Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Wednesday, December 17, 2014

KANUNI ZA UFUGAJI BORA WA MBUZI NA KONDOO

KANUNI ZA UFUGAJI BORA WA MBUZI NA KONDOO



1.. Utangulizi
Mbuzi na kondoo wanaweza kufugwa kwa gharama nafuu nakuishi katika mazingira magumu kama ya maradhi na ukame ikilinganishwa na ng’ombe. Kutokana na umbillao dogowanaweza kufugwa katika eneo dogo na pia wanaweza kuhudumiwa na familia yenye nguvukazi na kipato kidogo. Uzaowa muda mfupi unamwezesha mfugaji kupata mbuzi/kondoo wengikwa kipindi kifupi. Wanyama hao hufugwa kwa ajili ya nyama, maziwangozi, sufu na mazao mengine kwa matumizi ya familia nakuongeza kipato. Ufugaji bora wa mbuzi na kondoo uzingatie kanuni zifuatazo:-
i)       Wafugwe kwenye banda au zizi bora,
ii)      Wachaguliwe kutokana na sifa za koo/aina na lengo la uzalishaji
(nyama, maziwa au sufu),
iii)      Wapatiwe lishe sahihi kulingana na umri na mahitaji ya mwili,
iv)      Kuzingatia mbinu za kudhibiti magonjwa kama inavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo,
v)      Kuweka na kutunza kumbukumbu sahihi za uzalishaji; na
vi)      Kuzalisha nyama, maziwa au sufu yenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko

2. Zizi au Banda la Mbuzi/Kondoo

Mbuzi/kondoo wanaweza kufugwa katika mifumo ya huria, shadidi na kwa kutumia njia zote mbili. Zizi hutumikakatika mfumo huria ambapo mbuzi/kondoo
huchungwa wakati wa mchana na kurejeshwa zizini wakati wa usiku. Zizi bora nlillenye sifa zifuatazo:-
•    Lililo imara linaloweza kumkinga mbuzi/kondoo dhidi ya wanyama hatari na wezi,
•    Lililojengwa mahali pa mwinuko pasiporuhusu maji kutuama,
•    Ukubwa wa zizi uzingatie idadi na umri wa mifugo. Ni vema mbuzi/kondoo watengwe kulingana na umriwao; na
•    Liruhusu usafi kufanyika kwa urahisi.

Palambapo mbuzi/kondoo wanafugwa kwa mfumo wa shadidi hufugwa katika banda wakati wote. Bandabora la mbuzi/kondoo linatakiwa kuwa na sifzifuatazo:-
•    Imara, lenye uwezo wa kuwahifadhi kiafya na pia dhidi ya hali ya hewa hatarishi kwa mfano jua kali,upepo, baridi na mvua pamoja na wanyama hatari,
•    Lenye mwanga, hewa na nafasi ya kutosha inayoruhusu usafi kufanyika kwa urahisi,
•    Lijengwe sehemu isiyoruhusu maji kutuama na liwe mbali kidogo na nyumba ya kuishi watu. Pia ujenziuzingatie mwelekeo wa upepo ili hewa kutoka bandani isiende kwenye makazi,
•    Liwe na sakafu ya kichanja chenye urefu wa mita 1 kutoka ardhini (Kwa banda la mbuzi),
•    Liwe na sehemu ya kuwekea chakula, maji na mahali pa kuweka jiwe la chumvichumvi; na
•    Liwe na vyumba tofauti kwa ajili ya majike na vitoto, mbuzi/kondoo wanaokua, wanaonenepeshwana wanaougua.

3. Vifaa vya Kujengea na Vipimo vya Banda
Inashauriwa banda la mbuzi/kondoo lijengwe kwa kutumia vifaa vinavyopatikana kwa urahisi katika eneo husika. Ukubwa wa  banda utategemea idadi  ya

mbuzi/kondoo wanaofugwa humo na ukubwa wa umbo kama inavyoonekana kwenye Jedwali Na. 1
JedwalNa 1: Eneo la mbuzi/kondoo linalotakiwa
Kundla Mbuzi/Kondoo               Eneo kwa Mnyama Mmoja
(Mita2)
Vitoto                                                                  0.3
Wasio na mimba                                                  1.5
Wenye mimba                                                     1.9
Dume                                                                   2.8

•    Paa lijengwe kwa kutumia vifaa kama miti, mbao, na kuezekwa kwa nyasi, makuti, majani ya migomba, mabati au hata vigae kwa kutegemea uwezo wa mfugaji,
•    Kuta zijengwe kwa kutumia mabanzi, mbao, nguzo, wavu wa waya, fito na matofali. Kutziwe imarazinazoruhusu hewa na mwanga wa kutoshaMlango uwe na ukubwa wa sentimita 60 x 150,
•    Sakafu inaweza kuwa ya udongo au zege. Sakafu ya kichanja inaweza kujengwa kwa kutumia miti,fito, mianzi, mbao au mabanzi na iweze kuruhusu kinyesi na mkojo kupita. Chumba cha majike navitoto kiwe nnafasi ya sentimita 1.25 kati ya papi na papi, fito na fito au mti hadi mti. Chumba chambuzi/kondoo wakubwa iwe sentimita 1.9 kati ya mbao na mbao.

4. Uchaguzwa Mbuzi/Kondoo wa Kufuga
Madhumuni ya kuchagua mbuzi au kondoo wa kufuga ni kuboresha uzalishaji na kuendeleza kizazi bora. Kunaaina nyingi za mbuzi/kondoo wanaoweza kufugwa kulingana na mazingira na mahitaji ya mfugaji. Uchaguzihufanyika kwa kuangaliumbile, uzalishaji na kumbukumbu za wazazi kama vilumbo kubwa, ukuaji waharaka, uwezo wa kutunza vitoto na kutoa maziwa mengi.
Mbuzi wanaofaa kwa ajili ya maziwa ni aina ya Saanen, Norwegian na Toggenburg pamoja na chotara wao.

Mbuzi wanaofaa kwa ajili ya nyama nBoer na chotara wao, mbuzi wa asili kama vile Pare white, Newala na Ujiji.Mbuzi aina ya Malya (Blended) wanafaa kwa ajili ya nyama na maziwa. Aidha, kondoo aina ya
Aidha, kondoo aina ya Black Head Perrsian (BHP), Masai na Red Suffalk Hampshire wanafaa kufugwa kwa ajili yanyama. Merino na Lincoln hufugwa kwa ajili ya sufuwakati Corriedale na Romney hufugwa kwa ajili ya nyama nasufu. Hapa Tanzanikondoo wanaopatikana kwa wingi ni Black Headed Persian, Masai Red Dopper na kondoowengine wa asili.

Mbuzi/kondoo jike wanaofaa kwa ajili ya kuzalisha maziwa na nyama wawna sifzifuatazo:-
•    Historia ya kukua upesi, kuzaa (ikiwezekana mapacha) na kutunza vitoto vizuri,
•    Umbo la mstatili linaloashiria utoaji wa nyama nyingi; na
•    Asiwe na ulemavu wa aina yoyote

Sifa za Ziada kwa Mbuzwa Maziwa

•    Awe na miguu ya nyuma iliyo imara na iliyonyooka na yenye nafasi kwa ajili ya kiwele; na
•    Awe na kiwele kikubwa na chuchu ndefu zilizokaa vizuri
  Sifa za Dume

Dume bora awe na sifzifuatazo:-
•    Miguu iliyonyooka, imara na yenye nguvu,
•    Asiwe na ulemavu wa aina yoyote,
•    Mwenye uwezo na nguvu ya kupanda; na
•    Mwenye kokwa mbili zilizo kaa vizuri na zinazolingana
Angalizo: Dume lichaguliwe kwa makini kwa sababu “dume ni nusu ya kundi”.

5. Utunzajwa Vitoto vya Mbuzi/Kondoo
Utunzaji huanza mara tu baada ya kuzaliwaMfugaji ahakikishe:-
•  Kitoto cha mbuzi/kondoo kinapata maziwa ya mwanzo (dang’a) ndani ya masaa 24 tangu kuzaliwa nakwa muda wa siku 3,
•  Kama kinanyweshwa maziwa, kipewe lita 0.7- 0.9 kwa siku. Maziwa haya, ni muhimu kwani yana viinilishena kinga dhidi ya magonjwa,
• Iwapo mama hatoi maziwa au amekufa, inashauriwa kutengeneza dang’a mbadala au kama kunambuzi/kondoo mwinginaliyezaanaweza kusaidia kukinyonyesha kitoto hicho,
•    Kitoto cha mbuzi/kondoo kiendelee kunyonya kwa wiki 12 - 16. Wiki baada ya kuzaliwa, pamoja namaziwa, kianze kupewa vyakula vingine kama nyasi laini na chakula cha ziada ili kusaidia kukua kwatumbo. Aidha, kipewe maji wakati wote,
•    Vyombo vinavyotumika kulishia vinakuwa safi muda wote,
•    Kitoto cha mbuzi/kondoo kiachishwe kunyonya kikiwa na umri wa miezi 3 hadi
4 kutegemea afya yake; na
•    Vitoto vipatiwe kinga na tiba ya magonjwa kulingana na ushauri wa mtaalam wa mifugo.

6. Matunzo Mengine
Utambuzi

Mbuzi huwekewa alama ili atambulike kwa urahisi na kuwezesha utunzaji wa kumbukumbu zake. Shughuli hiihufanyika kwa mbuzi/kondoo akiwa na umri wa siku 3 - 14. Njia zitumikazo ni pamoja na:
•         Kuweka alama sikioni kwa kukata sehemu ndogo ya sikio,
•         Kumpa jina kwa wafugaji wenye mbuzi wachache,
•         Kumvisha hereni ya chuma au plastiki yenye namba kwenye sikio,
•         Kumvalisha mkanda wenye namba shingoni; na

•         Kuweka namba kwa kuunguza sehemu ya ngozi ya mbuzi. Pale mfugajanapotumia njia hiiinashauriwa aweke alama kwenye eneo ambalhalitaathiri ubora wa ngozi
Kuondoa vishina vya pembe

Mbuzi/kondoo aondolewe vishina vya pembe akiwa na umri kati ya siku hadi 14Visipoondelewa hukua nakusababisha kuumizana na kuhitaji nafasi kubwa
kwenye banda. Kazi hii ifanywe na mtaalam wa mifugo.
Kuhasi

Vitoto vya mbuzi/kondoo ambavyo havitatumika kwa ajili ya kuendeleza kizazi vihasiwe kabla ya kufikia umri wamiezi 3. Kazi hii ifanywe na mtaalam wa mifugo.

7. Utunzajwa Mbuzi/Kondoo wa Miezi 4 - 8

Mbuzi wa miezi 4 mpaka 8 ni walambao wameacha kunyonya mpaka umri wa kupandishwa kwa mara yakwanzaMbuzi wa umri huu wana uwezo wa kula aina mbalimbali za malisho kama nyasi, mikunde, miti malishona mabaki ya mazao wakati kondoo hupendelea zaidi nyasi fupi. Wakati wa kiangazi huhitaji kupatiwa chakulacha ziada au kupewa pumba znafaka mbalimbali, mashudu ya alizeti, pamba na dengu, majani ya mikunde yaliyokaushwa, madini na vitamini.
Katika ufugaji huria ni vema kuzingatia idadi ya mbuzi/kondoo inayoweza kuchungwa katika eneo, ainana hali ya malisho.

Ili mbuzi/kondoo aweze kukua na kufikia uzito wa kuchinjwa/kupevuka mapema, mfugaji anapaswa kufuatakanuni zufugaji bora zifuatazo:-
•    Kumpatia vyakula vya ziada kwa muda wa miezi 2 mfululizo kiasi cha kilo 0.2 –0.7 kwa siku kuanziaanapoachishwa kunyonya,
•    Kumpatia dawa ya kuzuia minyoo kila baada ya miezi 3 na kutoa kinga za magonjwa mengine kamaitakavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo,

•    Kuchanja na kuogesha ili kuzuia magonjwa mbalimbali,
•    Kukata kwato mara zinapokuwa ndefu; na
•    Kuhasi madume yasiyotumika kuzalisha.

8. Umri wa Kupandisha Mbuzi/Kondoo
Mbuzi/kondoo wakitunzwa vizuri wanaweza kupandishwa wakiwa na umri wa
miezi hadi 12 kwa mbuzi/kondoo walioboreshwa na miezi 18 hadi 24 kwa mbuzi wa asili kutegemea afya yake.Hathivyo, inashauriwa wapandishwe wanapofikiuzito wa kilo 12 au zaidi na wasipandishwe mbuzi/kondoo waukoo mmoja.
Dalilza joto

Mfugaji anashauriwa asimpandishjike kabla hajafikisha umri wa kupandwa wa miezi hadi 12 kwambuzi/kondoo walioboreshwa na miezi 18 hadi 24 kwa mbuzi wa asili hata kama ataonyesha dalili ya kuhitajidume. Mbuzi/kondoo aliyezaa anaweza kupandishwa siku 30-60 baada ya kuzaa. Mbuzi/kondoo aliyeko kwenyejoto huonyesha dalili zifuatazo:-
•    Hutingisha/huchezesha mkia,
•    Hupanda na kukubali kupandwa na wengine,
•    Hutoa ute mweupe ukeni,
•    Huhangaika mara kwa mara na kupiga kelele,
•    Hufuata madume,
•    Hamu ya kula hupungua,
•    Hukojoa mara kwa mara,
•    Uke huvimba na huwa mwekundu kuliko ilivyo kawaida; na
•    Kwa mbuzi anayekamuliwa hupunguza kiwango cha maziwa

Mbuzi/kondoo apelekwe kwa dume mara tu dalili za joto zinapoonekana kwanjoto hudumu kwa wastani wasiku (saa 48). Chunguztena dalili zjoto baada ya siku 1hadi 2na kama dalili hazitaonekana tena kunauwezekano mkubwa
kuwa   mbuzi/kondoo   amepata   mimba.   Mfugaji   apange   msimu   mzuri   wa mbuzi/kondoo kuzaaMsimumzuri ni mara baada ya mvua.

9.   Utunzajwa Mbuzi/Kondoo MwenyMimba

Kwa kawaida mbuzi/kondoo hubeba mimba kwa muda wa miezi 5. Utunzaji wa mbuzi/kondoo mwenye mimbani muhimu kwani ndiyo chanzo cha kupata vitoto vyenye afya bora. Mfugaji anashauriwa kufuata kanunizifuatazo:
•    Apatiwe vyakula vya ziada kilo 0.2 – 0.7 kwa siku ili kutosheleza mahitaji yake na kitoto kinachokuatumboni,
•    Apatiwe nyasi, miti malisho na mikunde mchanganyiko kilo 1.8 – 2.5 kwa siku.
Dalilza Mbuzi/Kondoo Anayekaribia Kuzaa

•    Huhangaika kwa kulala na kuamka mara kwa mara,
•    Sehemu ya nje ya uke hulegea,
•    Hujitenga na kundi na hutafuta sehemu kavu na yenye kivuli,
•    Hupiga kelele; na
•    Hutokwa na ute mzito ukeni.
Mfugaji akiona dalili hizi anashauriwa asimruhusu mbuzi/kondoo kwenda machungani, bali amtenge kwenyechumba maalum, ampatie maji ya kutosha na kumuandalia sehemu ya kuzalia.

10.  Utunzaji wa Mbuzi/Kondoo Anayenyonyesha
Mbuzi/kondoo anayenyonyesha huhitaji chakula kingi zaidi ili kukidhi mahitaji ya mwili na kuzalisha maziwa kwaajili ya kitoto/vitoto. Pamoja na nyasi, mikunde na majani ya miti malisho kilo 1.8 – 2.5 kwa siku ni muhimuapewe chakula cha nyongeza kilo 0.3 – 0.8 kwa kila lita ya maziwa inayoongezeka baada ya lita 2 na maji safi,salama na ya kutosha wakati wote.

Taratibu za Kuzingatia Katika Ukamuaji wa Mbuzi wa Maziwa
Lengo la ufugaji wa mbuzi/kondoo wa maziwa ni kupata maziwa mengi, safi na salama pamoja na mazaoyatokanayo na maziwaMambo muhimu ya kuzingatini:-
•    Sehemu ya kukamulia iwe safi na yenye utulivu,
•    Mbuzi/kondoo awe na afya nzuri, msafi, na kiwele kioshwe kwa maji safi ya uvuguvugu,
•    Mkamuaji asibadilishwe badilishwe awe msafi, mwenye kucha fupi na asiwe na magonjwa ya kuambukiza,
•    Vyombo vya kukamulia viwe safi; na
•    Maziwa ya mwanzo kutoka kila chuchu yakamuliwe kwenye chombo maalu(strip cup) ilikuchunguzugonjwa wa kiwele.

11. Utunzaji wa Dume Bora la Mbegu
Dume bora la mbegu ni muhimu litunzwe ili liwe na uwezo wa kutoa mbegu bora, kupanda na kuzalisha. Dumebora huanza kupanda akiwa na umri kati ya miezi.8 -
10 kwa mbuzi walioboreshwa. Katika msimu wa kupandisha dume moja liruhusiwe kupanda majike 40 hadi 50.Aidha, inashauriwa madume wenye umri wa miezi 8 –
9 waruhusiwe kupanda majike ambao ndio mara ya kwanza kupandwa.

Dume apatiwe:-
•    Malisho ya kutosha na vyakula vya ziada kiasi kisichopungua kilo 0.2 – 0.7 kwa siku na maji ya kutosha,
•    Majani ya miti malisho, mikunde na nyasi mchanganyiko na mabaki ya mazao; na
•    Kilo 0.45 hadi 0.za chakula cha ziada za nyongeza kwa siku kulingana na uzito wake na wingi wamajike anayopanda.wiki 2 kabla na baada ya kuanza kupanda.


12.    Matunzo Mengine

Kukata Mkia

Mara nyingine kondoo hukatwa mkia ili kuruhusu mtawanyiko mzuri wa mafuta katika misuli mwilini. Piakondoo aliyekatwa mkia huwa msafi. Kazi hii ifanywe kama itakavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo kwakutumia vyombo maalum. Inashauriwa mkia ukatwe urefu wa sentimita 2.5 – 3.8 kutoka kwenye shina la mkiawakati kondoo akiwa na umri wa siku 3 mpaka mwezi 1.
Kumnyoa Kondoo wa Sufu

Sufu hunyolewa wakati kondoo akiwa hai au amechinjwa. Kwa kawaidhunyolewa miezi hadi mwaka 1ambapo sufu huwa imefikia urefu wa sentimita
15 – 20. Vifaa vinavyotumika ni pamoja na mikasi au visu maalum. Uangalifunahitajika wakati wa kunyoa ilingozi ya kondoo isiharibike. Unyoaji ufanyike wakati wa kiangazi na siyo wakati wa mvua, kondoo akiwa namimba au kipindcha majani kutoa mbegu.

13.  Udhibitwa Magonjwa ya Mbuzna Kondoo
Magonjwa husababishwa na vimelea jamii ya virusi, bakteriaprotozoa na riketsiaMagonjwa menginehusababishwa na upungufu wa viinilishe, vitamini na protini. Dalili za mbuzi/kondoo mgonjwa ni pamoja na:-
 Manyoya husimama,
 Kuzubaa, kusinzia, kukohoa na kupiga chafya,
 Kukosa hamu ya kula na kunywa maji,
  Kujitenga na kundi,
  Kuvimba taya la chini,
  Kupumua kwa shida,
 Kutokwa na machozi na makamasi,
 Kuwa na upelau uvimbe kwenye sehemu ya mwili; na
 Kutupa mimba.
•    Hatua za haraka za kumuona mtaalamu wa mifugo zichukuliwe iwapo baadhi ya dalili hizizitaonekana,

•    Mbuzi na kondoo wachanjwe dhidi ya magonjwa ya homa ya maapafu.
Ugonjwa huu ni hatari sana na huenea kwa njia ya hewa na unaweza kusababisha vifo kati yaasilimia 60-100,
•    Kila baada ya miezi 6 mifugo ipatiwe kinga dhidi ya ugonjwa wa miguu na midomo na magonjwa mengine kama Kimeta, bondla ufa, kutupa mimbna chambavu (BQ) zitolewe kulingana na ushauri wa mtalaam wa mifugo,
•    Kama kuna wanyama walioathirika watengwe kwenye kundi, wasisafirishwe au kuuzwa,
•    Mbuzi/kondoo wapatiwe dawa ya minyoo Vitoto vya mbuzi/kondoo vipatiwe dawa ya minyoo vinapofikiaumri wa mwezi 1. Viendelee kupatiwa dawa ya minyoo kila mwezi hadi vinapofikia miezi na baada yahapo vipatiwe dawa ya minyoo kila baada ya miezi 3 - 4; na
•    Zingatia usafi wa banda ili kuwakinga na ugonjwa wa kuharisha na kuharisha damu na magonjwambalimbali.

14.  Utunzajwa Kumbukumbu za Mifugo
Kuweka kumbukumbu za mifugo ni muhimu katika uzalishaji kwa ajili ya kutambua kosaafu, gharama za utunzajina faida. Piahumsadia mfugaji kufanya maamuzi katika uendelezaji wa ufugaji wake. Mtalaamu wa mifugo piaanaweza kutumia kumbukumbu hizi ili kumsaidia mfugaji kuboresha ufugaji wake.
Kumbukumbu muhimu zinazohitajika kutunzwa ni:-
•    Kumbukumbu za idadi na ukuaji wa wanyama waliopo, jinsi zao, uzito wa mbuzi/kondo kwa  kil mwezi il kufuatili ukuaj wake tareh ya kuachishwa kunyonya na idadi ya waliouzwa,
•    Kumbukumbu ya uzazi zinazoonyesha tarehe ya kuzaliwa, namba yake, jinsi yake, aina (breed)namba yadume/jike, na uzito wa kuzaliwa,
•    Kumbukumbzupandishaj zinazoonyesh namba  ya  mbuzi/kondoanayepandwatarehe ya joto naya kupandwa, namba ya dume lililotumika kupanda, tarehe ya joto la pili kama atarudia na tarehe ya kuzaa,
•    Kumbukumbu   za   chanjo   na   matibabu   zinazoonyesha   namba   ya mbuzi/kondoo, tarehe yamatibabu, aina ya chanjo au ugonjwa, dawa iliyotumikaidadi ya waliokufa na waliopona na jina la mtaalamaliyetibu,
•    Kumbukumbu za maziwa zinazoonyesha namba ya mbuzi/kondoo, tarehe ya kuzaa, kiasi cha maziwa kwasiku, na kiasi cha maziwa kwa kipindi chotcha kukamuliwa, tarehe ya kuacha kukamua na idadi ya sikualizokamuliwa,
•    Kumbukumbu za mapato na matumizi zinazoonyesha mapato na matumizi, vitu vilivyouzwa au kununuliwakwa siku, kiasi cha fedha unachokuwa nacho kila wakati, kiasi cha fedha unachodai na kudaiwa.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG