Ndugu zangu,
Maishani wengi wetu tumetongozwa, iwe kwa mwanammke au mwanamme.
Juzi hapa nikiwa kwa Bi Mkora pale Msamvu, akanilalamikia hili, kuwa siku hizi ameanza kutongozwa na hata ambao hakuwadhania.
Ama , makubwa hayo. Lakini, akaniomba nimpe tafsiri ya jambo hilo.
Nikamjibu,
kuwa mwanadamu ukianza kuona unatongozwa na wale ambao hukuwadhania,
basi, uanze kwanza kujitathmini, maana, kuna mawili;
Ama,
ulivyo sasa na mwenenendo wako, ikiwamo staili yako ya maisha, na hata
mavazi yako, yamewafanya wale ambao hukuwadhania , kuanza sasa
kukutongoza, au, kwa mabadiliko hayo, wale ambao walikuwa wakikutongoza
zamani wameacha sasa kukutongoza, na kuwa sasa unatongozwa na wapya
wenye kuvutiwa na mabadiliko hayo yenye kukuhusu wewe.
Lililo
jema kwa mwanadamu, ni kwa wale waliokuwa wakikutongoza zamani
kuendelea kukutongoza, na juu ya hapo, ukapata watongozaji wapya. Hivyo,
personal transformation ( Mabadiliko binafsi) uliyoyapitia yatakuwa
yamefanikiwa.
Na
katika hili unaweza kuzama kifikra. Ukaangalia hata kwenye chama cha
siasa. Kama chama cha siasa kitaanza kukimbiwa na wale waliokuwa
wakikimbilia zamani, na kupata wakimbiliaji wapya, basi, hapo kuna
tafsiri kama ya hapo juu. Nacho kitahitaji kujitathmini.
No comments:
Post a Comment