Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Friday, November 21, 2014

Wanaotumia dawa michezoni wafungiwe


Varier Adams
Bingwa wa dunia Olimpik riadha Valerie Adams amependekeza kufungiwa maisha kwa mwanariadha atakayebainika kutumia dawa za kuongeza nguvu michezoni.
"Udanganyifu ni udanganyifu tu hauna muamana" amesisitiza Adams, akiongeza kuwa hata kama itakuwa ni kosa la kwanza adhabu iwe hiyo hiyo.
Kwa sheria za sasa anayebainika kutumia dawa hizo michezoni anafungiwa kutoshiriki michezo kwa miaka miwili,adhabu ambayo inatarajiwa kuongezeka hadi miaka minne hapo mwakani.
Adams ni mmoja wa wanariadha wanawake aliyetajwa na shirikisho la riadha IAAF kuwania tuzo kwa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG