Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Thursday, November 27, 2014

Mauaji ya weusi yaendelea Marekani

Tamir Rice aliyeuawa
Polisi katika mji wa Cleveland nchini Marekani, wameachilia video inayoonesha mauaji ya kijana wa miaka kumi na miwili akipigwa risasi mwishoni mwa wiki iliyopita.
Kipande hicho cha video kinamwonesha Tamir Rice akipigwa risasi sekunde chache tu gari la polisi lilipofika na kusimama pembeni yake katika eneo la tukio.
Polisi waliitwa katika eneo la michezo na mapumziko,na kuelezwa kuwa kuna watoto wanaocheza na bunduki bandia na hawakuelezwa ikiwa bunduki hizo zilikuwa halisi.
Polisi wanaeleza kuwa walimtaka Tamir Rice mara tatu kunyanyua mikono juu,akakaidi,lakini familia ya kijana huyo inaeleza kuwa kifo cha Tamir kingeweza kuepukwa,lakini polisi walikuwa wepesi kuamua kumpiga risasi, na wazazi hao wamewataka waandamanaji mjini humo kuwa na amani.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG