Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Tuesday, February 3, 2015

TEMEKE yatwaa ubingwa TAIFA CUP

Timu ya Temeke ikipokea hundi
Chama cha kandanda mkoa wa Dar es salaam DRFA, kimeipongeza timu ya Temeke kwa kutwaa Ubingwa wa Taifa Wanawake,baada ya kuifunga Pwani kwa bao 1-0,kwenye mchezo wa fainali uliopigwa jumapili ya Januari 31 kwenye dimba la Azam Complez huko Chamazi.
Katika fainali hiyo iliyohudhuriwa na waziri mwenye dhamana ya michezo Dk.Fenella Mukangara,imeshuhudiwa Temeke ikijipatia bao lake mnamo dakika ya 66 kupitia kwa mchezaji wao Neema Paul.
Temeke walifanikiwa kutinga hatua ya fainali baada ya kuwafunga ndugu zao Ilala kwa mabao 4-0,huku pwani wakitinga hatua hiyo kwa kuifunga Kigoma mabao 3-2,katika michezo ya nusu fainali.
Mshindi amejinyakulia kitita cha shilingi milioni tatu, makamu bingwa sh. milioni mbili, wakati mshindi wa tatu ameondoka na sh. milioni moja katika michuano hiyo.
Mbali na Temeke kubeba ubingwa huo,pia imefanikiwa kutoa mlinda mlango bora, Belina Julius aliyezawadiwa kitita cha shilingi 500,000/-.
Mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu uliwakutanisha, Ilala dhidi ya Kigoma ambapo ilala imefanikiwa kuchukua nafasi ya tatu baada ya kushinda mabao 3-0.
Uongozi wa DRFA,unatoa shukurani kwa mashabiki wa mkoa wa Dar es salaam na maeneo ya jirani,ambao wamejitokeza kwa wingi kushuhudia michuano hiyo,na kuwaomba waendelee na mfumo huo ili kuleta hamasa kwa wachezaji.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG