Mwanachama wa zamani wa Chadema, Batuli Abdallah akijieleza mbele ya wanahabari (hawako pichani)
Yassin Bahama aliyekuwa mwanachama wa zamani wa Chadema akizungumza.
Mohamed Ngulangwa aliyekuwa mwanachama wa zamani wa CCM akivaa fulana ya chama hicho.(T.K)
Wajumbe waliohudhuria mkutano.
Mwenyekiti wa ACT, Hamis Chambuso akiwa ameshika kadi za Chadema zilizorudishwa na wanachama hao wapya.
Wajumbe na wanahabari wakiwa mkutanoni.
CHAMA cha
siasa hapa nchini cha Alliance for Change and Transparency ‘ACT, leo
kimewapokea wanachama wapya ambao wamehama toka vyama mbalimbali vya
siasa nchini.
Waliopokelewa
ni Yassin Bahama aliyekuwa mjumbe wa serikali ya mtaa wa matofalini,
Ujiji Kigoma, Batuli Abdallah aliyekuwa Katibu Mwenezi Bavicha katika
Jimbo la Kawe, Ofisa na mwasisi wa chama cha Chauwa, Sylvester Kasonga
pamoja na Engineer Mohammed Ngulangwa toka Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza
mbele ya GPL, eneo la Msasani Club, jijini Dar, Mwenyekiti wa Mkoa wa
ACT, Hamis Chambuso amewakaribisha na kuwapongeza wanachama hao wapya
kwa hatua waliyoichukua.
No comments:
Post a Comment