Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Sunday, December 21, 2014

KWAYA MAALUM MBEYA YATINGA KAMBINI KUIBEBA KRISMASI

images
Na Mwandishi Wetu
KWAYA maalum jijini Mbeya wiki iliyopita iliingia kambini kwa siku moja kujiandaa na uzinduzi wa albamu yao ya Mubhopeghe Pa Finganilo (Kimbilieni kwenye ahadi) yenye nyimbo nane.
Kwa mujibu wa Mchungaji wa Kanisa wa EAGT, Zacharia Mwakasaka kambi hiyo inashirikisha waimbaji ambao ni Maaskofu, Wachungaji na viongozi mbalimbali wa dini waliomo kwenye Kwaya hiyo.
Mwakasaka alisema uzinduzi huo unashirikisha waimbaji, maaskofu na wachungaji waliopita kwenye mikono ya mzee Amulike Mwakiteka (84).
Mwakasaka alisema kupitia uzinduzi huo waumini mbalimbali watajionea viongozi hao ambao wanaongoza makanisa mbalimbali hapa nchini.
Mwakasaka alizitaja nyimbo zilizoko kwenye albamu hiyo ni pamoja na Mubhopeghe Pa Finganilo, Lazaro, Ilisubha ‘Jua Linachomoza’, Yesu alipokwenda, Jesu Bho Ikufyuka ‘Yesu alipopaa’, Matendo, Gwe Kyala Mwikemo ‘Mungu Mtakatifu’ na Nasobhile ‘Nilikuwa nimepotea Msituni’

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG