Blogger Widgets FURSA KWA VIJANA WOTE TUPAMBANE KWA KILA NJIA ILI MRADI TUWEZE KUEPUKA HUU UMASKINI TANZANI NA AMIN KILA ATAFUTAYE KWA NIA HUPATA MAANA ATA MAANDIKO HUSEMA PENYE NIA PANA NJIA

Tuesday, September 2, 2014

Msigwa atoa mifuko 100 Kata ya Nduli kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Sekondar

  • Written by  Tupambane Blog
  • Email
  • Tuma Maoni
  • Share on facebook Share on google_plusone_share Share on twitter 
Hii ndiyo Mifuko 100 iliyotolewa na Mbunge wa Iringa mjini Mch Peter Simon Msigwa
Mbunge wa Iringa mjini Mch Peter Simon Msigwa akizungumza na wakazi wa Nduli kabla ya kukabidhi mifuko 100 ya saruji


Na thommy kundy Moahi
Mbunge wa Iringa Mjini Mch Peter Simon Msigwa ametoa mifuko 100 ya Saruji kumalizia shule ya Sekondari Nduli ili kupunguza usumbufu mkubwa wanaoupata wananchi wa Kata hiyo kwani wanafunzi wamekuwa wakiteseka kusoma mbali na kijiji hicho.
Amesema kuwa tofauti za kisiasa kati yake na Diwani wa Kata hiyo zimemalizika badala yake ni muda wa kufanya shughuli za maendeleo.
Ameongeza kuwa waliosababisha kuchelewa kufika kwa fedha za mfuko ni wananchi wenyewe hivyo sio sehemu ya yeye kulaumiwa.
Akizungumzia kuhusu mifuko 100 iliyopelekwa kijijini hapo kabla ya leo kutoa mifuko hiyo, Msigwa amesema kuwa Chama cha Mapinduzi CCM kilitoa mifuko 100 ya Saruji baada ya kusikia kuwa anataraji kutoa Saruji hivyo wakaamini kwamba wamemzima kiutendaji kumbe wamewasaidia wananchi na sio kumkomoa yeye.
Hata hivyo wakazi wa kijiji hicho waliojitokeza wamesema kuwa hawatambui kuletwa mifuko 100 na CCM na kuhoji kama kweli imeletwa wafahamishwe mahali ilipo wasipo onyeshwa itakuwa ni kiini macho.
Msigwa amefikia uamuzi wa kuwapatia wananchi hao mifuko 100 baada ya kupata taarifa kwamba wananchi wanatakiwa kuchangia mifuko 15 aliamua kusitisha zoezi hilo la kuchangishana wananchi badala yake kuamua kutoa ili kutowakandamiza wapiga kura ambao ni hazina ya mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment

TUPAMBANE BLOG