Mkurugenzi wa FBI James Comey
Mkurugenzi
mkuu wa FBI James Comey amesema kitengo chake kimemtambua mtu ambaye
huficha sura yake ambaye ni muuaji,ambaye pia huoneshwa wakati
akiwachinja mateka
watatu kwenye video inayo nadi wanamgambo wa dola ya
kiislam IS.
Pamoja na
hayo Bwana Comey amegoma kuutaja uraia wa mtu huyo ama hata kutaja
jina
lake,ingawa imeshajulikana lafudhi ya mtu huyo kuwa ni mwenye asili ya
mji wa
London, na Comey amesema kwamba utambuzi wa mtu huyo
umefanikishwa kwa msaada
mkubwa wa marafiki wa kimataifa.
Muuaji
huyo wa waandishi James Foley na Steven Sotloff pamoja na mfanyakazi wa
kujitolea David Haines walipigwa picha ya video na kuwekwa kwenye
mitandao na wanamgambo
hao wa dola ya kiislam na kusaidia kufanya
maamuzi juu ya mipango ya wapiganaji wa jihad
No comments:
Post a Comment