Mwigizaji na muongozaji mkongwe wa filamu zakibongo, Jacob Stephen “JB” amefunguka na kumtajamwigizaji wa kike , Dianarose Kimary “Diana” kuwa ni moja kati ya waigizaji wa kike wanne anaowakubali.
“Kwangu mimi Diana kimaro atabaki kuwa mmoja kati ya waigizaji wanne wakike ninaowakubali”.
JB aliyasema haya wakati wakiwa “ON SET” kwa movie yake mpya inayoitwa KALAMBATI LOBO ambayo inafanyika chini ya kampuni yake mwenyewe ya Jerusalem Films. Diana ni moja kati ya waigizaji wanaoshiriki kwenye movie hiyo.
Alipoulizwa anawataje hao watatu wengine, JB alijibu kuwa atawaja siku nyingine.
No comments:
Post a Comment