mechi ya robo fainali ya Kombe la Mapinduzi, sasa kila kitu kiko wazi. Simba itaivaa Taifa Jang'ombe katika mechi ya michuano hiyo hatua ya robo fainali hii leo usiku.
Mechi hiyo itachezwa saa 2 usiku kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Siku inayofuata Alhamisi, mechi nyingine ya robo fainali itapigwa jioni, nayo ni kati ya Azam dhidi ya Mtibwa Sugar.
Mechi hiyo inaaminika kuwa moja ya zile ngumu na safi za michuano ya Mapinduzi.
Yanga sasa itacheza mechi yake ya robo fainali dhidi ya maafande wa JKU.
Mechi hiyo itapigwa Alhamisi kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Yanga inakutana na JKU baada ya kumaliza vinara wa kundi A wakiwa na pointi 9. Walipata pointi hizo baada ya kushinda mechi zote tatu katika makundi kwa kujikusanyia mabao tisa, wakiwa hawajafungwa hata moja.
Walikamilisha pointi hizo tisa baada ya kuifunga Shaba kwa bao 1-0 katika mechi tamu na ya kuvutia jana usiku.
Bao la mchezo huo lilifungwa na Mbrazil Andrey Coutinho.



SINGANO AIVUSHA SIMBA ROBO FAINALI KOMBE LA MAPINDUZI

SAM_4333

Kikosi cha Simba sc kilichoanza 
WEKUNDU wa Msimbazi wamefanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali ya kombe la Mapinduzi kufuatia kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya vinara wa ligi ya Zanzibar, JKU katika mechi iliyomalizika usiku huu uwanja wa Amaan Zanzibar.Bao pekee la Simba limefungwa na Ramadhani Singano ‘Messi’ katika dakika ya 11 kwa shuti kali  akipokea pasi murua ya Said Ndemla.
SAM_4332
Kikosi cha JKU kilichoanza 
Kwa matokeo hayo, Simba wameibuka vinara wa kundi C kwa kujikusanyia pointi 6 kibindoni, huku nafasi ya pili ikishikwa na Mtibwa Sugar wenye pointi tanoSimba walianza mchezo kwa kasi, lakini JKU walionekana kuchakarika kuwadhibiti wakali hao wa Msimbazi.Kikosi cha Mnyama kinachonolewa na Mserbia Goran Kopunovic kimeonekana kucheza mpira wa kasi na pasi za uhakika kuanzia sehemu ya ulinzi na safu ya ulinzi.Baada ya mechi hiyo, kocha Kopunovic amesema timu yake inaimarika kidogo kidogo na ilicheza tofauti kwa vipindi vyote.

 

 

Barcelona yafungiwa kusajili mpaka 2016





































Timu ya Barcelona

Shirikisho la soka dunia FIFA limeitupilia mbali rufaa iliyokatwa na klabu ya Barcelona kuhusu kuizuia kusajili kwa kukiuka kanuni ya usajili.
Barca walifungiwa kwa miezi 14 kusajili baada ya kufanya makosa kwa kusajili kinda wa chini ya miaka 18, Ikiwa ni kinyume na kanuni za usajili za Fifa.
Kwa maamuzi haya timu hii haitakua na uwezo wa kusajili mchezaji mpya mpaka Januari 2016.Barcelona wantarajia kukata rufaa tena maamuzi haya ya Fifa kwenye mahakama ya usuhuhishi michezoni(Cas).
Miamba hiyo ya soka ilifanikiwa kuwasajili mshambuliaji Luis Suarez , mabeki Thomas Vermaelen Jeremy Mathieu golikipa Claudio Bravo na kiungo Ivan Rakitic mwanzoni mwa msimu baada ya baada ya kupewa ruhusa maalumu na Fifa.

Tanzania mwenyeji mpira wa ufukweni






































Mazoezi ya wavu yakiendelea

Tanzania imechaguliwa na shirikisho la mpira wa wavu Afrika (CAVB) kuwa wenyeji wa michuano ya kanda ya Tano ya Beach Volleyball ( mpira wa wavu ufukweni).
Michuano hiyo itakayofanyika kuanzia February 16-18 mwakani itakuwa ni sehemu ya kufuzu kwa michuano ya Olimpiki itakayofanyika Rio de Janeiro, Brazil mwaka 2016.
Mkurugenzi wa Kamisheni ya wavu ufukweni, Muharrami Mchume amesema wapo tayari kwa uwenyeji na kuongeza kuwa Kenya, Burundi, Somalia, Ethiopia, Djibouti na wenyeji Tanzania ndio nchi zitakazoshiriki.
Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa Tanzania kuwa wenyeji wa michuano hiyo.
Mchezo wa mpira wa wavu sio maarufu sana nchini Tanzania licha ya kuwa na fukwe nyingi za bahari.
CAVB ipo katika jitihada za kuendeleza mchezo huo wa ufukweni na hivi karibuni liliendesha semina nchini Tanzania ambayo ilishirikisha washiriki kutoka zaidi ya nchi tano katika jitihada za kuukuza mchezo huo katika nchi za kanda ya tano hasa mashuleni.
Michuano hiyo inategemewa kufanyika katika fukwe za beach ya Mbalamwezi jijini Dar es Salaam.

Alan Ivrine afukuzwa kazi West Brom






































Alan Ivrine

Timu ya West Brom imemfuta kazi kocha wake Alan Ivrine ambaye amekuwa na klabu hiyo kwa miezi saba tangu apate kibarua hicho.
Kocha huyo mwenye miaka 56 raia wa Scotland alikuwa na mkataba wa miezi 12 ambaa upo katika mfumo wa uendelevu.
Ivrine alichukua nafasi ya Pepe Mel ambaye alikuwa akikinoa kikosi hicho ambapo kwa sasa mfululizo vipigo na hiki cha Jumapili cha 2-0 toka kwa Stoke City kimeuchefua timu hiyo na kuona iko haja kocha huyo kuachia ngazi.

Tanzania:ligi ya kwanza soka wanawake 2015








































kikosi cha wanawake kitakachoshiriki Taifa Cup

Mashindano ya Taifa ya mpira wa miguu kwa wanawake (Taifa Cup Wanawake) yanazinduliwa rasmi Januari Mosi mwakani kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kwa mechi kati ya wenyeji Mwanza na Mara. Mechi hiyo itakayoonyeshwa moja kwa moja na televisheni ya Azam itachezwa kuanzia saa 10 jioni. Mashindano hayo yanayodhaminiwa na kampuni ya Proin yatachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini katika hatua ya kwanza.
Januari 10 mwakani ndipo zitachezwa mechi kwa mikoa yote ambapo Geita itakuwa mwenyeji wa Kagera (Uwanja wa Geita), Tabora vs Kigoma (Ali Hassan Mwinyi), Simiyu vs Shinyanga (Uwanja wa Simiyu), Arusha vs Manyara (Sheikh Kaluta Amri Abeid), na Kilimanjaro vs Tanga (Uwanja wa Ushirika).
Mechi nyingine ni Lindi itaikaribisha Mtwara kwenye Uwanja wa Ilulu, Ruvuma vs Njombe (Uwanja wa Majimaji), Mbeya vs Iringa (Uwanja wa Sokoine), Katavi vs Rukwa (Uwanja wa Katavi), Dodoma vs Singida (Uwanja wa Jamhuri) na Pwani itakuwa mwenyeji wa Morogoro katika Uwanja wa Mabatini.
Timu hizo zitarudiana Januari 13 mwakani, ambapo baada ya matokeo ya nyumbani na ugenini timu iliyoshinda ndiyo itakayoingia hatua inayofuata ambayo pia itashirikisha mikoa ya kisoka ya Ilala, Kinondoni na Temeke.
Hatua hiyo, mechi zake za kwanza zitachezwa Januari 17 mwakani wakati zile za marudiano zitafanyika Januari 21 mwakani.
Baada ya hapo, hatua itakayofuata ni robo fainali, nusu fainali na fainali ambayo ndiyo itakayotoa bingwa wa michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini.
Mdhamini atatoa jezi kwa timu zote zinazoshiriki kabla ya kuanza mashindano hayo.



Harakati za Man U zafifia











































nahodha wa kikosi cha Man U wayne rooney baada ya timu hiyo kupata sare ya 0-0 dhidi ya Totenham

Harakati za Manchester United kujaribu kuwafikia Chelsea na mabingwa wa ligi hiyo Mancity zilipata pigo baada ya kupata sare ya 0-0 dhidi ya Totenham Hotspurs.
United ilitengeza nafasi nyingi za wazi katika kipindi cha kwanza huku shambulizi la Juan Mata likipiga chuma cha goli.
Hatahivyo mlinda lango wa Totenham Hugo Lloris alilazimika kufanya kazi ya ziada baada ya kuwanyima mabao Radamel Falcao,Robin Van Persie na Ashley Young.
Kiungo wa kati wa Spurs Andros Townsend alifanya mashambulizi makali katika ngome ya manchester United huku Ryan Mason akikosa bao la wazi katika dakika za mwisho.
Kikosi hicho cha Mauriccio Pochettino kimekuwa kikifunga mabao yake katika dakika za lala salama dhidi ya Swansea na Leicester lakini licha ya kudhibiti mpira dakika 15 za mwisho katika kipindi cha pili hawakuweza kupata bao.

Chelsea na Man U wapata kibarua kigumu











































Mshambuliaji wa Manchester United Robie Van Persie akifunga bao

Mlinda lango wa Totenham Hugo Lioris yuko tayari kuchukua mahala pake Dhidi ya Manchester United licha ya kuuguza jeraha katika mdomo wake wakati wa ushindi dhidi ya Leicester.
Ryan Mason pia anatarajiwa kurudi katika kikosi cha kwanza baada ya kucheza dakika 45 kama mchezaji wa ziada siku ya boxing dei.
Kiungo wa kati wa Manchester United Angel Di Maria hajulikani iwapo atashiriki mechi hiyo kufuatia jereha alilopata siku moja tu kabla ya krisimasi.










































Mchezaji wa Southampton wanyama

Kwengineko, beki wa Manchester City Vincent Kompany huenda akarejea katika kikosi dhidi ya Burnley baada ya kukosa mechi mbili kutokana na jeraha la paja.
City pia itamchunguza mshambuliaji Stevan Jovetic aliye na jeraha la mguu baada ya kutotumiwa siku ya boxing dei.
Kwa upande wake Burnley itamkosa beki Michael Duff na Stephen ward.










































Beki wa Mancity Vincet Kompany

Wakati huohuo kocha wa Chelsea Jose Mourinho hana wasiwasi wa majeraha mapya.
Didier Drogba,Fillipe Luis,Andre Schurrle na John Obi Mikel huenda wakashiriki iwapo the blues inataka kubadilisha kikosi chake dhidi ya Southampton.
Wachezaji wawili wa West Ham Alex Song na Diafra Sakho waligeuzwa katika kikosi cha kwanza dhidi ya Chelsea lakini sasa wanatarajiwa kurudi dhidi ya Arsenal.










































Mchezaji wa Chelsea Didier Drogba

Upande wa Arsenal mshambuliaji Olivier Giroud anaanza kuhudumia marufuku yake ya mechi tatu hatua ambayo itamfanya Danny Welbeck kuanza kama mshambuliaji wa katikati.
Gunners pia itamchunguza beki wa kati Laurent Koscielny ambaye anakaribia kurudi kikosini kutokana na jeraha la mguu.

Frank Lampard kusalia Manchester City












































Frank Lampard

Bosi wa Manchester City Manuel Pellegrini anaamini watambakisha kiungo Frank Lampard.
Kiungo huyo mwenye miaka 36 yuko Manchester City kwa mkopo akitokea New York City,lakini Man City wanataka kumbakisha klabuni hapo kwa muda mrefu.
"Frank ni mchezaji muhimu kwa timu natumaini ataendelea kuwepo hapa," alieleza Pellegrini.
Lampard amekua mchezaji muhimu akiwa amefunga magoli 6 katika mechi 15 aliyocheza na anaoneka atakua mbadala wa Yaya Toure ambae ataenda kuliwakilisha taifa lake katika michuano ya kombe la Afrika mwezi Januari.
Man City wanataka kumalizana na Lampard kabla ya timu yke inayomliki hawajaanza na maandalizi ya msimu mpya wa ligi ya Marekani .




UEFA GOO NIGHT CLUB KUZINDULIWA MKESHA WA KRISMAS

3Kiwanja kipya cha maraha Uefa Goo Night Club kinatarajiwa kuzinduliwa mkesha wa sikukuu ya Krismas jijini Dar es salaam Kiwanja hiki ni cha Kisasa kiko maeneo ya Ukonga Mombasa Barabara ya kuelekea Moshi Baa Karibu na njia panda ya Mahita mita 200 kutoka barabara kuu iendayo Pugu, siku ya mkesha wa Krismas burudani kibao zimeandaliwa  na kiwanja hicho kiko katika hatua za mwisho mwisho kukamilisha kila kitu ili kuwapa burudani wateja wake ikiwa ni pamoja na Ligi mbalimbali za ulaya, muziki wa kisasa kama vile Bongofleva na muziki wa zamani na vyakula mbalimbali vitapatikana
12Hizi ni baadhi ya picha zinazoonyesha jengo kwa nje na maendeleo ya kukamilisha ujenzi kwa ndani kwenye klabu hiyo ambao umefikia asilimia 99 kabla ya kufunguliwa mkesha wa Krismas.7654



BONDIA TWAHA KASSIM WA MOROGORO AMTWANGA KWA KO, MUSSA CHITEPETE WA SONGEA

  • Share on facebookShare on google_plusone_shareShare on twitterShare on linkedin
Mabondia Twaha Kassim wa Morogoro kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Mussa Chitepete wa Songea wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Kassim alishinda kAwa K,O ya raundi ya sita Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Mussa Chitepete wa Songea akiwa chini baada ya kupokea konde zito kutoka kwa Twaha Kassim wa Morogoro wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Kassim alishinda kwa K,O ya raundi ya 6 Picha na SUPER D BOXING NEWS
Bondia Cosmas Cheka kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Ramadhani Shauri wakati wa mpambano wao uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Cheka alishinda kwa point mpambano uho wa raundi 8 Picha na SUPER D BOXING NEWS

Real Madrid ndio kilabu bingwa duniani
















































Real Madrid washerehekea ushindi wao wa kombe la kilabu bingwa duniani baada ya kuinyuka kilabu ya marekani kusini San Lorenzo 2-0 katika fainali iliochezwa nchini Morrocco.

Kilabu ya Real Madrid imeshinda taji lao la nne mwaka 2014 baada ya kuwashinda mabingwa wa Marekani Kusini kutoka Argentina San Lorenzo katika fainali la za kilabu bingwa duniani zilizochezwa nchini Morrocco.
Mabingwa hao wa kombe la kilabu bingwa barani ulaya,Copa Del Rey na mabingwa wa Super Cup barani Ulaya walianza kufunga kupitia kichwa cha Sergio Ramos.
Makosa ya mlinda lango wa Lorenzo yaliihakikisha ushindi Real madrid baada ya Gareth Bale kuongeza bao la pili.
Real madrid hawakutatizwa na mabingwa hao wa Marekani kusini na hivyobasi kuongeza rekodi yao ya ushindi katika mecho zote kufikia 22.
Ushindi huo pia ni wa kwanza wa kilabu hiyo Bernabeu.

Liverpool yaambulia sare kwa Arsenal

















































Liverpool na Arsenal zatoka sare

Liverpool, wakiwa uwanja wa nyumbani Anfield, wamenusurika kupata kichapo toka kwa Arsenal kwa kupata sare ya goli 2-2.
Mshambuliaji Philippe Coutinho alianza kuiandika Liverpool goli la kwanza, kabla ya Mathieu Debuchy hajaisawazishia Arsenal, Olivier Giroud akaongeza bao la pili dakika ya 64.
Beki Martin Skrtel alifunga bao la kusawazisha dakika za nyongeza za kipindi cha pili(90+7) kwa mpira wa kichwa uliomshinda kipa wa Wojciech Szczesny
Mshambulaiji Fabio Borini alitolewa nje baada ya kupewa kadi mbili za njano na kuwafanya liverpool kucheza pungufu.
Katika mchezo mwingine wa Sundeland walipata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Newcastle United.
Winga Adam Johnson ameibuka shujaa kwa kufunga goli pekee la ushindi kwa upande wa Sunderland, bao la dakika ya 90.
Katika mchezo huo beki wa Newcastle Steven Taylor alipata majeraha baada ya kupasuka eneo la jicho katika heka heka za kumzuia mshambuliaji Steven Fletcher.

Mwanariadha wa Kenya alitumia dawa

Mshirikishe mwenzako
















































Mwanariadha wa kenya Ritaa Jepoo aligunduliwa kutumia dawa za kusisimua misuli

Mwanariadha wa mbio za marathon raia wa Kenya Rita Jeptoo amegunduliwa kuwa alitumia dawa zinazosisimua misuli.
Shirika la riadha nchi Kenya limesema kuwa uchunguzi wa pili ulibaini kuwa mwanariadha huyo alitumia dawa hizo.
Shirika hilo linasema kuwa litasikiliza kesi hiyo mwezi Januari mwaka ujao .
Jeptoo alikuwa ameshinda mbio za Boston marathon mara tatu na za Chicago mara mbili na ni mmoja wa wanariadha maarufu zaidi nchini Kenya kupatikana na hatia ya kutumia dawa za kusisimua misuli.

FIFA sasa kuchapisha 


















































Aliyekuwa mchunguzi wa kamati ya maadili katika shirikisho la soka FIFA.

Maafisa wakuu wa shirikisho la FIFA wamekubaliana kuchapisha ripoti yote kuhusu uchunguzi wa madai ya ufisadi uliotokea wakati wa kutolewa kwa kandarasi za kombe la dunia kwa mataifa ya Urusi mwaka 2018 na Qatar mwaka 2022.
Wamekubaliana kutoa kurasa 430 za uchunguzi wa Michael Garcia baada ya kufanya mkutano kufuatia pendekezo la mkuu wa kufuata maagizo Domenica Scala.
Ripoti hiyo itawekwa wazi baada ya uchunguzi unaondelea kuhusu watu watano kukamilika na inatarajiwa kufanyiwa uhariri ili kuficha majina ya mashahidi.
Hatua hiyo ya kuichapisha ripoti hiyo inaonyesha mabadiliko ya sera baada ya FIFA kukataa shinikizo kutoka kwa Garcia mwenyewe na wengine kutoa ripoti hiyo.
Garcia alijiuzulu siku ya Jumatano baada ya ombi lake la kupinga ripoti fupi ya uchunguzi wake iliotolewa na mwenyekiti wa kamati ya maadili katika shirikisho hilo Hans-Joachim Eckert kukataliwa.

Steve Gerrard:Arsenal haitatushinda




















































Nahodha wa kilabu ya Liverpool Steve Gerrard amesema kuwa hatokubali timu yake kulazwa na Arsenal katika mechi ya jumapili.

Nahodha wa kilabu ya Liverpool Steven Gerrard amekiri kuwa Manchester United ilikuwa bora ikilinganishwa na Liverpool wakati timu hizo mbili zilipochuana wikendi iliopita lakini anasema kuwa hatokubali kushindwa na Arsenal wikendi hii.
Man United iliicharaza Liverpool 3-1 katika mechi hiyo.
Lakini Gerrard anaamini kwamba motisha uliopatikana katika timu hiyo baada ya kuishinda kilabu ya Bournemouth 3-1 katika mechi ya Kombe la Ligi na hivyobasi kuingia katika semi fainali na chelsea inaiweka timu hiyo katika nafasi nzuri dhidi ya Arsenal siku ya jumapili.
''Tofauti ya siku ya jumatano ikilinganishwa na siku ya jumapili ni kwamba tulifanya makosa makubwa katika uwanja wa Old Trafford na tukaadhibiwa na wachezaji wa kimataifa'',alisema Gerrard.
''Dhidi ya Bournemouth tulipunguza makosa hayo na kipindi cha kwanza kilikuwa kizuri sana pengine tunaweza kusema tulikaribia viwango vya msimu uliopita''.aliongezea.























































Kocha Maximo

Klabu ya Yanga na wawakilishi wa michuano ya shirikisho ya Afrika imewatupia virago rasmi makocha wabrazil Marcio Maximo na msaidizi wake, Leonardo Neiva kwa kile kinachoelezwa kutofurahishwa na mwenendo wa timu katika ligi licha ya kuwa na wachezaji wengi mastaa wa kigeni na kutumia mamilioni katika kusajili wachezaji mahiri wa kigeni.
Yanga hivi karibuni ilimsajili mrundi na mfungaji bora msumu uliopita, Hamis Tambwe kutoka kwa mahasimu wao (Simba) akiungana na Mliberia, Kpah Sherman, Wanyarwanda Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite na Mbrazil Andrey Coutinho kukamilisha idadi ya wachezaji watano wa kigeni
Tayari uongozi wa Yanga, katika kile kinachoonekana pesa si tatizo, chini ya Mwenyekiti bilionea Yusuf Manji umemrudisha klabuni aliyekuwa kocha wa zamani, Mholanzi Van de Pluijm, atakayesaidiwa na kocha mzalendo na mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa na klabu hiyo, Charles Boniface Mkwasa.
Katika maelezo yake, Manji amewatakia kila la kheri wabrazil hao na kusema na mungu akipenda wataendelea kushirikiana nao katika siku za usoni.



















































Alama ya wana Jangwani

Tayari makocha hao wawili , Pluijm na Mkwasa wameshatambulishwa kwa wachezaji wa Yanga na habari za uhakika kutoka klabu hapo zinasema baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja na nusu, Pluijm, aliyewahi kuipatia yanga mafanikio katika ligi kuu, ana anza kibarua chake rasmi leo.
Hata hivyo, kuondoka kwa Maximo, aliyewahi kuajiriwa na Serikali ya Tanzania kama kocha mkuu wa timu ya taifa, Stars Stars katika miaka ya nyuma na kurudi nchini kivingine kuongoza Yanga, kumegubikwa na sintofahamu huku kukiwa na habari kuwa bado anavutana na uongozi juu ya mafao yake kwa kuvunjiwa mkataba.
Maximo, aliiongoza Yanga katika mechi tisa ndani ya miezi mitatu (akipoteza mechi mbili katika mechi saba) baada ya kupokelewa kwa shangwe uwanja wa ndege alipowasili kuwafundisha mabingwa hao wa zamani wa Tanzania.
Inasemekana kuondolewa kwake kunatokana na kipigo cha mabao 2-0 Yanga ilichokipata baada ya kufungwa na watani wao wa jadi, Simba katika mechi isiyo ya ligi (Nani Mtani Jembe) chini ya kocha Mzambia Patrick Phiri.
Maximo anakuwa kocha wa pili kufukuzwa na Yanga baada ya matokeo mabaya ya mechi ya Nani Mtani Jembe. Kocha kutoka Uholanzi, Ernie Brandts, pia alifukuwa baada ya kupata kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Simba .






















































Ander Herrera


Mwendesha mashitaka kutoka idara ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini Hispania imeiagiza mahakama kumchunguza kocha wa zamani wa klabu ya Real Zaragoza na baadhi ya wachezaji kutokana na tuhuma za kudaiwa kuuza mchezo.
Tuhuma hizo ni katika mchezo wa kufunga wa msimu wa ligi 2011 ambapo Real Zaragoza iliishinda timu Levante.
Upande wa mashitaka unadai kuwa watuhumiwa wanahusishwa na rushwa ya dola million mbili.
Baadhi ya wachezaji wanaotuhumiwa katika kashfa hiyo ni Ander Herrera, ambaye sasa anachezea zamani na captain wa timu ya Atletico Madrid,Gabi na Javier Aguirre.























































Andre akiwa kazini.

Kiungo wa timu ya Manchester United Ander Herrera amesisitiza hajawahi kupanga matokeo ya mechi wakati akiichezea klabu Real Zaragoza.
Mhispania huyu ametajwa katika kundi la wanamichezo 41 wakiwemo wachezaji ,makocha na wakurugenzi katika uchunguzi wa kashfa ya upangaji matokeo kwenye ligi kuu ya Hispania.
Herrera ameandika katika ukurasa wake wa facebook.:Sijawahi na kamwe sintofanya chochote katika kupanga matokeo,naupenda mpira naamini katika mchezo wa haki nje na ndani ya uwanja:
Waendesha mashitaka wanadai fedha taslimu € 965,000 zililipwa kwa kocha Javier Aguirre na wachezaji tisa wa Zaragoza, ikiwa ni pamoja na Herrera, kabla ya mchezo wa La Liga mwishoni mwa msimu wa 2010-201.
Herrera aliondoka Zaragoza na kujiunga na timu ya nyumbani kwao ya Athletic Bilbao mwezi Agosti 2011, kabla ya kujiunga na Man United mwezi Juni 2014.






















































Thierry Henry

Mshambuliaji wa zamani wa Klabu ya Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa Thierry Daniel Henry ametangaza kustaafu kucheza soka rasmi.
Nyota huyu alietwaa kombe la dunia mwaka 1998 akiwa na timu ya Ufaransa alijiondoa kwenye klabu yake New York Red Bulls mapema mwezi huu na kukawa na tetesi atachagua kujiunga na klabu nyingine kubwa barani ulaya.
" Napaswa kuwashukuru mashabiki wote, nawashukuru wachezaji wenzangu na watu binafsi wanaohusika na AS Monaco, Juventus, Arsenal FC, FC Barcelona,na New York Red Bulls na pia Timu ya taifa ya Ufaransa waliufanya wakati wangu wa mchezo kuwa Maalumu".
Henry alianza kuwika katika soka la kimataifa akianzia klabu ya Monaco kisha akaelekea Juventus ,kabla ya kutua Arsenal alikocheza kwa mafanikio makubwa.

Kutimuliwa Maximo,Wachezaji Yanga kilio





















































Aliyekuwa Kocha wa Yanga Marcio Maximo amewaaga wachezaji wa Yanga

Mechi ya Mtani Jembe nchini Tanzania, inayozikutanisha timu mbili za jijini Dar es Salaam zenye ushindani wa jadi, za Simba na Yanga imegeuka uwanja wa machinjio kwa makocha wa Yanga kwa mara ya pili mfululizo.
Mechi kama hiyo ilipofanyika mwaka jana, 2013, Yanga ilifungwa magoli 3-1 na kusababisha aliyekuwa kocha wake Ernie Brandts kutimuliwa pamoja na benchi lake la ufundi. Mwaka huu ni zamu ya kocha Marcio Maximo kufungashiwa virago vyake baada ya kunyukwa mabao 2-0 katika mechi ya Mtani Jembe iliyofanyika Jumamosi iliyopita katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, na huu ukiwa ni mchezo wa nane wa ushindani baada ya michezo saba tu ya ligi kuu ya Vodacom ya nchi hiyo.
KOCHA Maximo ambaye alipokelewa kwa vifijo na nderemo na mashabiki na wanachama wa Yanga mwezi Juni mwaka huu baada ya kutangazwa kuwa kocha mpya wa timu yao, amewaaga rasmi wachezaji wa timu hiyo kwenye mazoezi uwanja wa Sekondari ya Loyola ya jijini Dar es Salaam.
Mazoezi hayo ya Jumanne asubuhi yaligeuka simanzi baada ya Maximo kuwakusanya wachezaji wake na kuwambia kuwa kuanzia hiyo jana hakuwa kocha wa timu hiyo tena na kuwatakia maisha mema ndani ya klabu hiyo ya Jangwani.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wachezaji wa klabu hiyo walielezea kutoridhishwa na uamuzi wa uongozi wa klabu hiyo kumuacha kocha wao na mshambuliaji Hamis Kiiza kutoka Uganda.
Mmoja wa wachezaji hao alisema "Ni kweli kocha ametuaga asubuhi daa! ndio hivyo tumesikitika lakini hatuna jinsi."





















































Naye mchezaji mwingine ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema "Inaumiza sana jana (juzi) tumefanya nae mazoezi vizuri kabisa tena amechangamka kama kawaida kumbe nyuma kuna mambo yanaendelea, leo asubuhi tumeenda mazoezi kama kawaida tukijua tunafanya mazoezi matokeo yake anasema acheni kila kitu kaeni hapo nataka kuzungumza na nyinyi".
Mchezaji mwingine wa timu hiyo alisema "Hakuna mchezaji kwa kweli aliyependezwa na kitendo cha uongozi, yaani kwenye mazoezi asubuhi ilikuwa kama msiba, 'mood' ya kufanya mazoezi iilisha kabisa, yaani hakuna aliyekuwa na hamu ya kuendelea na mazoezi.
"Tumefanya kidogo mazoezi tukaondoka, ukiangalia ni sawa tumefungwa cha muhimu ilikuwa ni kukaa chini na kuzungumza na kuangalia cha kufanya, kama kuna mapungufu basi yafanyiwe kazi, mimi sijaona haja ya kumfukuza kocha hasa kipindi kama hichi."
Meneja wa timu hiyo Hafidhi Saleh alikiri Maximo kuwaaga wachezaji kabla ya mazoezi ya timu hiyo kwanza akiwapa moyo wajitume kwa kuwa ni wachezaji wazuri na timu ni nzuri na kuwataka kuongeza bidii ili wafike mbali.
"Kwa kweli inasikitisha hakuna mchezaji wala mtu aliyefurahia, kama yupo labda kimoyomoyo ila dah imetuumiza, ni mazoea cha muhimu tugange yajayo hayo mengine tuwaachie viongozi."alisema Saleh
Mchezo wa Mtani Jembe ambao ni wa kujifurahisha na kuongeza utani kati ya timu hizo, umegeuka kuwa kipimo cha ubora wa kocha hata kama kocha huyo anafanya vizuri katika michezo ya ligi kuu. Hadi wakati anafukuzwa, kocha wa Yanga Mbrazil Marcio Maximo, timu yake inashika nafasi ya pili baada ya Mtibwa inayoongoza katika msimamo wa ligi hiyo kutokana na michezo saba tu iliyochezwa.
Baadhi ya mashabiki wameunga mkono uamuzi wa kumtimua Maximo wakisema timu haikuwa na uwezo wa kupambana na timu pinzani, huku wengine wakipinga uamuzi huo kuwa haukustahili kuhukumu uwezo wa kocha huyo katika mchezo mmoja wa kirafiki na kusahau nafasi inayoshikiliwa na timu katika msimamo wa ligi kuu.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG