Makala: SHANI RAMADHANI
MWANAMUZIKI
mahiri wa muziki w Bongo Fleva nchini, Sande Mangu ‘Linex’ au ‘Voa’
amesema kabila lake linamsababisha kupata ‘tone’ ambayo mtu mwingine
hana na kuna baadhi ya wasanii ambao wanatamani wawe wanajua lugha za
kwao.GPL(P.T)
Host wa kipindi cha Mtu Kati cha Global TV Online, Pamela Daffa (kushoto) akifanya mahojiano na msanii wa Bongo Fleva, Linex (kulia).
Akihojiwa
na safu hii, huku akirekodiwa na ‘kruu’ ya Global Tv Online mwishoni
mwa wiki iliyopita katika Chumba cha Habari cha Global Publishers, Linex
alisema asingekuwa mwanamuziki angekuwa askari, ifuatayo ni sehemu ya
mahojiano ambayo pia unaweza kuyapata kupitia tovuti ya www.globaltvtz.com .
Mwandishi: Huwa unajiita Voa, ni nini maana yake?
Linex:
Dah aisee Voa kirefu chake ni Voice of Africa yaani maana yake ni Sauti
ya Afrika niliamua kujiita hivyo kwa jinsi sauti yangu ilivyo na
ninavyoimba.
Mwandishi: Wewe ni kiongozi wa Kundi la Kigoma All Stars?
Linex:
Kigoma All Stars ni vijana kumi na kadhaa ambao ni maarufu na
wanaotokea sehemu (mji mmoja) walikutana mjini wakaamua kushirikiana na
kufanya kitu cha pamoja ambacho siyo lazima kifanyike tena.
Linex akifafanua jambo wakati wa mahojiano.
Mwandishi: Ilikuwaje mpaka mkaamua kufanya kitu kama kile, je huwa mnapeana sapoti katika kazi zenu?
Linex: Ni jinsi ambavyo binadamu tunaishi siyo kwamba watu tumefanya wimbo wa pamoja ndiyo tukawa tunasapotiana ile ni kazi na tulikutana kazini na kwenye maisha ya kawaida kila mtu anaweza kuwa na maisha yake.
Linex: Ni jinsi ambavyo binadamu tunaishi siyo kwamba watu tumefanya wimbo wa pamoja ndiyo tukawa tunasapotiana ile ni kazi na tulikutana kazini na kwenye maisha ya kawaida kila mtu anaweza kuwa na maisha yake.
Mwandishi: Una ukaribu gani na Mhe. Zitto?
Linex: Mh. Zitto naishi naye freshi yaani kama braza mtu ambaye anapenda sanaa zaidi kile ambacho ninakifanya na tumejuana kimjinimjini.
Linex: Mh. Zitto naishi naye freshi yaani kama braza mtu ambaye anapenda sanaa zaidi kile ambacho ninakifanya na tumejuana kimjinimjini.
Mwandishi: Ulishawahi kuwaga na mpenzi Mzungu, hatukuoni naye na wala hatusikii chochote vipi?
Linex:
Sasa hivi ninapenda maisha yangu yawe siri siyo lazima kila
ninachokifanya mtu ajue kwa sababu nimetokea kwenye maisha fulani ya
kushindwa kumudu hata tumbo langu mwenyewe na hata nauli ya daladala,
Mzungu alikuwepo juzi tu hapa Bongo kakaa kama mwezi hivi kaondoka.
Mwandishi: Vipi kuna usumbufu wowote unoupata kutoka kwa wadada wa mjini?
Linex: Aaah! Mi sipati usumbufu wowote labda kwa sababu siishi maisha fulani ya hivyo mimi naishi maisha ya kawaida tu.
Linex: Aaah! Mi sipati usumbufu wowote labda kwa sababu siishi maisha fulani ya hivyo mimi naishi maisha ya kawaida tu.
Pamela Daffa katika pozi na Linex baada ya kipindi cha Mtu Kati.
Mwandishi: Kuna kipindi ulikuwa kama umetibuana na Mzungu, mlishamaliza tofauti zenu?
Linex: Yaa ni kweli nilikuwa na tatizo kweli na Mzungu na alivyokuja hapa tumemaliza tofauti zetu na tuko pamoja na sasa hivi yeye karudi zake Ulaya na mimi nipo Bongo maisha yanaenda.
Linex: Yaa ni kweli nilikuwa na tatizo kweli na Mzungu na alivyokuja hapa tumemaliza tofauti zetu na tuko pamoja na sasa hivi yeye karudi zake Ulaya na mimi nipo Bongo maisha yanaenda.
Mwandishi: Ulimpa mimba msichana halafu ukawa hujui kama mimba ni yako, vipi mwanao sasa hivi?
Linex: Unajua siku zote mzazi anatakiwa awe ‘proud’ na mtoto wake hata familia yake lakini kuna vitu fulani kama vinanishinda na ninajitahidi sana kutoa sapoti kwa mama yake na nilimwambia tufanye mpango kwa sababu yule mtoto mpaka leo hatumii jina langu anatumia jina la mtu mwingine na ana umri wa miaka nane mpaka sasa.
Linex: Unajua siku zote mzazi anatakiwa awe ‘proud’ na mtoto wake hata familia yake lakini kuna vitu fulani kama vinanishinda na ninajitahidi sana kutoa sapoti kwa mama yake na nilimwambia tufanye mpango kwa sababu yule mtoto mpaka leo hatumii jina langu anatumia jina la mtu mwingine na ana umri wa miaka nane mpaka sasa.
Mwandishi: Ulijuaje kama mtoto ni wako?
Linex: Unajua nimeletewa mtoto akiwa na miaka saba, nami sijakataa na wala sikutaka mambo ya DNA kwa sababu nilivyomuona niligundua ni wangu kabisa na hata mama yangu pia.
Mwandishi: Unatoa sapoti ya kutosha kwa mwanao?
Linex: Unajua nimeletewa mtoto akiwa na miaka saba, nami sijakataa na wala sikutaka mambo ya DNA kwa sababu nilivyomuona niligundua ni wangu kabisa na hata mama yangu pia.
Mwandishi: Unatoa sapoti ya kutosha kwa mwanao?
Mfanyakazi wa Global, Clarence Mulisa (kulia) akiongea jambo na Linex baada ya mahojiano.
Linex:
Ninasapoti kwa kiasi kidogo kwa vitu vidogovidogo na nilimwambia mama
yake kama yuko tayari tufanye mpango mtoto abadilishwe jina kwa sababu
mimi ni baba yake napambana na kazi, kila siku silali muda mwingine
nakesha studio narekodi kwa hiyo ninaweza kumpa maisha mazuri dogo naye
asije kupita katika njia ambazo nilipita mimi.
Mwandishi: Mwanao yuko Kigoma au Dar es Salaam?
Linex: Yupo hapahapa Dar.
Mwandishi: Ulimzingua sana mama mtoto wako mpaka akaamua kufanya hivyo nini?
Linex: Yupo hapahapa Dar.
Mwandishi: Ulimzingua sana mama mtoto wako mpaka akaamua kufanya hivyo nini?
Linex:
Hapana, ilivyotokea hiyo kitu tulipoteana halafu alikuwa katika mipango
ya kuolewa na alivyoolewa jamaa akaja kugundua kuwa mtoto hakuwa wake
wakawa wana tofauti, baadaye wakaja kuachana mtoto akiwa na miaka mitano
na amekuja kunitafuta tayari mtoto akiwa na miaka nane.
No comments:
Post a Comment