Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Ephraim Mafuru
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafala ya
kumtangaza msanii wa Marekani TI ambaye atashiriki tamasha la Fiesta
litakalofanyika mwezi ujao jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki
wa Kimarekani katika miondoka ya Hip-hop ambaye pia ni mtayarishaji wa
muziki, mwigizaji na mwekezaji, Clifford Joseph Harris Jr, alimaarufu
kama T.I. amethibitishwa rasmi na kampuni ya Serengeti Breweries Ltd
(SBL)kama mwanamuziki wa kimataifa atakayetumbuiza katika kilele cha
shangwe za Serengeti Fiesta zitakazofanyika jijini Dar es salaam tarehe
18 Oktoba mwaka huu.
Katika
mkutano na waandishi wa habari uliofanyika makao makuu ya SBL, Meneja
Masoko Allan Chonjo alisema, ” hivi karibuni tumetia saini na
kukamilisha mikataba yote ili kuhakikisha kwamba mwanamuziki huyu wa
kimarekani anafika Leaders Club jijini Dar essalaam tarehe husika”
Chonjo aliendelea kusema, ‘Tungependa kuwashukuru washirika wetu, Prime
Time Promotions kwa kuhakikisha tunakamilisha mikataba yote na vile vile
kwa kuhakikisha kamba tamaha hili linakamilika kwa mafanikio. Hii
itakuwa ni mara ya kwanza kwamba T.I kutia mguu wake katika ardhi ya
Tanzania.(T.K)
Akizungumza
na vyombo vya habari, Sebastian Maganga kutoka Prime Time Promotions,
alikuwa na haya ya kusema, “kwa miaka kadhaa sasa tumekuwa tukihakikisha
kwamba tunaelewa nini watanzania wanataka na tumekuwa tukijitahidi bila
kuchoka kuhakikisha kamba tukio tunalolifanya, kwa mwaka huu, wapenzi
wetu watashuhudia shoo ya nguvu ambayo haijawahi yanyika hapa nchini.
“mpaka sasa, Serengeti imetembelea mikoa kumi (10) nchini, na itaendelea
na ziara hiyo katika mikoa ya Singida, Songea, Mtwara, Dodoma na Mbeya.
Mkurugenzi wa Prime Time na meneja wa vipindi wa Radio Clouds FM Ruge
Mutahaba akizungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Serena
jijini Dar es Salaam kuhusu ujio wa mwanamuziki wa Marekani TI
atakayeshiriki tamasha la Fiesta litakalofanyika Dar es Salaam mwezi
ujao.
Katika
mabadiliko mengine Serengeti Breweries na Prime Time Promotions
wamewaomba mashabikiwachague msanii wa kitanzania ambaye wangependa
atumbuize na TI. “Hiki ni kitu kipya natunataka kuhakikisha kwamba
mashabiki wanaburudika vya kutosha, alisema Maganga. ‘Habari
zitasambazwa kwa njia ya TV na redio kuelezea jinsi ya kushiriki’,
aliongeza. Serengeti Fiesta inatambulika kwa kuleta wasanii wa
kimataifa hapa nchini, miongoni mwao ni pamoja na Rick Ross, Shaggy na
Davido T.I aliyetamba na kibao “No Mediocre” amekuwa akijishughulisha na
shughuli mbalimbali ikiwemo biashara. Yeye ni muasisi na mkurugenzi
mkuu wa Grand Hustle Records.
T.I.
alianza kupata umaarufu mwaka 2003, baada ya kushirikishwa na
mwanamuziki mwenzake Bone Crusher, ambaye ni mkazi wa Atlanta, katika
wimbo wa “Never Scared”. Alipata umaarufu zaidi baada ya kutoa wimbo
wa Trap Muzik (2003). Mwaka 2004, T.I. alionekana kwenye wimbo wa
Destiny’s Child’s “Soldier”, sambamba na Lil Wayne.
Albamu ya
sita ya TI, Paper Trail (2008), ilikuwa albamu yake ya mafanikio zaidi ,
na imefanikiwa kuuza nakala 568,000 katika wiki ya kwanza nchini
Marekani na kuifanya ya tatu katika chati ya albam bora nchini humo.
Mpaka sasa, T.I. amdeshinda tuzo tatu za Grammy Awards. T.I. pia ametoa
nyimbo kama vile”Bring Em Out”, “What You Know”, “Swagga Like Us”
(akimshirikisha Kanye West, Jay-Z and Lil Wayne), “Dead and Gone”
(akimshirikisha Justin Timberlake), “Ball” (akimshirikisha Lil Wayne)
and “No Mediocre” (akimshirikisha Iggy Azalea).
Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya Serengeti Ephraim Mafuru
(kushoto) akimpongeza Mkurugenzi wa Prime Time Ruge Mutahaba wakati wa
kumtangaza mwanamuziki wa Marekani TI atakayeshiriki tamasha la Fiesta
mwezi ujao jijini Dar es Salaam.
Meneja
wa Masoko wa Kampuni ya Serengeti Allan Chonjo akizungunza na waandishi
wa habari (hawapo pichani) wakati wakimtangaza mwanamuziki TI
atakayeshiriki tamasha la Fiesta litakalofanyika jijini Dar es Salaam
mwezi ujao.
Mkurugenzi Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya Serengeti (SBL) Ephraim Mafuru
(katikati) pamoja na Meneja wa Bia ya Serengeti Rodney Rogamba (kushoto)
na meneja masoko Allan Chonjo wakati wa kumtambulisha mwanamuziki wa
Marekani TI atakayeshiriki tamasha la Fiesta. Hafla hiyo ilifanyika
katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Masoko ya Kampuni ya Serengeti (SBL), Ephraim Mafuru
(wa pili kulia), Mkurugenzi wa Prime Time Ruge Mutahaba ( wa tatu
kushoto), meneja wa bia ya Serengeti Rodney Rugambo (wa pili kutoka
kushoto), Elihuruma Ngowi (kushoto) na kulia ni meneja masoko wa
Serengeti Allan Chonjo, wakati wakitangaza ujio wa mwanamuziki wa
Marekani TI akayeshiriki katika tamasha la Fiesta litakalofanyika Oktoba
18 jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment