- Written by Tupambane Blog
- Tuma Maoni
-
Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter
MBRAZIL
Geilson Santos Santana ‘Jaja’ kwa mara ya kwanza akicheza katika uwanja
wa kisasa wa Taifa jijini Dar es salaam amefanikiwa kuifungia Yanga bao
pekee katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Thika United ya Kenya.
Katika mechi hii iliyoanza saa 11:00 jioni, Jaja aliandika bao hilo katika dakika ya 60 ya mchezo.
Jaja ameweza kumfunika Mbrazil mwenzake, Andrey Coutinho aliyoonekana kuwa moto wa kuotea mbali katika mechi tatu zilizopita.
Coutinho
aliifungia Yanga mabao 2 katika mechi tatu alizocheza Zanzibar wakati
Jaja alifunga moja dhidi ya Chipukizi FC uwanja wa Gombani Pemba.
Cuutinho aliitungua Shangani na KMKM, Yanga ikishindi mabao 2-0 kwa kila mechi.
Lakini leo Jaja alitulia na kumzidi kete Coutinho aliyetarajia kuwavutia mashabiki wengi wa Yanga.
Maximo
aliwaanzisha pamoja Jaja, Saimon Msuva na Coutinho katika safu ya
ushambuliaji, wakati Haruna Niyonzima na Mbuyu Twite walianza katikati.
Winga
ya kulia alianza Hassan Dilunga. Safu ya ulinzi walianza Juma Abdul,
kulia, Oscar Joshua, kushoto na mabeki wa kati walianza Nadir Haroub na
Kelvin Yondani.
No comments:
Post a Comment