Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Thursday, October 16, 2014

Alichosema Nooij kuhusu Samatta kifanyiwe kazi


Mbwana Samatta 


Posted  by tupambane blog
In Summary
Ni hivi majuzi tu vyombo vya habari vilitawaliwa na habari ya aibu kuhusu Mashindano ya Wizara na Idara za Serikali (Shimiwi) baada ya timu ya Mchezo wa Pete (netiboli) ya Uchukuzi kuondolewa mashindanoni katika hatua ya nusu fainali.
KATIKA sekta ya michezo nchini lipo tatizo kubwa la udanganyifu ambao hufanywa na wanaojidai wanamichez
Ni hivi majuzi tu vyombo vya habari vilitawaliwa na habari ya aibu kuhusu Mashindano ya Wizara na Idara za Serikali (Shimiwi) baada ya timu ya Mchezo wa Pete (netiboli) ya Uchukuzi kuondolewa mashindanoni katika hatua ya nusu fainali.
Timu hiyo iliyoibuka mshindi katika mchezo huo iliondolewa ilipobainika kuwatumia wachezaji mamluki katika mechi yao na timu ya netiboli ya Mahakama.
Tukio kama hilo linaonyesha ni vipi Watanzania wanaamua kujidanganya wenyewe hata katika mashindano yaliyoandaliwa kwa ajili ya kujifurahisha na kujumuika pamoja nje ya shughuli zao za kila siku za maofisini.
Katika soka mchezo unaopendwa na wengi nao umetawaliwa na hujuma na udanganyifu wa kila aina mambo ambayo tunaamini ni sehemu ya tatizo au kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya mchezo huo.
Katika soka usiposikia hujuma za wizi wa tiketi, utasikia hujuma za kupanga matokeo, usiposikia hujuma za wachezaji kununuliwa utasikia hujuma za waamuzi kuhongwa.
Haya ni baadhi ya matatizo ambayo ni muhimu yakadhibitiwa ili harakati za maendeleo ya soka ziweze kufikia malengo yanayokusudiwa.
Kati ya yote hayo udanganifu ambao umekuwa ukitukera mara kwa mara ni ule wa kudanganya umri kwa wachezaji, jambo ambalo hufanyika mara kwa mara katika mashindano mbalimbali ya vijana wadogo yenye lengo la kuibua vipaji.
Hili kwa sasa ni tatizo sugu ambalo linakwamisha juhudi za kuibua vipaji na kibaya ni kwamba hazionekani dalili zozote za kukabiliana na tatizo kwa nia ya kulimaliza.
Nia ya kuyazungumzia yote haya ya udanganifu na hujuma ni kuweka msisitizo katika hoja iliyotolewa hivi karibuni na Kocha wa Taifa Stars, Mart Nooij aliyelalamikia kitendo cha timu hiyo kumtegemea mno Mbwana Samatta.
Nooij alisema kwamba ni vyema juhudi zikafanyika kuibua vipaji vya wachezaji ili kuachana na utegemezi wa mchezaji mmoja.
Ni ukweli ulio wazi kwamba mshambuliaji huyo anayeichezea Klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni mchezaji mzuri na tegemeo katika Taifa Stars.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG