Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Wednesday, August 27, 2014

WAZAZI IRINGA WAASWA KUWASOMESHA WATOTO WA KIKE


  • Written by Tupambane  Blog
  • Email
  • Tuma Maoni
  • Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter

     

Mbunge wa Viti Maalum mkoa wa Iringa(CCM) Rita Kabati akizungumza na wanawake viongozi wa chama hicho hawapo pichani.

Baadhi ya wanawake walihudhuria mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyofanyika katika ukumbi mdogo wa ccm mkoani Iringa. (Picha na Denis Mlowe)


Na Denis Mlowe,Iringa
WANAWAKE mkoani Iringa wameshauriwa kuwasomesha watoto wako bila kukata tamaa kwa faida ya familia na nchi kwa ujumla. FRIDAY SIMBAYA
Wito huo umetolewa na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa (Ccm), Rita Kabati wakati akizungumza na viongozi wanawake wa ccm mkoani hapa katika semina ya mafunzo kuwajengea uwezo katika kujiandaa uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.
Alisema kuwa imekuwa kasumba ya mabinti wengi kukimbilia mijini na kuacha masomo ambayo yangewasaidia katika maisha yao ya mbele na familia.
Aliwataka wanawake kushirikiana katika malezi ya watoto hasa wa kike kwa kuwapelaka shule kwa malengo ya kusaidia taifa na Familia kwa jumla hivyo upendo na ushirikiano ni jambo .
Kabati amewaasa wazazi kuipa kipaumbele suala la elimu na kuwaeleza kuwa wasichague kuwasomesha watoto wa kiume na kuwaacha watoto wa kike na kuwaona kuwa wao ndio wanaoweza kuwasaidia wazazi kuliko watoto wa kiume
"Watoto wanahitaji elimu iliyobora hivyo watoto wanakuwa katika misingi iliyo bora na wanawake wahakikishe wanalea katika maadili ya kanisa kuweza kupata misingi bora ya maisha kwa vizazi vijavyo." Alisema Kabati
Aidha aliwataka wanawake kuombea amani kwa lengo la kupata katiba iliyokuwa bora na yenye kuondoa utegemezi na kumkandamiza mwanamke.
"Kila mtu kwa nafasi yake mtii mungu kuweza kufanikisha malengo yake hivyo kushikamana kwa pamoja katika kuweza kupata katiba iliyo bora na ninawapongeza kwa kuweza kudumisha amani na upendo katika mkoa wa Iringa" alisema Kabati

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG