ETOILE du Sahel jioni hii imefanya mazoezi uwanja wa Taifa Dar es salaam kujiandaa na mechi ya kesho dhidi ya Yanga itayopigwa uwanja huo.
Hiyo itakuwa mechi ya kwanza ya hatua ya 16 ya kombe la Shirikisho na mchezo wa marudiano utapigwa nchini Tunisia baada ya wiki mbili.
Kocha wa Etoile, Faouzi Benzarti amesema hakuna kipya katika soka na wataingia kucheza soka la kawaida kwa kuwa hawakupata taarifa za kutosha kuhusu Yanga kutokana na ufinyu wa muda.
Add caption |
No comments:
Post a Comment