Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Friday, November 28, 2014

Je, Biblia Inakataza Kufurahia Ngono? Jibu la Biblia


Biblia inaonyesha kwamba ngono ni zawadi kwa watu waliofunga ndoa, na hivyo haiwakatazi kufurahia ngono. Mungu alimuumba “mwanamume na mwanamke” na kuona kwamba kila kitu alichofanya “kilikuwa chema sana.” (Mwanzo 1:27, 31) Alipowaunganisha mwanamume na mwanamke wa kwanza katika ndoa, alisema hivi: “watakuwa mwili mmoja.” (Mwanzo 2:24) Muungano huo ungewawezesha wafurahie ngono na pia ungewafanya wawe na uhusiano wa karibu sana wa kihisia.
Biblia inafafanua furaha ambayo waume hupata katika ndoa inaposema hivi: ‘Shangilia pamoja na mke wa ujana wako .   . Na maziwa yake yakuleweshe nyakati zote. Upendo wake na ukufurahishe sikuzote.’ (Methali 5:18, 19) Pia, Mungu anataka wanawake wafurahie ngono. Biblia inasema hivi: “Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.”1 Wakorintho 7:3, Union Version.

Kanuni zinazohusu kufurahia ngono

Ni watu waliooana tu ambao Mungu anawaruhusu wafanye ngono, kama vile tunavyosoma katika Waebrania 13:4: “Ndoa na iheshimiwe kati ya wote, na kitanda cha ndoa kiwe bila unajisi, kwa maana Mungu atawahukumu waasherati na wazinzi.” Watu waliooana wanapaswa kuwa waaminifu na wanapaswa kuwajibika sikuzote kwa mmoja na mwenzake. Wanapata furaha nyingi sana, si kwa kujitanguliza wenyewe, bali kwa kufuata kanuni ya Biblia inayosema: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”Matendo 20:35.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG