Waziri wa
Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
(SMZ),
Mohamed Aboud Mohamed amesema Katiba inayopendekezwa, itaibeba
CCM katika
uchaguzi mkuu ujao visiwani humo.
Akizungumza
katika mahojiano maalumu bungeni jana, Aboud alisema katiba hiyo
itawasaidia katika kujibu kero mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwani
imejibu
asilimia 90 ya kero hizo.
"Kwa
asilimia zaidi ya 90 kero za muda mrefu za wananchi wa Zanzibar
zimejibiwa.
Kwa hiyo wananchi watajua kuwa tumeshughulika na kero zao
kwa kuzipatia
ufumbuzi,"alisema.
Aboud
alisema watakwenda kwa wananchi wa Zanzibar wakiwa kifua mbele
kufafanulia kero ambazo zimetafutiwa ufumbuzi na wajumbe wa Bunge la
Katiba, wengi wao wakitokana na CCM.
"Mimi
ninaamini kuwa wananchi wakipelekewa Rasimu ya Katiba hii
inayopendekezwa na wakaiona kuwa imekidhi matakwa yao wataiunga
mkono,"alisema Aboud katika mahojiano hayo.
Aeleza kuhusu urais 2015 (t.k)
Waziri
huyo ambaye aliwahi kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar mara mbili
(mwaka 2000 baada ya Dk Salmin Amour kumaliza muda wake na mwaka 2010
wakati Amani Abeid Karume alipokuwa akiondoka madarakani), alisema
hatagombea tena nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015.
"Sina nia wala dhamira ya kugombea tena urais. Mimi dhamira yangu kubwa
ilikuwa ni kuiunganisha Zanzibar kazi ambayo Rais aliopo (Dk Ali Mohamed Shein)
ameifanya vizuri,"alisema.
Aboud alisema sifa ya Rais ni uadilifu na kuwaunganisha Wazanzibari na
Watanzania kwa jumla, sifa ambazo zote amekuwa nazo Rais wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar Dk Shein. Hata hivyo, alisema kazi yoyote
inayofanywa na mwanadamu inakuwa na upungufu, haiwezi kuwa kamili.
"Mimi nina uhakika matarajio ya Wazanzibari yamepata majibu katika
Rasimu hii ya Katiba. Na ninaamini kuwa wataipokea vizuri. Lazima
tufahamu kuwa Katiba ni mchakato," alisema.
Aboud alisema kama kuna jambo ambalo hawakulipata katika mchakato
wa sasa wa Katiba unaomalizika Oktoba 4 au hawakufikia mwafaka ,
kesho wanaweza kupata nafasi ya kulizungumza.
Alipoulizwa kero zilizopatiwa ufumbuzi katika Katiba hiyo, Aboud aliitaja
kero ya mafuta na gesi ambapo sasa Zanzibar itakuwa na uwezo wa kushughulikia.
"Zanzibar sasa itaweza kutunga sheria na sera zake za kushughulikia mafuta
na gesi, lingine lilikuwa ni ushiriki wa Zanzibar katika taasisi za
kimataifa," alisema Aboud.
Alisema Rasimu imetoa haki ya Zanzibar katika mikopo na imetoa fursa ya
kupunguzwa kwa mambo ya muungano ambayo ilikuwa ni sehemu ya kero
ya Wazanzibari.
Ukawa kuondoka bungeni
Aboud alisema Ukawa na wajumbe wanaotokana na CUF, kususia Bunge hilo,
hiyo haitaathiri uendeshaji wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa kwa vile bado
wana umoja.
"Hawa walijitoa si kwa sababu hawaoni umuhimu wa Bunge la Katiba.
Walijitoa kwa sababu waliamini suala la serikali tatu ni suala la msingi.
Sisi tumeona mfumo wa Serikali mbili ndiyo utakaodumisha muungano,"
alisema na kuongeza:
"Sisi tumejali sana masilahi ya wananchi, sasa wao pengine wamejali sana
masilahi yao. Sisi tumeona kuwa mfumo wa serikali mbili ndiyo utaweka
msingi wa muungano."
Alisema pengine CUF wamejali sana faida watakazopata kutokana na mfumo
wa serikali tatu.
"Wanajua wao kwa nini wanataka mfumo wa Serikali tatu. Lakini kwa mimi na
imani kabisa serikali mbili ndiyo njia sahihi," alisema Aboud.
(mwaka 2000 baada ya Dk Salmin Amour kumaliza muda wake na mwaka 2010
wakati Amani Abeid Karume alipokuwa akiondoka madarakani), alisema
hatagombea tena nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015.
"Sina nia wala dhamira ya kugombea tena urais. Mimi dhamira yangu kubwa
ilikuwa ni kuiunganisha Zanzibar kazi ambayo Rais aliopo (Dk Ali Mohamed Shein)
ameifanya vizuri,"alisema.
Aboud alisema sifa ya Rais ni uadilifu na kuwaunganisha Wazanzibari na
Watanzania kwa jumla, sifa ambazo zote amekuwa nazo Rais wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar Dk Shein. Hata hivyo, alisema kazi yoyote
inayofanywa na mwanadamu inakuwa na upungufu, haiwezi kuwa kamili.
"Mimi nina uhakika matarajio ya Wazanzibari yamepata majibu katika
Rasimu hii ya Katiba. Na ninaamini kuwa wataipokea vizuri. Lazima
tufahamu kuwa Katiba ni mchakato," alisema.
Aboud alisema kama kuna jambo ambalo hawakulipata katika mchakato
wa sasa wa Katiba unaomalizika Oktoba 4 au hawakufikia mwafaka ,
kesho wanaweza kupata nafasi ya kulizungumza.
Alipoulizwa kero zilizopatiwa ufumbuzi katika Katiba hiyo, Aboud aliitaja
kero ya mafuta na gesi ambapo sasa Zanzibar itakuwa na uwezo wa kushughulikia.
"Zanzibar sasa itaweza kutunga sheria na sera zake za kushughulikia mafuta
na gesi, lingine lilikuwa ni ushiriki wa Zanzibar katika taasisi za
kimataifa," alisema Aboud.
Alisema Rasimu imetoa haki ya Zanzibar katika mikopo na imetoa fursa ya
kupunguzwa kwa mambo ya muungano ambayo ilikuwa ni sehemu ya kero
ya Wazanzibari.
Ukawa kuondoka bungeni
Aboud alisema Ukawa na wajumbe wanaotokana na CUF, kususia Bunge hilo,
hiyo haitaathiri uendeshaji wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa kwa vile bado
wana umoja.
"Hawa walijitoa si kwa sababu hawaoni umuhimu wa Bunge la Katiba.
Walijitoa kwa sababu waliamini suala la serikali tatu ni suala la msingi.
Sisi tumeona mfumo wa Serikali mbili ndiyo utakaodumisha muungano,"
alisema na kuongeza:
"Sisi tumejali sana masilahi ya wananchi, sasa wao pengine wamejali sana
masilahi yao. Sisi tumeona kuwa mfumo wa serikali mbili ndiyo utaweka
msingi wa muungano."
Alisema pengine CUF wamejali sana faida watakazopata kutokana na mfumo
wa serikali tatu.
"Wanajua wao kwa nini wanataka mfumo wa Serikali tatu. Lakini kwa mimi na
imani kabisa serikali mbili ndiyo njia sahihi," alisema Aboud.
No comments:
Post a Comment