Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Tuesday, October 21, 2014

Mapigano yaanza tena Nigeria

Boko Haram
Taarifa kutoka Kaskazini Mashariki mwa Nigeria zinasema zaidi ya watu ishirini wameuawa katika mapigano kati ya wanajeshi na wanamgambo wa kundi la Boko Haram, licha ya makubaliano ya kusitisha vita kufanyika ijumaa iliyopita.
Vurugu zilifanyika siku ya katika mji wa Damboa. Makubaliano ya kusitisha vita kati ya wanamgambo wa Boko Haram na serikali ya Nigeria yanatarajiwa kuwaokoa wasichana zaidi ya mia mbili waliotekwa na kikundi hicho mwezi Aprili mwaka huu.
Mwandishi wa BBC nchini Nigeria anasema mapigano hayo yameleta hali ya wasiwasi kuhusiana na uwezekano kusitisha mapigano hayo.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG