Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Wednesday, March 4, 2015

Ligi kuuTanzania Bara kuanza Jumatano

Timu ya Mtibwa Sukari
Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea kutimua vumbi katika viwanja vitatu tofauti siku ya Jumatano.
Mkoani Morogoro katika uwanja wa Manungu-Turiani , wenyeji timu ya Mtibwa Sugar (wakiwa na pointi 19)watawakaribisha majirani zao, timu ya Polisi Morogoro.(nao wakiwa na pointi 19).
Katika uwanja wa Azam Complex – Chamazi, uliopo kando kidogo ya Dar es Salaam, maafande wa JKT Ruvu watawakaribisha maafande wenzao timu ya Tanzania Prisons kutoka jijini Mbeya, huku timu ya Ruvu Shooting wakiwa katika Uwanja wa nyumbani Mabatini – Mlandizi, mkoa wa Pwani kuwakaribisha timu ya Ndanda FC.
Yanga inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 31, huku mabingwa watetezi, Azam Fc wakifuatia wakiwa na pointi 27

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG