Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Thursday, September 4, 2014

JAJA AONESHA UWEZO WAKE YANGA IKIITANDIKA THIKA UNITED

  • Written by  Tupambane Blog
  • Email
  • Tuma Maoni
  • Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter 
10624911_689578434453205_8031115781331621810_n
MBRAZIL Geilson Santos Santana ‘Jaja’ kwa mara ya kwanza akicheza katika uwanja wa kisasa wa Taifa jijini Dar es salaam amefanikiwa kuifungia Yanga bao pekee katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Thika United ya Kenya.
Katika mechi hii iliyoanza saa 11:00 jioni, Jaja aliandika bao hilo katika dakika ya 60 ya mchezo.
Jaja ameweza kumfunika Mbrazil mwenzake, Andrey Coutinho aliyoonekana kuwa moto wa kuotea mbali katika mechi tatu zilizopita.
Coutinho aliifungia Yanga mabao 2 katika mechi tatu alizocheza Zanzibar wakati Jaja alifunga moja dhidi ya Chipukizi FC uwanja wa Gombani Pemba.
Cuutinho aliitungua Shangani na KMKM, Yanga ikishindi mabao 2-0 kwa kila mechi.
Lakini leo Jaja alitulia na kumzidi kete Coutinho aliyetarajia kuwavutia mashabiki wengi wa Yanga.
Maximo aliwaanzisha pamoja Jaja, Saimon Msuva na Coutinho katika safu ya ushambuliaji, wakati Haruna Niyonzima na Mbuyu Twite walianza katikati.
Winga ya kulia alianza Hassan Dilunga. Safu ya ulinzi walianza Juma Abdul, kulia, Oscar Joshua, kushoto na mabeki wa kati walianza Nadir Haroub na Kelvin Yondani.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG