Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Friday, June 12, 2015

Al Shabaab ladai kuwaua askari wa Ethiopia

Al shabaab
Kumekua na mapigano makali katikati mwa Somalia baina ya wanajeshi wa taifa hilo ,wanamgambo wa kiislam wa Alshaabab na wanajeshi wa Ethiopia
Al Shabaab linasema limewauwa askari 30 wa Ethiopia ambao ni sehemu ya kikosi cha muungano wa Afrika na kuharibu magari saba ya kijeshi .
Watu katika kijiji cha Jame kilichopo karibu na mji wa Bur Hakaba wanasema kuwa walisikia milio ya risasi.
Hakuna ripoti yoyote kutoka kwa serikali ya Ethiopia kufikia sasa.
Kundi la alshabaab limefurushwa katika miji mingi ya Somalia lakini bado linadhibiti maeneo mengi ya mashambani.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG