Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Friday, October 10, 2014

England yaisambaratisha San Marino 5-0

  • Written by  Tupambane Blog
  • Share on facebook Share on gmail Share on twitter 
Timu ya England imefanikiwa kupata ushindi mara mbili katika michezo miwili ya kundi E ya kufuzu kucheza michuano ya bara la Ulaya ya mwaka 2016 baada ya kupata ushindi mnono wa 5-0 dhidi ya San Marino.
England alianza kuvuna magoli kupitia kwa mlinzi wake Phil Jagielka aliyefunga katika dakika ya 24 kwa mpira wa kichwa kabla ya Wayne Rooney kuongeza bao la pili kwa njia ya penalti katika dakika ya 43 kutoka na madhambi ya mchezaji wa San Marino Andy Selva.
Naye mshambuliaji Danny Welbeck alifanikiwa kutumbukiza goli la tatu kwenye dakika ya 49. Goli hili lilitokana na mpira wa pasi kutoka kwa mchezaji mwenzake wa Arsenal ambaye aliingia kipindi cha pili Alex Oxlade-Chamberlain.
Andros Townsend aliiongezea timu yake ya England goli la nne kwa mkwaju wa mbali kabla ya Alessandro Della Valle kujifunga mwenyewe kutokana na kugongwa na mpira uliopigwa na Rooney.
Matokeo ya michezo mingine: Belarus 0: Ukaraine 2, Macedonia 3: Luxembourg 2, Slovakia 2: Spain 1, Lithuania 1:Estonia 0, Slovenia 1: Switzerland 0, Liechtenstein 0: Montenegro 0, Moldova 1:Austria 2, Sweden 1: Russia 1

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG