Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Tuesday, September 2, 2014

David Rudisha amaliza wa tatu

02 september  2014 - Saa 11:28 GMT
  • Google+
  • Chapisha
Nijel Amos alimzidi nguvu David Rudisha
Katika michuano ya Diamond League ya jana usiku, Nijel Amos alimzidi kasi ya kuufukuza upepo David Rudisha katika michuano ya mita 800 mjini Zurich.
Mshindi huyo wa michuano ya Olympic David Rudisha alimaliza mbio zake katika nafasi ya tatu kwenye mbio hizo za mita 800 wakati mwanariadha mchanga na mwenye ubavu wa kutanua mapafu mbioni Nijel Amos kwa mara ingine tena amejitwalia tena ubingwa huo wa mita 800.
Na hii si mara ya kwanza kwa Amos kumshinda nguvu Rudisha kwani mwezi uliopita katika michuano ya jumuiya ya madola maarufu kama Commonwealth Games na kujitwalia medali ya dhahabu huku akitumia dakika 43. sekunde 77
Naye Ayanleh Souleiman alimshinda Rudisha na kutwaa nafasi ya pili kitendo kilichomlazimisha Rudisha kushika nafasi ya tatu

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG