Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Saturday, October 18, 2014

USA:Hatuamini mkataba na Boko Haram

Marekani inasema kuwa haina thibitisho lolote kuhusu mkataba wa kusitisha mapigano uliotangazwa kati ya jeshi la Nigeria na kundi la wanamgambo wa Boko Haram.
Msemaji wa rais nchini Nigeria amesema kuwa makubaliano hayo yalihusu kuachiliwa kwa zaidi ya wasichana 200 wa shule waliotekwa na Boko Haram miezi sita iliyopita.
Boko Haram
Lakini hata hivyo Boko Haram hawajasema lolote lakini mwandishi wa habari raia wa Nigeria anayeishi uhamishoni na anayehusishwa na Boko Haram anasema kuwa kundi hilo limekasirishwa kutokana na kile alichokitaja kuwa njama za kisiasa.
Makubaliano hayo yaliafikiwa baada ya wiki kadha za mazungumzo yalioongozwa na Chad na mikutano zaidi inahitajika ili kuafikia jinsi wasichana hao watakavyoachiliwa.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG