- Written by Tupambane Blog
- Tuma Maoni
-
Share on facebook Share on gmail Share on twitter
Mkuu wa
idara ya data na vifaa vinavyotumia intarnet kutoka Tigo, David Zacharia
akielezea wateja watakavyotumia huduma hiyo kwa urahisi.
Mkuu wa ukuaji na ushirikiano wa mitandao ya kijamii kutoka Tigo, Naheed Hirji, akielezea upatikanaji wa huduma hiyo.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhulia hafla hiyo.
KAMPUNI ya
mtandao wa Tigo, imetangaza rasmi ushirikiano kati yao na mtandao wa
kijamii wa Facebook ambapo itatoa ofa ya Intaneti itakayotumiwa kwa bei
nafuu kupitia ‘application’ maalum ya Intaneti Organisation.
Tigo pia
inatoa fursa ya wateja kununua simu za kisasa ‘smartphones’ kwa bei
nafuu, ili kupata huduma bora ya intaneti na tovuti za huduma kama
vile elimu, afya, habari na mitandao ya kimawasiliano zitakazopatikana
bila malipo
Akizungumza
na kwenye mkutano na waandishi wa habari mapema leo jijini Dar, mkuu wa
idara ya data na vifaa vinavyotumia intaneti kutoka Tigo, David
Zacharia, alisema ushirikiano wao na Facebook utaongeza matumizi ya
tekinolojia ya kidijitali nchini kwa Watanzania wengi kutumia mtandao wa
intaneti.
(Habari/Picha: Musa Mateja/GPL)
No comments:
Post a Comment