- Written by Tupambane Blog
- Tuma Maoni
-
Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter
Mashambulizi nchini Ukraine
Milipuko mikali imesikika katika mji wa Bandari wa Mariupol mashariki mwa Ukraine.
Waandishi walioshuhudia makombora hayo
wanasema kuwa kizuizi muhimu cha serikali kiliharibiwa na mashambulizi
makali kutoka kwa wapiganaji wanaounga mkono Urusi.Mji wa Mariupol unaonekana na wapiganaji wanaounga mkono Urusi kama muhimu katika barabara inayoelekea Crimea mbali na kuwa kitega uchumi cha eneo la Donbas iwapo litakuwa huru.
Mwandishi wa BBC katika mji huo amesema kuwa haijulikani iwapo mashambulizi hayo ni ya mda ama ni mwisho wa makubaliano ya kusitisha vita yalioafikiwa siku ya ijumaa.
Awali viongozi wa Urusi na Ukraine walisema kuwa wameridhika kuwa makubaliano hayo yanaafikiwa.
Rais Vladmir Putin na mwenzake wa Ukraine Petro Porishenko walizungumza kuhusu mwafaka huo kupitia njia ya simu.
Shirika la kimataifa la msalaba mwekundu limesema kuwa makombora yaliyalazimu malori ya misaada yaliokuwa yakielekea katika mji unaodhibitiwa na waasi wa Luhansk kurudi.
No comments:
Post a Comment