Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Saturday, December 6, 2014

SERIKALI KUENDELEA KUNUFAISHA VIJANA KATIKA KUTENGENEZA AJIRA

JJJJJJ2JJJJ3JJJJJ1
Serikali imeahidi kuendelea kusaidia kuwajengea Vijana uwezo wa kujitambua na kufanya kazi kwa hari ikiwemo kujitolea.
Hayo yamebainishwa katika Hotuba ya Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara iliyosomwa kwa niaba yake na Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana wakati wa hafla ya madhimisho ya Siku ya Kimataifa yakujitolea iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Akihutubi baadhi ya Vijana wanaofanya kazi za Kujitolea katika taasisi mbalimbali Kajugusi amesema vijana wanapaswa kufanya kazi za kujitolea ili kujenga uwezo wa utendaji kazi na kupata uzoefu utakaopelekea kuajirika kwa ulahisi.
“Jengeni tabia ya kujitolea kwa kuwa kutawajenga na kuwapa fursa kubwa ya kupata ajira zenye staha zitakazo kidhi matarajio yenu”
Aidha Mkurugenzi huyo alitoa rai kwa vijana kujunga tabia ya kujifunza na kutumia kwa manufaa yao na taifa kwa jumla wake
Kajugusi aliongeza kuwa Serikali ipo mbioni kuboresha mkakati wa Taifa wa kushirikisha Vijana katika shughuli za maendeleo hapa nchini ambapo vijana watapa fursa ya kushiriki moja kwa moja katika kutekeleza mipango ya maendeleo ya nchi yao.
Kwa upande wake Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Matifa (UNIC) Bibi. Stella Vuzo amesema kuwa kadri vijana wanavyofanya kazi za kujitolea ndipo wanapopata fursa ya kujijengea uwezo utakapoelekea waajirike katika sjira zenye staha
Aliongeza kuwaidi ya vijana asilimia 80 wanajitolea katika taasisi mbalimbali duniani kote, ambapo kati yao asilimia 30 ujitolea ndani ya nchi zao hivyo kusaidia kuongeza nguvu kazi katika shughuli za maendeleo.
Akisoma ujumbe mahususi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon kwa ajili ya maadhimisho hayo, Bibi. Vuzo alisema kuwa Katibu Mkuu huyo anawashukuru zaidi ya watu 6,300 wanaofanya kazi kwa kujitolea katika Umoja wa Mataifa na na 11,000 wanaojitolea kupitia Mtandao kwa kuweza kuwasidia zaidi ya mamilioni ya watu katika kufanya mabadiliko kwa kuwapa sauti katika maendeleo endelevu na jitihada za utunzaji wa amani duniani kote’Alisema Stella Vuzo.
Siku ya Kujitolea duniani uadhimishwa kila mwaka tarehe 5 Desemba duniani kote ambapo kwa Tanzania kitaifa maadhimisho haya yamefanyika jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG