Rais wa
shirikisho la soka barani Ulaya UEFA Michel Platini amesisitiza kuwa
hatorejesha saa yenye thamani ya Yuro elfu kumi na sita aliyopewa kama
zawadi na shirikisho la soka nchini Brazil CBF.
Shirikisho la soka
duniani FIFA limewataka maafisa wote waliopewa saa hizo katika kombe la
dunia kuzirudisha kwa kuwa zawadi hizo zinakiuka maadili ya sheria za
FIFA.Lakini Platini mwenye umri wa miaka 59 amesema yeye hawezi kurudisha zawadi.
Platini amesema kuwa FIFA ilikuwa na habari kwamba zawadi hizo zilitolewa mnamo mwezi juni ,lakini akashangazwa ni kwa nini shirikisho hilo halikuchukua hatua wakati huo.
Saa hizo zilitolewa na mmoja ya wafadhili wa shirikisho la soka
No comments:
Post a Comment