Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA
Showing posts with label marekiani. Show all posts
Showing posts with label marekiani. Show all posts

Tuesday, November 17, 2015

Marekani yakerwa na ziara ya Assad Moscow


Assad na Putin


Marekani imeshutumu Urusi kwa kumpa mapokezi ya taadhima Rais wa Syria Bashar al-Assad mjini Moscow.

"Tunatazama mapokezi ya zulia jekundu aliyopewa Assad, aliyetumia silaha za kemikali dhidi ya watu wake, kuwa kinyume na lengo lililoelezwa wazi na Urusi la kutaka kuwepo na shughuli wa mpito kisiasa Syria,” msemaji wa ikulu ya White House Eric Schultz amewaambia wanahabari.

Afisa wa wizara ya masuala ya ndani ya Marekani alisema taifa hilo halijashangazwa na ziara hiyo, lakini wasiwasi mkubwa kwa Marekani ni Urusi kuendelea kumsaidia kivita Assad.

Alisema hilo litaipa nguvu zaidi serikali ya Assad na hivyo kuendeleza mapigano ya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.

Ziara hiyo ya kiongozi huyo wa Syria Jumanne ilifanyika wiki tatu baada ya Urusi kuanza kushambulia kwa ndege ngome za wapiganaji wa Islamic State na makundi mengine yanayopinga utawala wa Assad.

Ilikuwa ziara ya kwanza kabisa kwa Assad nje ya nchi baada ya mapigano kuzuka Syria 2011. Mapigano hayo ya wenyewe kwa wenyewe yameua watu 250,000.

Akiwa jijini Moscow, Assad alitoa shukrani zake kwa Urusi kuingilia kati kijeshi nchini mwake.

Alisema operesheni hiyo ya Urusi ilikuwa imezuia ugadi kueneza zaidi na kuwa madhara makubwa Syria.

Kwa upande wake, Bw Putin alisema matumaini ya Moscow ni kwamba suluhu ya muda mrefu itapatikana kupitia mchakato wa kisiasa na kwa kushirikisha makundi yote ya kisiasa, kikabila na kidini.

Mwandishi wa BBC aliyeko Moscow Steve Rosenberg anasema kuwa kwa kumkaribisha kiongozi huyo wa Syria mjini Moscow, Putin alikuwa akituma ujumbe mkali kwa mataifa ya Magharibi kwamba Moscow ni mhusika mkuu katika mzozo huo Mashariki ya Kati na kwamba suluhu haiwezi kupatikana bila kuhusisha Urusi.

Tuesday, January 27, 2015

DHARUBA KUBWA YA THELUJI NA UPEPO MKALI YAPELEKEA KUSIMAMISHA HUDUMA ZA UMMA KASKAZINI MASHARIKI YA MAREKANI.


A plow truck clears snow off South Church Street, in Hazleton, Pennsylvania on Monday. The area received another three-inches of snow overnight
Lori maalumu la usafishaji likiondoa theluji iliondoka barabara ya South Church Street, katika mji wa Hazleton, Pennsylvania siku ya Jumatatu Jan 26, 2015. Photo via .dailymail.co.uk.
By Abou Shatry Washington DC 
Zaidi ya watu 60 million wataadhithika kutokana na kimbunga kikubwa cha upepo unaoambatana na unyeshaji wa theleji katika eneo la kaskazini mashariki ya Marekani.
 
 
Kwa mujibu wa kitengo cha hali ya hewa nchini Marekani, imetaja maeneo ambayo yataathiriwa na tharuba hiyo, ya kihistoria ambayo itapelekea zaidi ya watu kadhaa kukosa huduma ya umeme, pamoja na huduma za usafiri wa anga na nchi kavu.
Imetaja baadhi ya majimbo ambayo yatakumbwa na kimbunga hicho kuwa ni New York, New Jersey, Massachusetts, Connecticut na Rhode Island, ambapo viongozi wakuu wamajimbo hayo kutangaza hali ya hatari kwa tukio hilo ambalo litatokea siku ya Jumatatu, Jumanne na Jumatano.
Imetabiriwa kiasi cha unyeshaji wa theluji hiyo 36inches katika jimbo la New York 16 hadi 26 inches katika jimbo la Boston, na kiwango chengine kama hicho katika baadhi ya majimbo mengine.
Zaidi ya safari za ndege 3,800 zimesimamishwa mapema leo Jumaatatu katia viwavya vya ndege vya JFK, LaGuardia na Newark airports, pia huduma za shule kufungwa siku ya jumanne na jumatano katika majimbo hayo.

Tuesday, November 25, 2014

Waziri wa Ulinzi wa Marekani ajiuzuru


Chuck Hagel waziri wa ulinzi mstaafu wa Marekani
Waziri wa ulinzi nchini Marekani, Chuck Hagel,amejiuzuru nafasi yake hiyo akiwa ametumia muda wa chini ya miaka miwili kazini.
Rais Barack Obama ameielezea hatua hiyo kuwa ni ya kawaida, na kumsifu Hagel kwa uamuzi aliouchukua lakini pia kwa ushauri alokuwa akimpatia na tabia yake ya ukweli na uwazi kwa kipindi chote alichokuwa waziri wa ulinzi.
Lakini wachunguzi wa mambo mjini Washington wanaielezea sababu halisi ya kujiuzuru kwa waziri huyo wa ulinzi ni kushindwa kuingilia misimamo ya raisi Obama juu ya sera ya uhamiaji.
Mwandishi wa BBC mjini humo amemuelezea waziri Hagel ambaye ni M Republican kuwa alichaguliwa kuvirejesha nyumbani vikosi vya kijeshi vya nchi hiyo vilivyoko Afghanistan na nje ya hapo lakini bajeti yake ikakatwa.
Lakini changamoto hiyo inayolikabili taifa hilo kutokana na kitisho cha kikundi cha dola ya kiislam Is,mgogoro wa Syria na Urusi na uchokozi wa Ukraine inadhaniwa kuwa ni toufauti za kitaaluma na bwana Hagel ametakiwa kusalia madarakani mpaka hapo mrithi wake atakapoteuliwa na baraza la Seneti.

Saturday, September 20, 2014

Marekani:Iran ina jukumu dhidi ya IS


Waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani John Kerry amesema kuwa Iran ina jukumu la kutekeleza katika juhudi za kimataifa dhidi ya wapiganaji wa Islamic State nchini Iraq na Syria.
Bwana Kerry ameliambia baraza la usalama la umoja wa mataifa kwamba muungano wa kuliangamiza kundi hilo una majukumu mengine mbali na hatua za kijeshi na kwamba huenda Iran ikashirikishwa.
Wizara ya maswala ya kigeni nchini Marekani imebaini kwamba wawakilishi wa Iran na wale wa Marekani wamejadiliana kuhusu tishio linalosababishwa na wapiganaji hao kandokando ya vikao vya mkutano kuhusu mpango wa nuklia wa Iran.

Thursday, September 11, 2014

Marekani kupambana na Islamic State


  • Written by Tupambane   Blog
  • Email
  • Tuma Maoni
  • Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter 

Rais wa Marekani Barack Obama ametoa tamko kua hatasita kuchukua hatua stahiki dhidi ya kikundi cha wanamgambo wa dola ya kiislam huko Syria na Iraq.
Katika hotuba yake kwa taifa hilo ilooneshwa kupitia runinga ya taifa ameelezea mipango yake ya utekelezaji dhidi ya wanamgambo hao kua kikundi chochote cha kigaidi kitakachoitishia Marekani hakitakua salama milele.
Rais Obama pia amesema kwamba kikosi namba 475 watapelekwa Iraq ingawa hawatakua na jukumu lolote la kupambana na wanamgambo hao.
Inaelezwa kuwa kundi hilo la wanamgambo wa dola ya kiislam wanatwala eneo kubwa la Syria na Iraq,na wanamgambo hao wamegeuka kua hatari kwa matendo yao ya kuua watu kwa kuwakata vichwa waandishi wa habari kutoka ughaibuni huku ulimwengu ukishuhudi.
Marekani imesha fanya mashambulizi ya anga yapatayo
150 dhidi ya kikundi hicho cha Is na kugawanya silaha kwa wale wanakipinga kikundi hicho Iraqi vikundi vya ki Kurdi .
Katika hotuba yake hiyo ilodumu kwa muda wa dakika rais huyo amesema huu ni muda muafaka Marekani kuingilia kati na lazima Marekani itaongoza na kuwarejesha nyuma wanamgambo hao wa IS.
Akiizungumzia Iraq, amesema ataongeza nguvu za kulinda raia wa Marekani na kusambaza misaada ya kibinaadamu na tutaipiga Is .
Rais Obama amesema kwamba anakaribisha uungwaji mkono kutoka katika Bunge la Marekani lakini kwa mamlaka laonayo anayweza kuendelea na dhamira yake bila ruhusa ya bunge hilo.
Rais Obama alichaguliwa na chama chake cha Democrat kwasababu ya ari yake ya kupinga uvamizi katika nchi ya Iraq mnamo mwaka 2003 na kuongoza harakati za kuondoa wanajeshi wa Marekani nchini humo.

Wednesday, September 3, 2014

Obama kuongeza vikosi Iraq


 3 Septemba, 2014 - Saa 04:52 GMT
  • Google+
  • Chapisha na Tupambane
Rais Barack Obama
Rais Barack Obama wa Marekani ameidhinisha kupelekwa vikosi vya wanajeshi wapatao 350 kwa lengo la kuwalinda wanadiplomasia na wafanyakazi raia wa nchi hiyo waishio mji mkuu wa Iraq Baghdad.
Ikulu ya Marekani imesema wanajeshi hao watakaopelekwa baadhi yao ni wale wanaojihusisha na diplomasia ya ulinzi ya iraq ambao ni zaidi ya mia nane.
Hata hivyo Marekani inatarajia kuwatuma maofisa waandamizi akiwemo John kerry katibu mkuu wa marekani na Chuck Hagel katibu wa ulinzi ambao watakwenda mashariki ya kati katika harakati za kuimarisha ushirikiano.
Hatua hiyo inafuatia vitendo vya mashambulizi na mauaji yanayoendelea Iraq ikiwa ni matokeo ya utofauti kati ya Marekani na makundi ya wapiganaji ambao wamekuwa wakiwalenga raia wa Marekani waliopo nchini humo
TUPAMBANE BLOG