Huu ni usafiri ambao naamini kuwa mtanzania yeyote ameutumia lakini pia hata kama hajatumia basi atakuwa anaufahamu.
Tanzania kuna magari lakini pia kuna usafiri aina ya tela ambao kule kwetu singida unatumika sana kubeba mizigo kama vile mchanga,mawe, matofali N.K
Lakini pamoja na kubeba mizigo hiyo pia hutumika kubeba watu ambao ndio waongozaji wa usafiri huo.
Nakumbuka mwaka 2009 ndo ilikuwa mara yangu ya mwisho kutumia usafiri huu wakati nikiwa kijijini kwetu Msisi Kata ya New Kiomboi Tarafa ya Kisiriri, Wilaya ya Iramba nikiwa nimebeba mbolea kutoka nyumbani kupeleka shambani karibu kilomita 15.
Safari ni hatua Tanzania hatuhitaji gharama kubwa ya kununua usafiri bali gharama ya kawaida tu kama vile TELA
No comments:
Post a Comment