Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Saturday, January 24, 2015

KWELI MWISHO WA DUNIA UMEKARIBIA..EMBU ONA HUYU MCHUNGAJI ANAVYOMWOMBEA HUYU MAMA!



Wanawake MUNGU awasaidie sana Mjue kujenga Mahusiano binafsi ya karibu na MUNGU mwenyewe kuliko kutegemea sana kuombewa hovyo hovyo,Kisa tu Umeambiwa na Rafiki yako kwamba yuko Apostle flani ana Upako sana.
Ndio ni kweli mna Matatizo mengi yamewasonga yakiwemo Ndoa zenu Watoto wenu,Biashara zenu,na Kadharika,Na mara nyingi nia yenu ni kufunguliwa kwenye hivyo vifungo vinavyowasumbua.Na shetani yuko karibu sana nanyi kwasababu anajua Nguvu iliyomo ndani yenu, ila wengi wenu hamjielewi.Ndio maana Mnafanyiwa vitu vingi sana kwa jina la kukombolewa na baadhi ya Watumishi kwa imani kwamba Mtapona.Na ndio maana kila huduma maombezi Mmejaa nyie na Ndio maana inakuwa rahisi sana kwenu kudhurumiwa mambo mengi kwa kujenga imani kubwa sana kwa watu kuliko BABA yenu.

Hebu tazama picha kama hii,Mumeo akikukuta unafanyiwa Maombi ya Staili hii "Atakuelewa kweli!?
 
Jifunzeni kumlilia MUNGU vyumbani mwenu na Mkumbusheni ahadi zake juu ya Maisha yenu na vizazi vyenu.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG