Katibu Mkuu,
Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Bibi Sophia Kaduma akitia sahini
utekelezaji wa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na Wabia wa
Maendeleo ili kusukuma kwa pamoja malengo ya SAGCOT, kushoto kwake ni
Bibi, Hanne- Marie Kaarstad, Msimamizi Mkuu wa maendeleo kutoka Ubalozi
wa Norway na anayefuatia ni Bwana Eric Beaume, kutoka Idara ya
Mahusiano ya Jumuia ya Ulaya.
Wabia wa Maendeleo wakiongozwa na Bwana
Philippe Dongier, Mkurugenzi Mkazi wa Bank ya Dunia nchini, leo wametia
sahini ya makubaliano ya kuisaidia SAGCOT, makubaliano hayo ni
utekelezaji wa ahadi za wabia hao ili kufanikisha utekelezaji wa
majukumu ya Mpango huo.
SAGCOT ni kifupi cha maneno, chenye maana ya
Southern Agricultural Growth Corridor Growth of Tanzania tafsiri yake
ni Mpango wa Kuboresha Kilimo Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini
ilianzishwa miaka mitatu iliyopita leo lake kubwa na kusaidi uwekezaji
mkubwa na mdogo katika kilimo kwa kushirikiana na sekta binafsi.
Awali katika hotuba yake ya ufunguzi wa tukio
hilo, Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Bibi Sophia
Kaduma alisema kutiliana sahini ni mwanzo mzuri, kwani Serikali kwa
kushirikia na sekta binafsi, maendeleo katika sekta ya kilimo
yatafikiwa kwa haraka.
Bibi Kaduma alisema, lengo la Serikali ni
kupunguza umaskini, kuboresha maisha ya watu vijijini na mijini na
kuongeza kuwa kiasi cha dola bilioni 2.1 za Marekani ambazo zitawekezwa
kupitia Mpango huo zitachangia katika ukuaji wa uchumi kupitia kilimo.
Naye Bwana Vel Gnanendran, Mwakilishi wa
Mkazi wa DFID alisema huu ni mwanzo mzuri na tukio la kutiliana sahini
ni mwanzo mzuri na kwamba wabia wa maendeleo wapo mstali wa mbele
kuhakikisha, malengo ya SAGCOT yanafikiwa ikiwa ni pamoja na kuboresha
utendaji kazi wa Mpango huo.
Bwana Geoffrey Kirenga, ambaye ndiye Mtendaji
Mkuu wa SAGCOT alisema, Mpango huo unatekelezwa kwa pamoja kati
Serikali kwa kushirikiana na wabia wa maendeleo na kuishukuru Serikali
kwa kuja na mtazamo mpya wa kuishirikisha Sekta binafsi katika kukuza
na kuendeleza uchumi wa Taifa.
Bwana Kirenga aliongeza kuwa, sasa ni wakati
wa kila Mtanzania kubadili fikra kwa kuwa, maendeleo yanaletwa kwa
ushirikiano kati ya Serikali na Sekta binafsi, na kushauri Watanzania
kuacha fikra za kusubiri kusaidiwa.
Bwana Kirenga alisema mpaka sasa, wabia wa
maendeleo wametoa ahadi ya kiasi cha Dola za Kimarekani, bilioni 1
ambazo zitatolewa punde ili kuanza utekelezaji katika eneo la usimamizi
na uratibu wa shughuli za SAGCOT.
No comments:
Post a Comment