- Written by Tupambane Blog
- Tuma Maoni
-
Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter
|
DC wa Iringa, Dk Leticia Warioba na
DED wa Iringa, Pedenciana Kisaka (kulia) wakifurahi wakati Edna Haule
anayeishi na maambukizi ya VVU akijaribu kuendesha moja katia baiskeli
50 zilizotolewa kwa vikundi 17 vya akina mama wenye maambukizi hayo |
|
Katika picha ya pamoja
|
|
Baadhi ya akinamama wanaounda vikundi hivyo wakishuhudia makabidhiano hayo |
|
Hizi ndio baiskeli zenyewe |
SHIRIKA
la Utafiti wa Tiba na Afya barani Afrika (AMREF) limetoa msaada wa
baiskeli 50 kwa vikundi 17 kati ya 36 vya watoto salama vinavyoundwa na
akina mama wenye maaambukizi ya virusi vya Ukimwi (VVU) vya Iringa
Vijijini.
Akivikabidhi msaada huo katika hafla iliyofanyika katika ofisi ya
halmashauri ya wilaya ya Iringa, Mkuu wa wilaya ya Iringa, Dk Leticia
Warioba aliwapongeza na akawataka wasikate tamaa kwani kuwa na VVU sio
mwisho wa maisha.
“Mjisikie wenye amani, majasiri na mnaopaswa kuigwa, kwani wako wengi
wana tatizo kama lenu lakini kwasababu ya hofu wanaogopa kupima afya zao
na mkiwaona barabarani mnaweza kufikiri wote wana afya njema,” alisema. (FS)
Akishukuru
kwa msaada huo, mmoja wa akina mama wenye maambukizi hayo, Edna Haule
kutoka kijiji cha Migori alisema “tumevunja ukimya tukiamini watanzania
wenzetu ambao hawajapima, watajitokeza kujua afya zao ili watakaobainika
kuwa na maambukizi waingie kwenye mpango wa mafunzo ya namna ya kutunza
afya zao na kutumia dawa.”
Aliwashangaa
baadhi ya watanzania wanaoendelea kuwacheka au kuwasimanga wenye
maambukizi ya VVU alisema kujua hali ya afya yako kuna faida nyingi
ikiwa ni pamoja kukusaidia kujiadhari na maambukizi mapya.
Naye
Thadei Madege wa kijiji cha Kihanga alisema baiskeli walizopewa
zitawasaidia katika safari zao za kufuata dawa katika vituo vya afya
pamoja na kurahisisha shughuli zao mbalimbali za kiuchumi.
Akizungumzia
umuhimu wa vikundi vya watoto salama, Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Wilaya ya Mufindi, Pudenciana Kisaka alisema vinasaidia kutoa elimu ya
kujikinga na maambukizi mapya ya VVU na inayowasaidia akina mama wenye
maambukizi hayo kuzingatia ushauri ili wanapopata mimba wajifungue
watoto wasio na maambukizi.
Kisaka
alisema kwa kupitia elimu hiyo, vikundi hivyo hufundishwa pia njia
zinazosaidia kuwanusuru na maambukizi ya VVU, watoto wanaonyonya kwa
akina mama wenye maambukizi hayo.
Mratibu
wa Amref anayeshughulikia mradi wa Kutoa Ushauri Nasaha na Upimaji wa
VVU, Boniface Magesa alisema baiskeli shirika lao litaendelea
kuviwezesha vikundi hivyo kwa kadri litakavyopata nafasi.
“Tumeanza
na vikundi hivi, tunajua viko vikundi vingi kwahiyo tunaendelea
kutafuta rasilimali zitakazowezesha vikundi vilivyopata vipate zaidi ili
kukidhi mahitaji yao na vile ambavyo havijapata navyo vinufaike na
huduma zetu
No comments:
Post a Comment