Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Friday, September 19, 2014

Li Na astaafu tenisi

Li Na astaafu tenisi
Mchezaji wa kwanza wa Uchina kuwahi kushinda mashindano ya tenisi Grand Slam, Li Na, amestaafu.
Li, ambaye sasa ana umri wa miaka 32, alisema kuwa anaondoka katika mashindano ya tenisi kwa sababu ya majeraha ya muda mrefu, hasa kwenye magoti yake.
Alishinda Grand Slams mara mbili - Frenc Open mwaka 2011 na Australian Open mwaka huu.
Chama cha Tenisi nchini Uchina kimepongeza juhudi zake za kuimarisha mchezo huo nchini mwake.
Hata hivyo waandishi wa habari wanasema kuwa chama cha tenisi cha Uchina hakikubaliana naye mara kwa mara jinsi alivyoendesha mambo yake ya tenisi.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG