Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Tuesday, October 7, 2014

MWANAFUNZI AUAWA KISHA KUPORWA PIKIPIKI

  • Written by  Tupambane Blog
  • Share on facebook Share on gmail Share on twitter 
rpc_c7169.jpg
Kamanda wa Polisi mkoani Iringa (RPC),Ramadhani Mungi
Na Thommy kundy, Iringa
Mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Lugalo ameuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali kichwani na watu wasiofahamika kisha kupora pikipiki yake ambayo haijafahamika namba za usajili.
Kamanda wa Polisi mkoani Iringa (RPC),Ramadhani Mungi amewaambia waandishi wa habari ofisini kwake leo kuwa Salehe Khamis (18) aliuawa tarehe 06/10/2014 majira ya saa 6:15 usiku katika Kitongoji cha Kikungwe Igumbilo, Kata ya Ruaha Manispaa ya Iringa.(Thommy kundy)
RPC alisema kuwa chanzo cha mauaji hayo ni pamoja na kuwania mali, ambapo hata hivyo, watuhumiwa wanatafutwa na jeshi la polisi.
Wakati huohuo, Jeshi la Polisi mkoani Iringa linamshikilia mmoja dereva wa lori aina ya Isuzu kwa kusababisha kifo cha mtembea kwa miguu huko katika Kijiji cha Itimbo Kata ya Ihimbo, Tarafa ya Kilolo mkoani Iringa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi alimtaja marehemu kuwa ni Linus Mwirafi (45) mkazi Kijiji cha Itimbo kwa kudondokewa na lori hiyo baada ya kupinduka.
Alisema kuwa gari hilo lenye namba za usajili T 244 CNK aina ya Isuzu likiendeshwa na Yoktani Kikula (25) mkazi wa Ipogolo lilipunduka na kumdondokea mtembea kwa miguu huyo na kusababisha kifo chake papo hapo.
RPC alisema kuwa tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 05/10/2014 majira 06:00hrs katika kijiji cha Itimbo wilayani Kilolo, mkoani Iringa, na kuongeza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi na dereva amekamatwa.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG