Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Monday, December 22, 2014

Liverpool yaambulia sare kwa Arsenal

Liverpool na Arsenal zatoka sare
Liverpool, wakiwa uwanja wa nyumbani Anfield, wamenusurika kupata kichapo toka kwa Arsenal kwa kupata sare ya goli 2-2.
Mshambuliaji Philippe Coutinho alianza kuiandika Liverpool goli la kwanza, kabla ya Mathieu Debuchy hajaisawazishia Arsenal, Olivier Giroud akaongeza bao la pili dakika ya 64.
Beki Martin Skrtel alifunga bao la kusawazisha dakika za nyongeza za kipindi cha pili(90+7) kwa mpira wa kichwa uliomshinda kipa wa Wojciech Szczesny
Mshambulaiji Fabio Borini alitolewa nje baada ya kupewa kadi mbili za njano na kuwafanya liverpool kucheza pungufu.
Katika mchezo mwingine wa Sundeland walipata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Newcastle United.
Winga Adam Johnson ameibuka shujaa kwa kufunga goli pekee la ushindi kwa upande wa Sunderland, bao la dakika ya 90.
Katika mchezo huo beki wa Newcastle Steven Taylor alipata majeraha baada ya kupasuka eneo la jicho katika heka heka za kumzuia mshambuliaji Steven Fletcher.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG