Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kilolo Seth Moto akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani).
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kilolo Iringa, Seth Moto, amewataka wanaohusika na sakata la Escrow aidha kwa kutajwa au kuchota fedha za akatunti hiyo wajitathmini na kijivua nyadhifa zao mapema wasisubiri kuondolewa au kufukuzwa na sheria na warudishe fedha zilizoibiwa.
Pia ametaka sheria ichukue mkondo wake kwani wananchi wamechoshwa na wizi huo unaofanya maisha yao kuwa magumu.
Pia Moto alishutumu tabia ya viongozi kujilimbikizia madaraka kama vile ubunge, uenyekiti wa wilaya na mkoa na ujumbe wa mikutano ya CCM.
No comments:
Post a Comment