Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Saturday, January 24, 2015

Ligi kuu Tanzania kuendelea Jumamosi

Timu kadhaa kujitupa uwanjani Jumamosi ligi kuu Tanzania
Ligi kuu ya Tanzania itaendelea Jumamosi hii huku mechi kadhaa zikichezwa ikiwemo ile kati ya bingwa mtetezi na wawakilishi wa nchi katika michuano ya klabu bingwa Afrika, Azam FC na Simba Sports Club ikiwa chini ya kocha Mserbia, Goran Kopunovic.
Azam inaongoza ligi ikiwa na pointi 20 na baada ya mechi yao na Simba itaenda Jamhuri ya Kongo (DRC) kwa ajili ya kucheza mechi za majaribio kwa ajili ya mechi yao na vigogo wa Sudan, El-Merreikh katika mechi ya kwanza klabu bingwa Afrika itakayochezwa Dar es Salaam kati kati ya mwezi ujao.
Mabingwa wa zamani wa Tanzania na wawakilishi wa nchi katika michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika, Yanga, ikiwa ya nne katika msimamo na alama (points) 15, watacheza na Polisi Morogoro wakati Mtibwa Sugar, ikiwa ya pili na alama 17, watacheza na Ruvu Shooting.
Mechi nyingine ni kama ifuatavyo
Stand United vs Coastal Union-Uwanja wa Kambarage,Shinyanga
Kagera Sugar vs Ndanda-Uwanja wa Kaitaba, Kagera
Mbeya City vs Tanzania Prisons-Uwanja wa Sokoine, Mbeya

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG