Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Tuesday, August 12, 2014

KIGAMBONI WAMKABA KOO WAZIRI TIBAIJUKA

Kigamboni wamkaba koo Waziri Tibaijuka

 Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile akizungumza kwenye kikao cha madiwani na watendaji wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kilichojadili malipo ya fidia kwa wakazi watakaopisha ujenzi wa mjini mpya wa Kigamboni. Kulia ni Waziri wa wizara hiyo, Prof Anna Tibaijuka. Picha na Rafael Lubava.      
Na Nuzulack Dausen, Mwananchi

Posted  Jumatatu,Agosti11  2014  saa 10:53 AM
Kwa ufupi
Pamoja na wito huo, viongozi hao walitaka mpango wa Serikali wa kuwataka wananchi kununua hisa za uendelezaji mji huo kwa asilimia 10 ya malipo ya fidia, uwe wa hiari na Serikali isiingilie uamuzi huo.

SHARE THIS STORYShare


Dar es Salaam. Viongozi wa Mji wa Kigamboni wamemtaka Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka kuharakisha malipo ya fidia kwa wakazi watakaopisha ujenzi wa mji mpya na kuacha mikutano ya hadhara isiyokuwa na tija.
Pamoja na wito huo, viongozi hao walitaka mpango wa Serikali wa kuwataka wananchi kununua hisa za uendelezaji mji huo kwa asilimia 10 ya malipo ya fidia, uwe wa hiari na Serikali isiingilie uamuzi huo.
Wakizungumza jana katika semina maalumu kati ya Prof Tibaijuka na viongozi wa mji huo, viongozi hao walisema wakazi wao wamechoka kucheleweshewa malipo yao na kwamba hakuna mkutano wa hadhara utakaofanyika kabla ya masilahi kutimizwa.
Diwani wa Kata ya Kibada, Juma Nkumbi alisema tatizo la uendelezaji mji huo lipo wizarani na si kwa wananchi, kwani wakazi wa maeneo ya Kibada na Uvumba walishakubali kupisha ujenzi huo.
“Asilimia 90 ya wakazi Uvumba na Kibada wako tayari na walishafanyiwa tathmini na kupata mrejesho wa fidia zao, lakini sasa ni mwaka na miezi sita hakuna aliyelipwa,” alisema Nkumbi na kuongeza:
“Natoa tahadhari... kusubiri sana bila mafanikio ni hatari.”
Awali, katika semina hiyo Prof Tibaijuka aliwasihi viongozi hao kuwaeleza wananchi wao umuhimu wa kununua hisa za taasisi itakayowekeza uendelezaji wa mji huo ili wawe sehemu ya wamiliki.
Alisema kuwa hatapenda kuona wakazi wa eneo hilo wakihama mji na kushuhudia watu wa nje wakinufaika na eneo hilo aliloliita “dhahabu” ya miaka ijayo.
“Itapendeza kama wananchi watakubali kukatwa asilimia 10 ya sehemu ya fidia yao ili iwe malipo ya hisa za kumiliki mji huu. Nitaonekana nimeshindwa, iwapo wananchi watachukua fidia na kuondoka kwenye ardhi ambayo itakuwa dhahabu,” alisema Prof Tibaijuka.
Hata hivyo, Mbunge wa Kigamboni Faustine Ndungulile alisema suala la hisa liwe hiari na serikali iweke bayana ni taasisi ipi na namna gani itawekeza fedha hizo ili iwapatie faida wakazi hao.
“Waziri naomba uwajibu wananchi masuala hayo na kama hautaweza mimi sitakuunga mkono hata kidogo. Ni lazima wananchi 2800 wanaosubiri fidia zao wayajue haya,” alisema.
Ndungulile alionekana kutoridhishwa na sehemu kubwa ya utekelezaji wa mradi wa mji mpya alisema wananchi hao wamechoka na maneno matupu ya serikali bila ya kuwa na fedha za kutosha

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG