Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Tuesday, April 28, 2015

WALIOFARIKI KWA TETEMEKO LA ARDHI HUKO NEPAL YAFIKIA 4000, MAJERUHI 8000,PICHA ZIKO HAPA


Utawala nchini Nepal unasema kuwa watu zaidi ya watu 4000 wamedhibitishwa kuaga dunia huku wengine 8000 wakijeruhiwa kwenye janga la tetemeko la ardhi lililosababisha uharibifu mkubwa siku ya Jumamosi. 
Tetemeko hilo lilikuwa na ukubwa wa kipimo cha richta 7.8. 
Jitihada za uokoaji zinaendelea kukiwa na matumaini ya kuwapata manusura, lakini jitihada hizo bado hazijayafikia maeneo mengine yaliyo mbali.
Watu wengi walilala nje kwa usiku wa tatu mfululizo kwenye mji mkuu Kathmandu wakihofia kutokea kwa mitetemeo mingine midogo.
Serikali ya Nepal inasema kuwa inahitaji kila msaada ukiwemo wa mablanketi , helkopta, madaktari na madereva. Kuna uhaba wa maji , chakula na umeme huku kukiwa na hofu ya kutokea kwa milipuko ya magonjwa. 
Via>>BBC Angalia Picha hali halisi ilivyo 
Wafanyakazi wa uokozi kutoka Japan wakiwasili Kathmandu
Hali ya barabara

Watu wakiwa wamelala mitaani baada ya tetemeko la ardhi

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG