Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Sunday, September 14, 2014

JOTO LA MECHI YA NGAO YA JAMII LAZIDI KUONGEZEKA

  • Written by  Tupambane Blog
  • Email
  • Tuma Maoni
  • Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgEZ91gbtN6j1WH200g7ZfN6NVn8v8UJGTZuq2LdnQ-AyyKhMmpN09q1rhMcMTlaySN5dJx-3VsPjaEqPGOSg607yqD8VRgBz3-imbs_bXr3z5arhhMvkAha2AQQkcO8u-4ibTOsXh3E26H/s640/Yanga+Vs+Azam.JPG

NA THOMMY KUNDY TUPAMBANE.BLOG
Mechi baina ya Azam na Yanga kuwania ngao ya jamii kuashilia ufunguzi wa ligi kuu Tanzania bara,inachezwa septemba 14 mwaka huu. Awali mechi hiyo ilikuwa ichezwe septemba 13 lakini Shirikisho la soka la Tanzania TFF,likasogeza mbele mchezo huo kwa sababu mbalimbali.
Mechi hiyo inasubiriwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa soka wa hapa nchini,kutokana na maandalizi ya timu hizo.Timu ya soka ya Yanga kujiandaa na mechi hiyo pamoja na ligi kuu,waliweka kambi kisiwani Zanzibar ambako walicheza mechi kadhaa za kujipima ubavu.
Huku timu ya Azam wakiwa hawana muda mrefu tangu watoke nchini Rwanda ambako walishiriki kwenye michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na kati maarufu kama kombe la kagame.Kwenye michuano hiyo timu ya Azam waliishia kwenye hatua ya robo fainali baada yakutolewa na timu ya El Merreikh ya Sudani kwa changamoto ya mikwaju ya penati.
Tayari shirikisho la soka Tanzania TFF, limetangaza viingilio kwenye mechi hiyo ambavyo ni kuanzia sh 5000 mpaka 30000.Tayari joto la mechi hiyo limeishaanza huku kukiwa na tambo za hapa na pale kutoka kwa timu zote mbili.
KILA LA HERI TIMU YA YANGA NA AZAM KUELEKEA MECHI HIYO

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG