Rais wa TAHLISO akitoa maazimio ya mkutano mkuu uliofanyika kwenye chuo cha
RUCO(Picha na Thommy kundy)
NaThommy kundy
MIKOPO KWA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
Kwa
mujibu wa ripoti iliyotolewa na Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya
juu,kupitia Afisa Habari wake tareh 19 agosti 2014,Ni kwamba mpaka
kufika
tarehe 31 julai 2014,jumla ya waombaji 58,037 walikua wameomba
wameomba
mikopo.Bodi ya mikopo walitoa Takwimu kutokana na Bajeti finyu
kati ya
waombaji 58,037 wa mikopo,Bodi itatoa mikopo kwa waombaji 30,000
pekee
sawa (51%) ,na waombaji 28,037 sawa na 49% hawatapata
mikopo,Karibu nusu
ya waombaji wote watakosa mkopo ingawa watajiunga na
Elimu ya juu
MAAZIMIO YA MKUTANO MKUU WA TAHLISO
Mkutano
mkuu wa TAHLISO umeazimia kwamba wote walioomba mikopo
mwaka huu yaani
wanafunzi 58,037 wapewe mkopo wote kama tu watakua
wamedahiliwa na Tume
ya vyuo vikuu kuingia Elimu ya juu,Hili ni jambo la
dharura na tunaitaka
serikali kuhakikisha kufanya hivo kwani wote ni watanzania
wanaostahili
mgawanyo sawa wa keki ya Taifa
MATABAKA KATIKA KUTOA MIKOPO
Kumekua
na kitu kinachoitwa kozi kipaumbele na zisizo kipaumbele katika
utoaji
wa mikopo,Hili limeleta matabaka miongoni wa wanafunzi wa Elimu ya
juu
ambao wote ni watanzania,Nchi hii bado iko nyuma kiuchumi na
kimaendeleo,
Taifa linahitaji wasomi waliofuzu katika kada zao ili
kusukuma mbele maendeleo
ya Taifa,Nchi hii inahitaji wataalamu katika
Nyanja zote walimu,wahandisi,
wanasheria na wataalamu katika Nyanja zote
na sit u katika Uhandisi na
Udaktari pekee ingawa tunakiri kada hizi
zina upungufu(t.k)
MAAZIMIO YA MKUTANO MKUU WA TAHLISO
Mkutano
mkuu wa TAHLISO kwa niaba ya wanafunzi wote wa Elimu ya juu
umezimia
kuitaka serikali ihakikishe mikopo inatolewa kwa wanafunzi wote wa
Elimu
ya juu wa Taifa hili bila kujali kozi kipaumbele na
zisizokipaumbele.
Mkutano mkuu umezimia hili lianze kutekelezwa mwaka huu
wa masomo
yaani 2014/15,Yaani wanafunzi wote waliokatika Elimu ya juu
wapewe
mikopo,kudahiliwa kuingia Elimua ya juu kiwe ndicho kigezo cha
kupata
mkopo na si vinginevyo.
Mfano
tuna wanafunzi........... wa chuo cha Elimu ya Biashara(CBE) Dodoma
wanaoingia mwaka wa waliomba mikopo mwaka jana na wote
hawakupata,
Mkutano mkuu wa TAHLISO umezimia mfano wa wanafunzi hawa wa
CBE
na wote walio katika vyuo mbalimbali wapewe mikopo mwaka huu wa
masomo 2014/15
MIKOPO KATIKA ELIMU YA KATI
Wanafunzi
wanaosoma stashahada(Diploma) katika Taifa hili wote wamekua
hawapewi
mikopo kama ilivyo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu yaani vyuo
vikuu
wanaosoma Shahada.Elimu ya kati ndiyo injini ya maendeleo ya Taifa
lolote lile kwani katika ngazi hii Elimu ya Ufundi,Elimu ya awali ya
udaktari,
uuguzi,ufamasia,ugavi na nyingine hutolewa na wahitimu katika
ngazi hii wengi
huenda kufanya ngazi maeneo ya pembezeno mwa nchi ambayo
yamesahaulika na
yanahitaji msaada mkubwa wa wataalamu,yaani wengi wao
huenda kufanya kazi
vijijini waliko watanzania wengi na ambako hali ya
maisha ni duni,kutotoa mikopo
kwa wanafunzi hawa ni kudidimiza maendeleo
ya Taifa
MAAZIMIO YA MKUTANO MKUU
Mkutano
mkuu wa TAHLISO umeazimia kwamba serikali ihakikishe wanafunzi
wote
katika ngazi hii wanapewa mikopo kama ilivyo kwa wenzao walio katika
Elimu ya juu wanaosoma shahada katika kada mbalimbali
DHANA YA 100% YA MIKOPO KWA VYUO BINAFSI
Wanafunzi
wanaosoma katika vyuo vikuu vya Binafsi wamekua wahanga wakubwa
wa kitu
kinacoitwa 100% ya mkopo.Wanafunzi hawa ambao wengi wao ni wale
wanaosoma kada ya Afya yaani Udaktari,uuguzi,ufamasia na utaalamu wa
maabara
katika vyuo binafsi wamekua wanapewa sehemu ndogo tu ya gharama
halisi
wanazolipa huku wakiitwa wanapewa 100%.Wanafunzi katika vyuo vya
KCMC,
Chuo cha kumbukumbu ya Hubert
Kairuki(HKMU),CUHAS-Bugando,St.Francis
Ifakara,Chuo cha kimataifa cha
Tiba na Teknolojia(IMTU) wanalipa ada na
michango mikubwa sana ambao
wanalazimika kuongeza kiwango kikubwa
kikubwa kama michango binafsi huku
ikiwepo dhana ya kwamba wanapewa 100%.
Tunaitaka
serikali itoe 100% kwa wanafunzi hawa wa vyuo hivi ili dhana ya 100%
itekelezwe,kwani kwa sasa wanapewa kati ya 40% na 60% tu,ya michango
yote
vyuoni,wanalazimika kuongeza zaidi ya Milioni 5 mpaka Milioni 6
kama mchango
binafsi(self-contribution) kiwango ambacho ni changamoto
kubwa kwani wanafunzi
wamelazimika kuacha masomo kwenda kutafuta
fedha,kushindwa kufanya mtihani
na kushindwa kulipa gharama hizi kubwa.
MAAZIMIO YA MKUTANO MKUU WA TAHLISO
Mkutano
mkuu wa TAHLISO umeazimia,Tunaitaka serikali itoe 100% ya kweli
kwa
wanafunzi kwa vyuo tajwa hapo yaani rejea juu,Kuanzia mwaka huu wa
masomo hilo litekelezwe mara moja kabala wanafunzi hawarudi vyuoni.
KIWANGO CHA MKOPO
Kutokana
na kupanda kwa gharama za maisha kwa zaidi ya 100% hivyo
kupelekea
wanafunzi Mkutano mkuu wa TAHLISO umeazimia kuitaka
serikali kuongeza
kiwango cha fedha ya kujikimu kutoka Shs.75,000/-
kwa siku iliyopo sasa
Hadi kiwango cha Shs.15,000/- kwa siku.
CHANGAMOTO YA ADA VYUONI
Kwa kuwa
Tume ya vyuo vikuu(TCU) ndiyo imepewa mamlaka kisheria na
sheria ya vyuo
vikuu na.7,2005 kusimamia Elimu ya juu nchini,Na kwa kua
TCU ilisambaza
waraka kwa vyuo vyote tarehe 4 Julai 2014 kuvitaka
kutopandisha viwango
vya Ada,Mapaka pale Mfumo wa upangaji
Ada wa pamoja(student Unit Cost)
utakapoanza kufanya,na kwa waraka ule
na maelekezo yale yamekiukwa.
Mkutano
mkuu wa TAHLISO umeazimia kuitaka TCU kutoa waraka na
maelekezo mengine
kwa vyuo hivi ambapo nakala zitatolewa pia kwa
TAHLISO kuvitaka vyuo
hivi kufuata maelekezo ya Barua ya tarehe 4
Julai 2014 kwa vyuo
hivi,Barua iliyovitaka visitisha uongezwaji wa ada.
Kwani
Mkutani mkuu wa TAHLISO umetoa muongozo kwa wanafunzi
wote wa Elimu ya
juu katika Taifa hili kuhakikisha analipa kiwango cha Ada
ambacho hakina
ongezeko lolote tofauti kwani Hakuna chuo kilichoongeza
ada na Ongezeko
lile likapitishwa(approved) na Kamisheni ya TCU(TCU
Commission),TAHLISO
pamoja na wajumbe wa Mkutanio Mkuu pamoja na
wanafunzi wa vyuo wahanga
St.Francis Ifakara,KCMC,CUHAS-Bugando na
wanafunzi wote wa Elimu ya juu
kuhakikisha hakuna anayelipa ongezeko na
mwanafunzi yeyote
atakayesumbuliwa kwa ajili wanafunzi wa Elimu ya juu
wote wa Elimu ya
juu wataungana kumtetea kwani ni uonevu
MAFUNZO KWA VITENDO
Kumekua
na Baadhi ya wanafunzi ambao hawaendi kufanya mafunzo kwa
vitendo(Fieldwork) mpaka wanahitimu masomo.Mkutano mkuu wa TAHLISO
umeazimia Mwanafunzi yeyote wa Elimu ya juu anyetakiwa kwenda Field
kwa
mijibu wa Mtaala na kama Mtaala una makosa urekebishwe ili wanafunzi
wote wawezwe kwenda Field hatuwezi kua na wasomi na wataalamu ambao
hawajifunzi kwa vitendo wakiwa vyuoni.
Mfano
chuo Kikuu cha Dodoma kitivo cha SOCIAL SCIENCE AND
HUMANITIES,Tangu
mwaka 2011 wanafunzi hawa waliandamana
kudai kwenda field na
hawakusikilizwa na baadhi yao walisimamishwa
masomo,Mwaka huu fedha ya
field ilipelekwa kutoka Bodi ya mikopo
kwa ajili ya wanafunzi
hawa,Lakini baadaya ilirudishwa Bodi ya mikopo
kwa madai ilipelekwa kawa
makosa kwa kua wanafunzi hawa hawendi
kinyume kabia na mtaala.
Mkutano
Mkuu umeazimia wanafunzi wote wanaotakiwa kwenda field
kwa mujibu wa
mitaala na wale amabo mitaala yao ina makosa irekebishwe
na wote waende
field na wapewe fedha ya kujikimu huko kama ulivyo
utaratibu,Mwaka huu
ewa masomo Mkutano mkuu wa TAHLISO
umeazimia wana funzi wote wa
UDOM,College of Humanities and Social
Science kozi za Project Planning
na Law waende field kama ulivyoutaratibu
na si vinginevyo,TAHLISO
haitakubali pamoja na wanafunzi wote wa Elimu
ya juu kuona kuna
wanafunzi wote wakiwemo hawa wa UDOM haweandi
field,Bali Mkutano mkuu
umeazimia kwamba mwanafunzi yeyote wa Elimu
ya juu aende field kwa
matakwa ya mtaala(Carricullum) ya kozi anayosoma
KUHUSU QUALITY ASSURANCE
WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA TAHLISO KUKUTANA KWA
DHARURA NA WAZIRI WA ELIMU
Mkutano
Mkuu wa TAHLISO umeazimia mambo mawili makubwa,Moja:FAX
tayari imetumwa
leo asubuhi kwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr.Shukuru Kawambwa
kwa mambo mawili;
(1).Moja,Mkutano
mkuu wa TAHLISO umeazimia MAAZIMIO haya yafike
katika ofisi ya Waziri
wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuhusu kutekelezwa
kwa wakati muafaka
MAAZIMIO HAYA na tupate majibu yake ndani ya
masaa ishirini na nne(24).
(2).Pili,Mkutano
mkuu wa TAHLISO umeazimia kwamba katika FAX
iliyotumwa kwa waziri wa
Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Imeambatana na
kuomba kukutana(Appointment)
na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
siku ya jumanne,tarehe 30
septemba 2014 pamoja na Wajumbe wa Mkutano
ili kujadili mambo kadha wa
kadha yahusuyo wanafunzi wa Elimu ya juu.
USHAURI WA MKUTANO MKUU WA TAHLISO KWA SERIKALI YA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Mkutano
Mkuu wa TAHLISO umeazimia kuishauri serikali iyasimamie
yafuatayo ili
kuboresha mapato ya serikali ambayo yatapelekea Bajeti ya
Wizara ya
Elimu na Mafunzo ya Ufundi kua ya kutosha na Baadaye kupelekea
Bodi ya
mikopo kupata kiasi cha kutosha ili waombaji wote wa
mikopo waweze
kupata;
(1).Ukwepaji Kodi
(2).Misamaha ya kodi
(3)Mishahara hewa
(4)Ukusanyaji mzuri wa kodi
(5).Mkakati wa kufufua viwanda vilivyokuwapo tangu uhuru zaidi ya 400
(6).Fedha zinazokopwa na serikali zielekezwe kwenye shughuli za maendeleo
ili kuinnua uchumi wa Taifa
No comments:
Post a Comment