(thommy kundy)
Yah:- kusogezwa kwa tarehe ya mashindano ya ngumi ya taifa 2014
Shirikisho
la ngumi Tanzania (BFT) limesogeza tarehe ya kufanyika kwa mashindano
ya ngumi ya Taifa na sasa yatafanyika kuanzia tarehe
03-08/11/2014.Dar es salaam.
Awali mashindano hayo yalikuwa yamepangwa kufanyika tarehe
08-14/10/2014 Dar es salaam.
Sababu za
kusogeza mashindano hayo ni kuyapisha mashindano ya ngumi ya kimataifa
yaliyoandaliwa na chama cha ngumi wilaya ya Temeke yanayotarajia kuanza
kufanyika mwishoni mwa mwezi huu, lakini pia ni kutoa nafasi zaidi kwa
mikoa ili kujiandaa vizuri na kufanya mashindano ya kuwapata wawakilishi
wa mikoa yao katika mashindano ya taifa.
BFT
tunawataki maandalizi mema na tunatoa wito kwa maafisa michezo wa mikoa
yote ya Tanzania bara kuhakikisha wanaleta wachezaji kutoka katika mikoa
yao ili kuleta upinzani utakaopelekea kupata timu ya taifa iliyo bora
kutoka katika mikoa yote ya Tanzania bara.
Aidha BFT
inawapongeza kampuni ya simu za mkononi ya Z antel kwa udhamini wa
mashindano hayo kwa kutoa kiasi cha Tsh. 10,000,000/=ambazo zitasaidia
baadhi ya mahitaji ya msingi ya kufanikisha mashindano hayo.
Natanguliza shukrani.
Makore mashaga
KATIBU MKUU
No comments:
Post a Comment