Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

DINI



Papa Francis akutana na rais wa Palestine

Kiongozi wa Wakatoliki duniani Papa Francis amefanya mazungumzo na rais wa Palestina Mahmoud Abbas huko Vatican.
Papa Francis alimmiminia sifa Abbas akimtaja kuwa, kuwa ni malaika wa amani.
Kiongozi huyo wa wakatoliki alimsifu Abbas kabla ya kumtunukia medali ya amani.
Ziara ya bwana Abbas inawadia siku chache tu baada ya utawala wa kanisa Katoliki duniani wenye makao yake huko Vatican kutangaza kuwa wataweka sahihi ya kwanza na wapalestina hivi karibuni.
Mkataba huo utakaotiwa sahihi karibuni unatambua hoja ya kuweko kwa mataifa mawili mkabala ilikuchochea amani baina ya wapalestina na waisraeli.
Kulingana na Vatican hiyo itahakikisha kutambuliwa kwa wakatoliki katika maeneo yanayotawaliwa na rais Abbas.
Israeli kwa upande wake ilitangaza kutofurahishwa kamwe kwa mkataba huo baina ya kanisa katoliki na taifa la Plaestina kwani inatambua ''Palestina kuwa taifa''
Rais Abbas yuko Vatican kuhudhuria kutawazwa kwa watawa wa kipalestina na kanisa katoliki.
Sherehe hiyo itafanyika hapo kesho.


Viapo vya ndoa havitekelezeki.



Harusi na viapo visivyotekelezeka.

Ahadi ya kuwa pamoja maishani katika shida na raha,taabu na shida viapo hivi ama ahadi hizi zinaonekana kuchukuliwa kirahisi mno na wanandoa wapya, lakini kwa muujibu wa utafiti mpya uliotolewa hivi karibuni unathibitisha kuwa ni rahisi mno kutamka kuliko utekelezaji wa viapo vyenyewe .
Mtafiti uliofanywa kwa wanandoa wenye bahati 2,700 waliooana umegundua kwamba ,ikiwa mwanamke katika ndoa hiyo ataugua kwa muda mrefu asilimia sita hukaribia kupewa talaka kuliko wale ambao wana afya njema .
Ukilinganaisha na wanaume ambao huugua wakiwa kwenye ndoa,hatari ya kuvunjika kwa ndoa ni ndogo mno,hatahivyo upendo huendelea hadi hapo mmoja wao atakapo baki kuwa mgane ama mjane.
Utafiti ulioongozwa na wanazuoni wa chuo kikuu nchini Marekani,kinapendekeza kwamba kwa asili, wanawake wao wameumbwa kutoa huduma katika familia zao nah ii inamaanisha kwamba wanaume wao huwa hawana uvumilivu wake zao pindi wanapokumbwa na maradhi ya muda mrefu ,ambayo pia yanweza kuwa hayatabiriki kuyakabili.
Walifanyiwa utafiti wanandoa nchini Marekani,ambao wote walikuwa na umri wa miaka 50, mnamo mwaka 1990 ambao waliulizwa juu ya afya zao kuhusiana na maisha yao wakichnugza kwa miaka miwili,miwili ndani ya utafiti uliofanywa kwa miaka ishirini.
Asilimia thelathini na mbili ya ndoa ziliishia kwa kuachana na asilimia ishirini na nnenzilivunjika kutokana na vifo vya mmoja wa wanandoa.
Kikosi cha utafiti kiliongozwa na Amelia Karraker, ambaye ni profesa msaidizi juu ya masuala ya maendeleo ya binaadamu na utafiti juu ya familia kutoka katika chuo cha Iowa State University,analinganisha matukio ya namna nne kansa,magonjwa ya moyo,kiharusi na magonjwa ya njia ya hewa kwa wanawake na wanaume na matokeo ya ndoa.


Tamu na chungu ya ndoa

Utafiti huo umebainisha kwamba , kuna tofauti ya kujisikia mgonjwa sana na huwezi kupika chakula cha jioni, ama unahitaji mtu hasa wa kukulisha masuala haya yanaweza kubadili upepo ndani ya ndoa .
Katika hali hiyo,utafiti huo hauoneshi dhahiri kuwa mume ama mke anadai talaka,takwimu kamili zinaonesha kwamba wanawake ni wepesi zaidi kuomba talaka kuliko wenza wao.
Bi Karraker anasema amegundua kwamba kwamba inawezekana baadhi ya wanawake ambao huachwa kwasababu ya huduma zao ama kushindwa kuhudumia
Tafakari juu ya Uhai ama kifo husababisha watu wajitafiti wenyewe na kujiuliza maswali muhimu kuwa ni nini muhimu maishani mwao? Anaeleza mtafiti huyo.
Wanawake wakati mwingine huribuka kwa kusema kuwa waume zao hawawajali,na hawafurahishwi na suala hilo ama husema sikufurahishwa na mwanzo wa mahusiano yao, na wansema kwamba wako radhi kubaki peke yao kuliko kujitosa katika ndoa isiyofaa.

Mfalme Abdullah afariki dunia



Hayyat Mfalme Abdullah

Taarifa zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa mfalme wa Saudi Abdullah bin Abdulaziz amefariki dunia akiwa hospitalini .
Tamko la kifo cha mfalme huyo zilitolewa na kaka wa mfalme huyo aitwaye , Salman,ambaye naye aliwahi kuwa mfalme.
Kabla ya tamko hilo television ya taifa la Saudi lilikatiza matangazo yake na kuweka nyimbo za quraan ,kama ishara ya kifo cha kiongozi wa juu wa ufalme.
King Abdullah, amefariki dunia akiwa na miaka 90, alilazwa hospitalini kwa wiki kadhaa tangu December mwaka wa jana kutokana na maambukizi kwenye njia ya hewa.
Mfalme huyo aliingia madarakani mwaka 2005 lakini alikuwa ni dhaifu mwenye kushambuliwa na maradhi mara kwa mara.

Papa Francis azungumzia familia

  • Saa 3 zilizopita
Mshirikishe mwenzako



Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani ameunga mkono haki ya wazazi kuchagua ukubwa wa familia zao.
Amesema waumini wazuri wa Kanisa katoliki hawapaswi kuzaa bila ya mpangilio.
Kiongozi wa Kanisa katoliki duniani amelalamikia mawazo ya nchi za magharibi kuhusu kudhibiti uzazi na haki za wapenzi wa jinsia moja kuwa yamezidi kushinikizwa katika familia za nchi zinazoendelea.
Wakati wa ziara yake, Papa Francis ametetea utamaduni wa mafundisho ya kanisa katoliki unaopinga matumizi ya dawa za uzazi wa mpango.
Wakati wa ziara yake nchini Ufilipino, inakadiriwa kuwa watu milioni sita walihudhuria ibada iliyoendeshwa na kiongozi huyo wa kanisa katoliki duniani, katika mji mkuu wa nchi hiyo, Manila.

Waisilamu waandamana dhidi ya C.Hebdo

  • 16 Januari 2015
Mshirikishe mwenzako




Maandamano nchini Pakistan kuonyesha kero la waumini wa kiisilamu kuhusu Charlie Hebdo

Polisi nchini Pakistan wamekabiliana na waandamanaji, walioghadhabishwa na uamuzi wa jarida na Ufaransa la Charlie Hebdo wa kuchapisha vibonzo vya mtu wanayedai ni Mtume Mohammad.
Baada ya maombi ya ijumaa, maafisa wa ulinzi walitumia magari yenye majai kuwamwagia maji waandamanaji katika juhudi za kuwatwanya.
Walikuwa wamekusanyika nje ya ubalozi wa Ufaransa mjini Karachi.
Baadhi ya waandamanaji inaarifiwa walikuwa wamebeba bunduki. Watu watatu walijeruhiwa katika maandamano yenyewe.
Mwandishi wa BBC mjini Islamabad amesema idadi ya waandamanaji hao, kwa mujibu wa idadi ya wasisilamu nchini Pakistan, ilikuwa ndogo.
Maandamano kama hayo yameitishwa katika nchi zingine zilizo na idadi kubwa ya waumini wa Kiislamu kama vile Uturuki, Ufilipino,Kuwait, Mauritania na Sudan.

Askofu akosoa Ulaya kuhusu Boko Haram







Askofu Kaigama anasema Ulaya inapuuza sana vita dhidi ya Boko Haram

Askofu mmoja nchini Nigeria ametoa wito kwa mataifa ya magharibi kufanya juhudi za kutosha dhidi ya Boko Haram kama ilivyofanywa dhidi ya washambuliaji wa kiisilamu nchini Ufaransa.
Askofu Ignatius Kaigama amesema mataifa ya magharibi yanapuuza sana tisho linalotokana na Boko Haram kwa watu wa Nigeria.
Askofu huyo wa Jos, aliongeza kwamba rasilimali zote zinatakiwa kutumika ili kuzuia juhudi za kundi hilo kukita mizizi nchini Nigeria. Pia amesema kwamba dunia inapaswa kuonyesha ari ya kutaka kuangamiza kundi hilo.
Kadhalika askofu huyo amesisitiza kwamba mauaji ya hivi karibuni ya mamia ya watu mjini Baga ni ishara kwamba jeshi la nchi hio limeshindwa kukabiliana na wapiganaji hao.





Kiongozi wa kundi la Boko Haram ambalo limekuwa likifanya mashambulizi kila kukicha nchini Nigeria

Onyo la askofu huyo linakuja siku mbili tu baada ya mashambulizi ya bomu kuwaua zaidi ya watu 20.
Mnamo Jumapili,washambuluaji wawili wa kike walifanya mashambulizi ya kujitoa mhanga na kuwaua watu wanne huku wnegine zaidi ya arobaini wakijeruhiwa mjini Potiskum
Siku moja kabla ya mashambulizi hayo, mashambuluaji mwingine w akujitoa mhanga alishambulia mji wa Maiduguri na kuwaua watu 19.
Mashambulizi haya yametokea baada ya taarifa kwamba mamia ya watu waliuawa wiki jana wakati Boko Haram ili poteka mji wa Baga katika jimbo la Borno.

Afisa wa kanisa apigwa risasi Mombasa








Kanisa

Polisi nchini Kenya wanasema afisa mmoja wa kanisa amepigwa risasi na kuuawa alipokuwa akielekea katika maombi.
Madhumuni ya mauaji hayo hayajatambulika, lakini Muungano wa Makanisa mjini Mombasa tayari umesema ni mauji ya kidini.
Mauaji ya afisa wa kanisa jijini Mombasa yanatishia kuhangaisha wakaazi walioanza mwaka kwa amani baada ya machafuko mengi ya mwaka 2014.
Polisi wanasema afisa wa kanisa moja jijini Mombasa alipigwa risasi na kufariki alipokuwa akiingia ndani ya shule moja ambayo wameikodisha kufanya maombi yao.






Polisi Mombasa

Mkuu wa Upelelezi wa Uhalifu Mombasa Ondiek amesema mtu mmoja aliyekuwa na bunduki alimfuata jamaa huyo hadi akaingia ndani ya uwanja wa shule kabla ya kumpiga risasi. Alikufa papo hapo.
Aidha Ondiek amesema Polisi waliokuwa wameshika doria shuleni walisikia sauti za risasi na hivyobasi kumkabili muuaji huyo, lakini akahepa ndani ya vitongoji vilivyo karibu na shule.





SHEREHE ZA MAULID YA KUZALIWA MTUME MUHAMMAD S.A.W.

unnamedRais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) wakati alipojumuika na Mashekhe, Viongozi na Waislamu mbali mbali katika sherehe za Maulidi ya Kuzaliwa kwa Bwana Mtume Muhmmad S.A.W yaliyofanyika jana katika viwanja vya Maisara Suleiman Mjini Unguja,(pichani) Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi akitia ubani kama ishara ya Ufunguzi wa Maulid hayo,[Picha na Ikulu.]
unnamed1Mke wa Makamo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Zakia Bilali (katikati) akiwa na Wake wa makamo wa Pili wa rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi (kushoto) na Mama Pili balozi Seif (kulia) pamoja na Wake wa Viongozi mbali mbali na wananchi wa kawaida wakijumuika katika sherehe za Maulidi ya Kuzaliwa kwa Bwana Mtume Muhmmad S.A.W yaliyofanyika jana katika viwanja vya Maisara Suleiman Mjini Unguja ambapo hufanyika kila ifikapo mwezi kumi na moja mfunguosita,[Picha na Ikulu.]unnamed2Akina Mama kutoka mitaa mbali mbali ya Mji wa Unguja na Vitongoji vyake wakiwa katika viwanja vya Maisara Suleiman Mjini Unguja palipofanyika sherehe za Maulidi ya Kuzaliwa kwa Bwana Mtume Muhmmad S.A.W ambapo hufanyika kila ifikapo mwezi kumi na moja mfunguosita na mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein, [Picha na Ikulu.]unnamed3Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi (katikati) Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif,Kadhi Mkuu wa zanzibar Sheikh Khamis Haji (kulia) Waziri wa katiba na Sheria Abubakar Khamis Bakary akifuataiwa na makamo wa Pili wa Rais Alhaj Seif Ali Iddi wakisimaa kwa pamoja na waislamu wengine na Viongozi wakati wa Kumswalia Bwana Mtume Muhammad S.A.W.katika sherehe ya Maulid iliyofanyika jana viwanja vya Maisra Suleiman Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]unnamed4Wanafunzi wa Vyuo mbali mbali vya Quran na Waislamu mbali mbali waliohudhuria katika sherehe  za Maulid ya kuzaliwa Bwana Mtume Muhammad S.A.W zilizofanyika jana katika Viwanja vya Maisara Suleiman Mjini Unguja kama wanavyoonekanwa Pichani,[Picha na Ikulu.]unnamed6Wanafunzi wa Madrasatul Dhuriyatul Islamia kutoka Kisiwani Tumbatu Mkoa wa Kaskazini Unguja wakisoma Qaswida wakati wa sherehe za Maulid Matukufu ya kuzaliwa bwana Mtume Muhammad (S.A.W.) zilizofanyika jana katika viwanja vya Maisra Suleiman Mjini Unguja mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein,[Picha na Ikulu.]unnamed7Ustadh  salum Rashid kutoka Amani Wilaya ya Mjini Unguja akisoma  Mlango wa Barzanji(4) wakati wa sherehe za Maulid Matukufu ya kuzaliwa bwana Mtume Muhammad (S.A.W.) zilizofanyika jana katika viwanja vya Maisra Suleiman Mjini Unguja mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein,[Picha na Ikulu.]















Mwanamume akiandika katika kitabu cha kukunjwa










Mafundisho ya Biblia

Biblia inatoa mashauri bora zaidi katika maisha hasa kuhusiana na maswali magumu. Thamani yake imethibitika kwa karne nyingi. Habari hii, itakusaidia kuona jinsi mashauri ya Biblia yalivyo yenye thamani.—2 Timotheo 3:16, 17.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG