Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Wednesday, October 1, 2014

Wakurdi Iraq wakomboa mpaka Syria

Wapiganaji wa kikurdi nchini Iraq
Wanajeshi wa kikurdi nchini Iraq wameripotiwa kurejesha tena mpaka muhimu kuingia nchini Syria kutoka kundi la dola la kiislam Islamic state .
Wapiganaji wa kikurdi walifanya shambulizi la mapema asubuhi katika eneo la Rabia, inayomiliki njia kuu inayounganisha Iraq na Syria.
Kulikuwa na makabiliano kutoka kundi la kiislam IS, ambapo watu takribani watano walijilipua kwa bomu ndani ya gari na kusababisha vifo vya wapiganaji muhimu kikurdish.
Ndege za kivita za Uingereza zifanya shambulizi la kwanza kwa kuwalenga wapiganaji wa dola ya kiislamu IS nchini Irang wakati ndege za kivita za Marekani ziliwashambulia wapiganaji hao karibu na mji wa Kobani nchini Syria.karibu na mpaka wa Uturuki ambapo mapigano makali yanaendelea kati ya wakrudi na wapiganaji wa IS.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG