Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Tuesday, December 16, 2014

Sijawahi panga matokeo : Herrera

Andre akiwa kazini.
Kiungo wa timu ya Manchester United Ander Herrera amesisitiza hajawahi kupanga matokeo ya mechi wakati akiichezea klabu Real Zaragoza.
Mhispania huyu ametajwa katika kundi la wanamichezo 41 wakiwemo wachezaji ,makocha na wakurugenzi katika uchunguzi wa kashfa ya upangaji matokeo kwenye ligi kuu ya Hispania.
Herrera ameandika katika ukurasa wake wa facebook.:Sijawahi na kamwe sintofanya chochote katika kupanga matokeo,naupenda mpira naamini katika mchezo wa haki nje na ndani ya uwanja:
Waendesha mashitaka wanadai fedha taslimu € 965,000 zililipwa kwa kocha Javier Aguirre na wachezaji tisa wa Zaragoza, ikiwa ni pamoja na Herrera, kabla ya mchezo wa La Liga mwishoni mwa msimu wa 2010-201.
Herrera aliondoka Zaragoza na kujiunga na timu ya nyumbani kwao ya Athletic Bilbao mwezi Agosti 2011, kabla ya kujiunga na Man United mwezi Juni 2014.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG