Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Thursday, September 11, 2014

MKOA WA DODOMA KUKABILIANA NA UPUNGUFU WA DAWA ZA BINADAMU



Na Mwandishi wa MAELEZO, Dodoma
Mkoa wa Dodoma unatarajia kuzindua Mradi wa Kuboresha na kuimarisha mfumo wa uuzaji na usambazaji wa dawa katika wilaya zote.
Hatua hiyo inalenga kuboresha na Kuimarisha Mfumo wa Afya ili kukabiliana na upungufu wa huduma za dawa katika Hospitali ,Vituo vya Afya na Zahanati katika Mkoa wote wa Dodoma.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo mjini Dodoma chini ya Mradi wa Tuimarishe Afya wa Uswis na Tanzania , duka mmoja la dawa litasaidia usambazaji wa dawa za binadamu inapotokea upungufu katika Bohari Kuu ya Dawa(MSD) .
Taarifa hiyo imetaja kuwa Duka la hilo ni Bahari la mjini Dodoma ambalo ndio limechaguliwa baada ya taaratibu za manunuzi kufuatwa , hatimaye kupewa jukumu usambzaji wa dawa katika Hospitali na Vituo vya Afya ili kukabiliana na upungufu wa dawa.
Mkoa wa Dodoma kwa kushirikiana na Mradi wa Kukuza na kuimarisha Mfumo wa Afya (HPSS) umeadhamiria kukabiliana na tatizo la upatikanaji wa huduma za dawa kwa wananchi kwa kutafuta duka la dawa litakalosaidia kusambaza na kuuzia wilaya zote endapo itatokea MSD hawana dawa zinazohitajika.
Taarifa hiyo imesisitiza kuwa hatua hiyo ni mwanzo wa juhudi mbalimbali za Serikali na wadau wengine za kukabiliana na upungufu wa dawa katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya kuboresha afya za wananchi na kuimarisha ustawi wa Taifa kwa ujumla.
Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa katika makubaliano huo wahudumu watatakiwa kuzingatia taratibu zote zinazosimamia huduma za uuzaji na usambzaji wa dawa ili kulinda afya za wananchi.
Uzinduzi wa mpango huo unaratajiwa kufanyika katika Hotel ya Dodoma kesho.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG