- Written by Tupambane blog
- Add new comment
-
Kwa mujibu wa tangazo la serikali Na 300 lililotolewa Agosti 22 mwaka huu na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) imeonyesha maoeneo hayo kwa baadhi ya mikoa ya Kanda ya Ziwa Mwanza ya Kagera, Shinyanga, Mara, Simiyu na Geita.
Mkoa wa Mwanza Wilaya ya Ilemela, Manispa ya
Ilemela, awali ilikuwa na Kata tisa za Kirumba, Kitangiri, Nyamanoro,
Pansiasi, Ilemela, Sangabuye, Bugogwa, Nyakato na Buswelu ambapo Kata 11
mpya zilizoongezwa baada ya kugawanywa kutokana na mapendekezo ya
Manispaa hiyo yaliyowasilishwa TAMISEMI.
Alizitaja Kata 11 mpya kuwa ni Kata za Mecco,
Buzuruga, Nyansaka, Ibungilo, Kiseske, Kayenze, Shibula, Kawekamo,
Kahama, Kiseke, Nyamhongolo jumla zikiwa na mitaa 172 ikijumuisha ya
zamani na mipya.
Wilaya ya Nyamagana, Halmashauri ya Jiji la
Mwanza, awali ilikuwa na Kata 12 za Nyamagana, Isamilo, Mirongo,
Mbugani, Pamba, Igogo, Mkuyuni, Butimba, Mkolani , Buhongwa, Mahina na
Igoma na mitaa 110 na sasa Kata mpya sita zimeongezeka baada ya
kugawanywa na kuundwa Kata za Luchelele, Lwanhima, Nyegezi, Mabatini,
Kishiri na Mhandu ambapo jumla zitakuwa 18 zenye mitaa 175.
Mkoa wa Mara, Wilaya Musoma Mjini, Manispaa
ya Musoma, iliyokuwa na Kata 13 na kufikia 16 ambazo ni Kata ya Bweri,
Rwamlima (mpya), Kigera, Kwangwa (mpya), Makoko, Mwisenge, Nyakato,
Mshikamano (Mpya), Buhare, Iringo, Kamunyonge, Kitaji, Mkendo,
Mwigobero, Nyamatare na Nyasho.
Wilaya ya Tarime, Halmashauri ya Mji wa
Tarime awali ulikuwa na Kata sita na baada ya kugawanywa zimeongezeka
mbili na kuwa jumla ya Kata nane ambazo ni Bomani, Nyamisangura,
Sabasaba, Turwa, Nkende (mpya), Kenyamanyori (Mpya) na Kitare ambazo
jumla zitakuwa na mitaa 73.
Mkoa wa Simiyu, Halmashauri ya Mji wa
Bariadi, awali haikuwa na mitaa wakati wa uchaguzi Mkuu 2010 hivyo baada
ya kuanzishwa sasa imepata mitaa 92 na kutoka katika Kata 10 zilizopo
za Bunamhala, Bariadi, Malambo, Nyangokolwa, Isanga, Sima, Somanda,
Guduwi, Nyakabindi na Mhango.
Mkoa wa Geita, Halmashauri ya Mji wa Geita,
ilikuwa na Kata saba za Kalangalala, Mtakuja, Kasamwa, Bung’wangoko,
Bulela, Nyanguku na Ihanamilo na sasa baada ya baadhi kugawanywa
zimeundwa Kata mpya tano za Buhalala, Nyankumbu, Bombambili, Mgusu,
Kanyala na kuwa na jumla ya mitaa 50 vijiji 13 na vitongoji 47 katika
mapendekezo yaliyopitishwa.
Mkoa wa Shinyanga, Halmashauri ya Mji wa
Kahama, awali ilikuwa na Kata sita za Kahama Mjini, Malunga, Zongomela,
Nyihogo, Mhongolo na Mwenda kulima ambazo baada ya kugawanywa zimefikia
Kata 20 ambapo Kata 14 mpya ni Nyandekwa, Majengo, Nyasubi, Nyahanga,
Busoka, Isagehe, Mondo, Kagongwa, Kinaga, Kilango Iyenze, Ngogwa na
Wendele ikatayokuwa na jumla ya mitaa 32, vijiji 42 na vitongoji 218.
Manispaa ya Shinyanga inazo Kata 17 ambazo ni
Kambarage, Lubaga, Chamaguha, Ibinzamata, Shinyanga Mjini, Ndala,
Masekelo, Kitangili, Ngokolo, Ndembezi, Mwawaza, Kizumbi, Ibadakuli,
Kolandoto, Old Shinyanga, Mwamalili na Chibe ambapo haikuwa na mitaa na
sasa mitaa 55, Vijiji 17 na Vitongoji 84 kwa mjibu wa mapendekezo
yaliyopitishwa na TAMISEMI.
Mkoa wa Kagera, Manispaa ya Bukoba inazo Kata
14 za Kashai, Bilele, Hamugembe, Miembeni, Bukoba Mjini, Ijuganyondo,
Kibeta, Kitendaguro, Nshambya, Rwamishenye, Buhembe, Nyanga, Kahororo,
Kagondo, ambapo iliwasilisha mapendekezo ya kuongeza idadi ya ya Kata na
mitaa lakini zimebaki kama ilivyokuwa 14 za awali na mitaa 66.
Mkoa wa Tabora, katika uchaguzi wa mwaka
2010 ilikuwa na Kata 28 na sasa imeongezeka Kata moja na kufikia 29
ambapo Kata za zamani ni Ipuli, Kitete, Chemchem, Mwinyi, Ng’ambo,
Kidongochekundu, kiloleni, Mapambano, Mtendeni, Malolo, Tambuka-Reli,
Isevya, Gongoni, Kanyenye, Mbugani, Cheyo, Ndevelwa na Kalunde.
Zingine ni Kata za Uyui, tumbi, Itonjanda,
Ikomwa, Ifucha, Kabila, Misha, Kakola, Itetemia na Ntalikwa ambapo sasa
imeongezeka Kata ya Mpela kufikia 29 ambazo zitakuwa na jumla ya mitaa
135, vijiji 32 na vitongoji 145.
Hatua hii inatokana na mapendekezo ambayo
yalipelekwa na baadhi ya vikao vya Halmashauri za Majiji, Manispaa na
Halmashauri za Miji kupitia Kamati za Ushauri za Mikoa (RCC) husika
ambapo TAMISEMI imelidhia na kupitisha ambapo sasa zitahusika katika
uchaguzi mkuu wa serikali za mitaa na Uchaguzi Mkuu wa Rais, Madiwani na
Wabunge mwaka 2015 kote nchini.
No comments:
Post a Comment