Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Saturday, May 30, 2015

Andy Murray asonga mbele French Open

Andy Murray asonga mbele mashindano ya French Open
Muingereza Andy Murray amezidi kusonga mbele katika mashindano ya French Open baada ya kutinga mzunguko wa tatu kwenye mashindano hayo pale alipomshinda Joao Sousa raia wa Ureno, kwa jumla ya set 6-2 4-6 6-4 6-1. Murry alianza mpambano huo akiwa vizuri na alibaki hivyo hadi mwisho, japo alionesha kupatwa na mshangao kutokana na ushindani mkali aliokutana nao kutoka kwa mpinzani wake huyo. Sasa Murray anataraji kuvaana na Nick Kyrgios kutoka Australia. "nilifurahi sana namna nilivyobadili mchezo na kuweza kufanya marekebisho pale uwanjani, ambapo upepo mzuri ukahamia kwangu" alisema Murray. Naye Muingereza mwingine Heather Watson, amegaragazwa na Mmarekani Sloane Stephens kwa set 6-2 6-4, huku Rafael Nadal na Novak Djokovic wakifanikiwa kusonga mbele kwenye hatua hiyo ya tatu.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG